UTANGULIZI
Geneviv ni binti mdogo ambaye amezaliwa katika familia yenye maisha mazuri sana.Mungu amemjaalia kuwa na sura nzuri yenye mvuto.Bahati mbaya kuzaliwa kwake akiwa na sura nzuri na urembo usio na kifani kunamfanya apate mateso makubwa sana kutoka kwa wanaume ambao kila mmoja akiwemo hata baba yake wanamtumia kimapenzi na baadae kumuacha akipata mateso makubwa mno.
Uzuri ambao Mungu alimjaalia unageuka kuwa sumu kali ambayo inammaliza taratibu mpaka anakaribia kupoteza uhai wake, akiwa katika hatua za mwisho kabisa za uhai wake.Ni mateso,maumivu, machozi,majeraha mtimani na kilio ndivyo vinavyotawala maisha yake.Anaichukia dunia,anawachukia wanaume…hawezi kulipa kisasi,anachoweza kufanya ni kutoa machozi muda wote,analia lakini hakuna anayemsikia! Anapokaribia kukata pumzi anasikia sauti ikimfariji…Shed no more tears Geneviv!
Ungana nami ufahamu mkasa mzima
SEHEMU YA KWANZA
Ilikuwa ni alfajiri tulivu,miale ya jua ikianza kuchomoza kwa mbali kuashiria mwanzo wa siku mpya,siku ya jumatatu.Milio ya ndege wa angani waliokuwa wakiimba na kurukaruka kutoka tawi moja hadi tawi jingine juu ya miti waliufanya mwanzo wa siku uwe wakuvutia sana.Jua lilikuwa likizidi kuchomoza huku nuru yake ikilifukuzia mbali giza la alfajiri.
Wakati kukizidi kupambazuka,upande wa pili alikuwepo binti mdogo aliyekuwa amejilaza chini ya mti mkubwa,mahali ambapo yamekuwa makazi yake kwa muda mrefu sasa,akishinda kutwa nzima akiwa amejilaza chini kivulini na giza likiingia alikuwa akilala na kujifunika kipande cha gunia palepale mpaka asubuhi.Mwili wake wote ulikuwa umejawa na vidonda vilivyokuwa vinatoa usaha na kumsababishia maumivu makali kupita kiasi.
Harufu kali ya majeraha yaliyokuwa yakiendelea kuuozesha mwili wake na harufu ya haja kubwa aliyokuwa anajisaidia hapo hapo, vilipafanya pale chini ya mti panuke mithili ya mzoga wa mnyama aliyejifia.
Binti yule mdogo hakuwa na msaada wowote,hakuweza hata kuinuka kutoka pale chini alipokuwa amelala…alichoweza ilikuwa ni kufumba na kufumbua macho na kufukuza nzi waliokuwa wakivizonga vidonda vyake.Alishakata tamaa ya kuishi na alionekana kama anayengojea pumzi yake ya mwisho ikatike aondokane na mateso makali yaliyokuwa yanamuandama.Kwake maisha yalipoteza maana kabisa,aliichukia dunia na vyote vilivyomo ndani yake.Mara kwa mara alikuwa akimkufuru Muumba wake kwa kumsababishia mateso makali kiasi kile kwani aliamini anateseka kwa sababu Mungu alimuumba akiwa mrembo kupita kiasi.
Aliamini anapata mateso makali kiasi kile kwa sababu ya uzuri wake aliopendelewa na Mungu,na huo ndio ulikuwa ukweli.Miaka michache tu aliyoishi duniani ilikuwa ni kama karne nzima kwani alipitia mateso makubwa sana ambayo kama angepata nafasi ya kuusimulia ulimwengu hakika kila mtu angemwonea huruma na kudondosha machozi.Aliendelea kuwaza akiwa amelala pale chini huku macho yake yakilitazama jua lililokuwa linazidi kuchomoza na kuanza kuwa kali.
Dunia aliiona kama shimo la hewa na zaidi aliwachukia wanaume.Aliapa kuwa kama angepata nafasi ya kulipa kisasi,angewateketeza wanaume wote duniani.Aliamini wanaume ni mashetani kwa waliyomfanyia na akazidi kukufuru dini kwa kumlaumu Mungu kwa kuwaumba wanaume.
“ I hate the world,I hate men…”
alijisemea Geneviv pale chini alipolala kwa sauti ya kunong’ona.
Kumbukumbu zake zilimrudisha nyuma alipokuwa bado mdogo.
Aliyakumbuka maisha ya furaha aliyoishi na familia yake kabla mambo hayajaanza kubadilika.Alishindwa kuyazuia machozi ambayo yalianza kuuloanisha uso wake mchanga uliochakazwa na mateso… soo many tears…hakika alitia huruma.
Geneviv alikuwa ni mtoto wa kipekee kwenye familia ya mzee Manuel Rwakatare na Bi. Patricia mahiza.Alizaliwa kwenye familia yenye uwezo mkubwa kifedha, baba yake akiwa ni Afisa utumishi katika wizara ya Madini na nishati huku mama yake akiwa Katibu Muhtasi katika ofisi ya waziri mkuu wa Nchini Blaziniar.Tangu anazaliwa maisha yalikuwa mazuri kupita kiasi huku wazazi wake wakijitahidi kumpatia kila alichokihitaji.
Waliishi kama wako peponi huku pesa kwao ikiwa sio tatizo.
Uzuri aliojaaliwa Geneviv ulianza kuonekana tangu akiwa mdogo hali ambayo ilizidi kuwaongezea fahari mzee Rwakatare na mkewe.Kila aliyemuona mtoto Geneviv alishindwa kujizuia kumsifia.Sura yake iliyokuwa na mchanganyiko safi wa baba na mama ulizidi kumfanya aonekane kama malaika…
“you have beared a very cute angel sir,congrats!”
(umezaa mtoto mzuri sana mzee,hongera sana)
Hiyo ilikuwa ni kauli kutoka kwa mmoja kati ya wafanyakazi wenzake mzee Rwakatare akimsifia kwa kuzaa mtoto mzuri kiasi kile.
Bi Patricia naye alikuwa akipokea sifa kila alipopita na mwanae hali iliyozidi kumpa kichwa na kumfanya ajione kama mama wa malaika.
”Atawasumbua sana vijana wa kiume akikua huyu,kama wewe ulivyonisumbua kipindi nakutafuta darling…”
Mzee Rwakatare alimtania mkewe wakati wakipata chakula cha jioni na mtoto wao Geneviv.Bi Patricia alitabasamu huku akimbusu mumewe shavuni.
Siku zikawa zinasonga kwa kasi huku Geneviv akizidi kukua na kupendeza zaidi, urembo wake ukizidi kujionyesha dhahiri hali iliyomfanya aonekane tishio mbele ya kila aliyemtazama.
Alipotimiza miaka saba wazazi wake wakaona bora wamuanzishe shule.Akatafutiwa shule nzuri yenye hadhi ya kimataifa, st Benard Blaziniar academy,shule iliyokuwa ikisifika kwa kutoa elimu bora kwa nadharia na vitendo.Baada ya taratibu zote kukamilika Geneviv akaanza shule.Aliahidi kwa wazazi wake kuwa atasoma kwa bidii mpaka afike chuo kikuu.
“I want to be a doctor daddy! I want to heal the world…”
(Nataka kuwa daktari baba,nataka kuuponya ulimwengu)
Geneviv alikuwa akimwambia baba yake asubuhi wakiwa ndani ya gari lao akimpeleka shule.
“Sure! Go for it and you can be what you you want to be”
(Hakika utakuwa kama unavyotaka kuwa ukijipangia malengo vizuri na kuyatekeleza)
Mzee Rwakatare alikuwa akimtia ujasiri bintiye kuwa anaweza kuwa daktari ikiwa atajiwekea malengo madhubuti ya kusoma kwa bidii.
“Let education be your only heritage daughter coz when everything has gone the future still remain dark”
(Ikazanie sana elimu ndio iwe urithi pekee maishani mwako, vitu vyote vitakapopita, maarifa yatabaki kuwa mwanga pekee wa maisha yako)
Baada ya kumfikisha shule,Geneviv alipokelewa na mwalimu na kuelekezwa utaratibu wa Shule.Ilikuwa ni furaha isiyo kifani kwa Geneviv kuanza shule.Alikuwa amechoka kufungiwa ndani kila siku,akaona huo ndio muda muafaka wa kuanza kufurahi na wenzake.Alijiwekea nadhiri ya kusoma kwa kadri ya uwezo wake wote ili azidi kuwafurahisha wazazi wake na kutimiza ndoto yake.
Baada ya siku chache tu tangu Geneviv ajiunge na Shule ya st Bernard Blaziniar, wanafunzi karibu wote na walimu walishamfahamu kutokana na uzuri aliojaaliwa.Wengine wakambatiza jina na kuanza kumuita “Cute Angel”. Usingepata shida kumtafuta kwani kila kona ya shule alifahamika. Akapata marafiki wengi huku wavulana anaosoma nao Grade one (darasa la kwanza) wakijigonga kila mmoja akitaka awe mchumba wake.
“Geneviv njoo tudimbedimbe mi niwe baba wewe uwe mama” aliongea mwanafunzi mmoja aliyeitwa Kim darasani na kusababisha darasa zima licheke.
Ukiacha uzuri na shani alivyokuwa navyo Geneviv,pia alitokea kuwa mwelewa “Bright” darasani hali ilyomfanya azidi kuwa kivutio kwa walimu wake na wanafunzi.
Kadri siku zilivyokuwa zinaenda mbele umaarufu wa Geneviv ukawa unaongezeka.
Nyumbani nako hali ilizidi kuwa shwari huku baba yake mzee Manuel Rwakatare na mkewe bi Patricia wakizidi kuonyeshana mapenzi motomoto. Amani na upendo vikazidi kutawala ndani ya familia ya mzee Rwakatare hali iliyozidi kumpa furaha Geneviv.Akawa anazidi kukua vizuri kimwili, kiakili na kiroho, kwani alifundishwa pia kumcha Mungu.
****
Katika kipindi hiki chote, baba yake alikuwa bado ni mfanyakazi wa wizara ya madini na nishati huku akipokea mshahara mnono na marupurupu yaliyomfanya aweze kuyamudu maisha ya familia yake kwa kiwango cha juu kabisa.Alianzisha vitega uchumi vingi nchini Blaziniar na katika nchi jirani ya Tanzania.Pamoja na kwamba alipata mshahara mkubwa na mke wake naye alikuwa akipokea mshahara mnono, bado siri ya utajiri wao uliokuwa unazidi kukua kila ilipoitwa leo haikufahamika.Kwa makadirio ya haraka ilitosha kusema kwamba mafanikio makubwa aliyokuwa nayo mzee Manuel Rwakatare yalizidi kipato chake halisi.
Mambo yakaanza kubadilika ofisini kwake mara baada ya Raisi mpya, mhe. James Kahungo “the JK”, kuingia ikulu ya Blaziniar.Raisi huyu mpya mwana mageuzi halisi aliwataka watumishi wote wa wizara zote nyeti kuorodhesha mali walizokuwa wanazimiliki na kueleza namna walivyozipata.
Tofauti na maraisi wengine ambao nao walikuwa wakitoa mkwara kama huo bila kusimamia utekelezaji, James kahungo alionyesha kudhamiria kiuhakika kuwapunguza wahujumu nchi.Miezi mitatu tu tangu aingie madarakani,watumishi zaidi ya mia tatu walisimamishwa kazi kwa kosa la ubadhirifu na kujilimbikizia mali kinyume na sheria ya nchi ya Blaziniar.
Kivumbi kikahamia kwenye wizara ya Madini na Nishati ambako uozo mkubwa ulifichuliwa wa hujuma nzito zilizokuwa zikifanyika.Mzee manuel Rwakatare, baba yake Geneviv naye akawa miongoni mwa waliokumbwa na Ufagio wa chuma.Alisimamishwa kazi baada ya kugundulika kuwa ameingiza hasara ya mamilioni ya pesa kwenye ofisi yake.Mahakama ikaamuru mali zake zote isipokuwa nyumba aliyokuwa anaishi zitaifishwe ili kufidia deni alilokuwa anadaiwa.
Ilikuwa vigumu sana kwa mzee Manuel Rwakatare kukabiliana na hali halisi.Alishazoea kucheza na mamiloni ya pesa,leo ghafla anafukuzwa kazi na mali zake zote kufilisiwa! hakutaka kuamini haraka kuwa ni kweli yamemkuta. Akaanza kuhangaika kwa waganga kutafuta ni nani aliyemloga bila mafanikio…akaanza pia kwenda kuroga usiku na mchana ili arudishwe kazini lakini wapi! Mwisho akajikuta akiishiwa mbinu. Mkewe bi Patricia akawa anajitahidi kumfariji mumewe na kumtuliza kwa maneno matamu lakini hgakufanikiwa.
“Mume wangu yote tumwachie mungu, mshahara wangu utatosha kutufanya tuishi vizuri na mwanetu atasoma bila shida, wewe kinachokuumiza ni nini? Calm down please my Huz, everything gonna be alright”
Bi patricia alikuwa akimbembeleza mumewe usiku baada ya kuona hali ya mumewe inazidi kuwa mbaya, chakula hali wala usingizi hapati.Pamoja na kujaribu kumfariji usiku kucha kila siku, bado haikusaidia kitu.Mzee Rwakatare alikuwa amekata tamaa kabisa…kila kitu kilipoteza maana kwake.Akaona njia bora ya kutoa mawazo na mfadhaiko ni kunywa pombe! Akaanza kidogokidogo kunywa pombe,kumbe ndio alikuwa anaongeza matatizo.
Maisha yakaanza kubadilika kwa kasi ya ajabu, kutoka kwenye umilionea hadi kwenye ufukara. Akiba ya Pesa zilizokuwa zimesalia akawa anazitumia kunywea pombe…”From Hero to Zero”
ndivyo wambea wa mitaani walivyoanza kumuita na kumbeza baada ya habari kuzagaa karibu kila kona ya nchi juu ya kufukuzwa kwake kazi.Ni katika kipindi hiki Geneviv alikuwa akijiandaa kufanya mtihani wa mwisho wa kuhitimu elimu ya msingi. Hakufahamu mara moja ni nini kimemtokea baba yake kwani muda mwingi alikuwa yuko shule akijiandaa na mitihani.
“Mama mbona dadii siku hizi haendi kazini?”
Geneviv aliuliza swali ambalo lilikuwa kama msumari wa moto kwa Bi Patricia. Ilibidi atumie uongo kumridhisha Geneviv kuficha aibu ya mumewe.
“Dadii yuko likizo mwanangu,ameamua kupumzika nyumbani”
Geneviv hakuridhika na jibu hilo lakini kwa jinsi alivyozisoma hisia za mama yake kwa haraka akajua lazima kuna kitu ambacho mama yake anamficha.Akauliza swali lingine ambalo nalo lilikuwa gumu…
“Lakini mbona siku hizi anachelewa sana kurudi nyumbani na akija anakuwa ananuka pombe…kwani ameanza lini kunywa Pombe? Mwalimu shuleni ametufundisha kuwa kunywa pombe ni vibaya na ni tabia hatarishi,sasa mbona baba ameanza kunywa?”
Geneviv alikuwa akiendelea kumshambulia mama yake kwa maswali mfululizo ambayo yote Bi. Patricia alishindwa kuyajibu.
“Basi mngoje akirudi umuulize mwenyewe maana mimi nashindwa kuyajibu.”
Alijitetea Bi Patricia na kabla hata hajamalizia ,wote walisikia mlango ukigongwa kwa nguvu,wakajua baba mwenye nyumba karudi.Geneviv akanyanyuka na kukimbilia mlangoni kwenda kumfungulia baba yake.
Tofauti na alivyozoea kumuona,mzee Rwakatare alikuwa tofauti kabisa,hali iliyomfanya Geneviv arudi nyuma kwa hofu…
“Whats wrong with you daddy?”
Aliuliza Geneviv kwa sauti iliyokuwa ikitetemeka kwa hofu.Mzee Rwakatare alikuwa amelewa kupita kiasi ,akishindwa hata kutembea vizuri kiasi cha kujiegemeza kwenye mlango kama mgonjwa,ile Geneviv anafungua tu mlango,mzee Rwakatare alidondokea kwa ndani na kuanguka sakafuni kama gunia …Puuh!
“Daddy! Are you sick? Mama njoo umuone daddy…”
alipaza sauti kwa nguvu Geneviv na kuanza kukimbilia ndani alikomuacha mama yake.Alikuwa ameshtuka kupita kiasi akidhani baba yake amepatwa na jambo baya.Hakujua kuwa Starehe ya pombe ndiyo iliyomfanya awe vile.
Hata kabla ya kumuona,Bi Patricia alishajua kilichomsibu mumuwe.Alichokifanya ni kumtuliza mwanae Geneviv ambaye alionekana kuchanganyikiwa,akampeleka chumbani kwake na kumsihi alale mpaka asubuhi na kumhakikishia kuwa baba yake hakuwa na tatizo lolote.Kweli Geneviv alikubali kulala kwa shingo upande huku maswali mengi yasiyo na majibu yakipishana kichwani mwake.
Baada ya kuhakikisha Geneviv ametulia Bi Patricia alirudi mlangoni na kumkuta mumewe akiwa bado palepale chini akikoroma kutokana na kuzidiwa na pombe.Kwa upole alimuinua na kumpeleka chumbani kwao.Alimvua nguo na kumpeleka bafuni ili angalau azinduke baada ya kuoga maji ya baridi.Kweli alifanikiwa kwani baada ya kummwagia maji mengi ya baridi Fahamu zilimrudia na pombe zikamuisha kichwani.Baada ya kumuogesha vizuri,Bi Patricia alimshika mkono mumewe na kumpeleka chumbani ambapo alimlaza vizuri na kumuacha apumzike.
Alipohakikisha kuwa kila kitu kimetulia Bi Patricia alienda chumbani kwa mwanae Geneviv.Alimkuta akiwa bado hajalala.Alikuwa amejikunja kitandani huku ameukumbatia mto wake.Aligundua namna mwanae alivyopatwa na mshtuko kwa kumuona baba yake katika hali ile.Akaamua kumfariji na kumfanya asahau kila kitu.Alianza kumfanyia utani kama walivyozoea kufanyiana kila siku na baada ya muda mfupi Geneviv alikuwa tayari ameshasahau yote yaliyotokea,wakawa wanacheka kwa furaha.
Kelele za vicheko zilimshtua mzee Rwakatare ambaye aliamka na kuanza upya kuvaa nguo.Japokuwa pombe ilikuwa imepungua lakini bado akili yake ilikuwa haijatulia.Alifikiri mkewe na mwanae wanamcheka yeye kwa sababu amelewa sana,kumbe haikuwa hivyo.Akajikuta hasira zikianza kumpanda na mara akainuka na kuanza kufoka kwa sauti. Bi Patricia aliposikia mumewe anafoka alitoka haraka na kumucha Geneviv akijiandaa kulala.Akawa anatembea kwa haraka kuelekea chumbani kwao, kabla hata hajafika akamuona mumewe akitoka kwa jazba chumbani.Wakakutana mlangoni…
”Mnachekacheka nini na mwanao? mnanicheka mimi sio? Sasa leo mtanijua!”
Aliongea kwa ukali mno mzee Rwakatare, akimfokea mkewe kama mtoto mdogo.Bi patricia alibaki ameduwaa akimshangaa mumewe.Tangu waoane karibu miaka kumi na tano iliyopita hakuwahi kumuona mumewe akiwa katika hali kama ile. Bila hata kusubiri mkewe ajitetee mzee Rwakatare akaanza Kurusha ngumi na mateke kama anapigana na mwanaume mwenzake.Mkewe akaamua kukimbilia chumbani bila ya kupiga kelele hata kidogo akihofia mwanae Geneviv angejifunza kitu kibaya.
Alipoingia chumbani alitaka kuwahi kujifungia kwa ndani lakini Mzee Rwakatare akamuwahi na kuusukuma mlango kwa nguvu.Akaingia na kuufunga mlango kwa ndani.Kilichoendelea humo ikawa ni kipigo mtindo mmoja.Bi Patricia alijitahidi kujitetea lakini wapi…baadae akaanguka chini na kupoteza fahamu baada ya kuzidiwa na maumivu huku damu nyingi zikimtoka puani na mdomoni.Baada ya kuona mkewe amedondoka na kupoteza fahamu,mzee Rwakatare akatoka na kuufunga mlango kwa nje.Akahamia kwenye chumba anacholala mwanae.
Kitendo cha Geneviv kumuona baba yake akiingia chumbani mwake kilimfanya moyo umlipuke kwa hofu.Alishasikia ugomvi uliokuwa unaendelea chumbani kwa wazazi wake, akajua sasa ni zamu yake.Tangu aanze kuwa na akili hakuwahi kupigwa hata kibao na baba yake,akabaki akisubiri aone kitakachomtokea.
Mzee Rwakatare baada ya kumuona mwanae akiwa amejawa na hofu kiasi kile,anajikuta nguvu zikimuishia na kuanza kumuomba msamaha mwanae.Geneviv alishindwa kuelewa nini lengo la baba yake na akabaki akimkodolea macho huku akishindwa kuificha hofu yake.Mzee Rwakatare akawa mpole ghafla na akasogea na kukaa karibu na geneviv juu ya kitanda chake.
Bado Geneviv akawa anatetemeka mwili mzima kiasi cha kufanya kijasho chembamba kimtoke na kuiloanisha Night dress ndogo aliyokuwa ameivaa.Dakika kama tatu zikapita huku wakiwa bado wanatazamana,mwishoni Geneviv alishindwa kujizuia na kumuuliza baba yake kwa sauti ya kutetemeka,
“Where is my mum,Why do you act like this to us?
(Mama yangu yuko wapi,kwanini unatufanyia hivi)
Kwa mara ya kwanza Mzee Rwakatare akaligundua kosa alilolifanya,akajikuta akikosa jibu la kumpa mwanae…akiwa bado anajikanyaga, Geneviv alimsukuma kwa nguvu na kukimbilia chumbani aliko mama yake,alipofika mlangoni akakuta mlango umefungwa kwa funguo, akawa anagonga kwa nguvu akimtaka mama yake amfungulie…akiwa bado anagonga,akaona kitu chini ya mlango ambacho kinamshtua mno.Aliona michirizi mikubwa ya damu ikichuruzika kupitia chini ya mlango kutoka ndani ya chumba alimo mama yake.Nguvu zikamuishia na taratibu akakaa chini na kuzigusa zile damu akiwa bado haamini.
“Dady, did you kill my mother? I hate you… “
Geneviv aliongea kwa sauti kubwa na kuanza kupiga kelele za kuomba msaada kwa majirani.Mzee Rwakatare akiwa amechanganyikiwa akatokea mlango wa nyuma na kutokomea gizani akielekea kusikojulikana.Geneviv akazidi kupiga mayowe yaliyowaamsha majirani ambao ndani ya muda mfupi walikusanyika kutaka kujua kumetokea nini.
Geneviv akisaidiana na majirani waliuvunja mlango na kufanikiwa kuingia chumbani ambako walimkuta mama yake akiwa amelala chini huku damu nyingi zikimtoka puani na mdomoni.Uso mzima ulikuwa umevimba kiasi cha kutotambulika…Geneviv akajikuta mwili wote ukimlegea akiwa haamini alichokiona, ghafla na yeye akaanguka na kupoteza fahamu.
****
Bi patricia alikuja kurudiwa na fahamu baada ya siku mbili.Alipofumbua macho tu,sauti ya kwanza kuisikia ilikuwa ni ya mwanae Geneviv aliyekuwa amekaa pembeni yake akilia huku akisali kwa sauti ya chini, ndani ya wodi ya upasuaji ya hospitali ya Planet Health Aid.
Kumbukumbu za matukio yote yaliyompata zilikuwa zimepotea kutokana na majeraha makubwa aliyokuwa ameyapata sehemu za kichwani na kifuani.
“Hapa ni wapi?” Aliuliza Bi Patricia huku akizishangaa dripu za maji na dawa zilizokuwa zinatiririka kuingia mishipani mwake.Kitendo cha kufumbua macho na kuuliza hapo ni wapi kilimshtua Geneviv aliyekuwa amezama kwenye kilio na Sala ya kumuombea mama yake.
“She is awake, Nurse Please come quick, my mother is back into her counciousness”
Aliongea Geneviv kwa sauti kubwa huku akiwa na furaha na akakimbia mpaka kwenye chumba cha nesi aliyekuwa anamhudumia mama yake.Sekunde chache baadae Geneviv alirudi akiwa ameongozana na nesi. Bi Patricia alikuwa bado akijaribu kukumbuka ni nini kilichomtokea mpaka akawa hapo.
Geneviv akawa anamshukuru Mungu kwa kumrejeshea fahamu mama yake huku machozi yakizidi kumiminika kwenye mashavu yake laini.Nesi alimtumliza Geneviv kwa kumwambia kuwa mgonjwa anahitaji kupumzika zaidi kwani alipata majeraha makubwa hivyo kelele zingemuongezea maumivu.Geneviv alielewa haraka na akatulia kimya akimtazama mama yake usoni alikokuwa amefungwa bandeji kubwa.
“Pole mum, My dad is a devil,I hate him…”
Aliongea Geneviv huku akimpiga busu mama yake.Hapo Bi Patricia akaanza kukumbuka yaliyomtokea mpaka akawa hpo hospitalini.Aliumia sana moyoni mwake, na kilichomuumiza haikuwa majeraha na maumivu aliyoyapata, aliumizwa zaidi na Geneviv ambaye aliyashuhudia yote na kujifunza kitu kibaya akilini mwake.
“Don’t cry for me Geneviv, im okay and everything is fine, Pray God for your daddy, don’t hate him.”
Aliongea Bi Patricia kwa taabu akimsihi binti yake kuchukulia kawaida yote yaliyotokea na kuzidi kumwomba Mungu kwani yeye ndiye mweza wa yote.
Bi Patricia aliendelea kutibiwa kwa siku kadhaa na hali yake ilipokuwa nzuri akaruhusiwa kurudi nyumbani.
Kwa siku zote alizokuwa Hospitalini, mumewe hakuwahi kuja hata mara moja kumjulia hali yake.Msaidizi mkubwa akawa ni mwanae pekee Geneviv ambaye ilibidi aache kwenda shule kwa takribani wiki mbili akimhudumia mama yake.Kipindi ambacho Geneviv alikuwa haendi shule, wenzake ndio walikuwa katika maandalizi ya mwisho kabla ya kufanya mtihani wa mwisho wa kumalizia elimu ya msingi
.
Aliendelea kumuomba Mungu amsimamie katika wakati mgumu aliokuwa nao.Kwa kipindi chote hicho Mzee Manuel Rwakatare alikuwa hafahamiki yuko wapi kwani hata nyumbani kwake alikuwa hakanyagi.
“Mum why cant we report dad on police station for the pain he has caused you?”
(mama kwanini usimshitaki baba polisi kwa maumivu aliyokusababishia?)
Aliuliza Geneviv wakati akimpoozea mama yake uji.Pamoja na maumivu aliyosababishiwa na mumewe,Bi Patricia bado alikuwa anampenda na alishamsamehe kwa yote yaliyotokea.
“Mwanangu Geneviv,matatizo ya kifamilia humalizwa na wanafamilia wenyewe kwa msaada wa Mungu baba wa Mbinguni,kwenda polisi ni kuongeza matatizo kwani hawatatusaidia chochote.Mungu anatufundisha kuwapenda wanaotufanyia mabaya, kusamehe
na kusahau kama yeye anavyotusamehe dhambi zetu,nakuomba usimchukie baba yako,msamehe kwani ni shetani ndio anamtumia kwa sasa,jifunze kusamehe…”
Bi Patricia alikuwa akimpa darasa zito binti yake kwani alionekana kuanza kumchukia baba yake.Wakiwa bado wanaendelea na mazungumzo yao, walisikia mlango ukigongwa kwa nguvu.Wakajua “Simba mtu amerudi”. Geneviv akainuka na kwenda kufungua mlango.Alikuwa ni baba yake,mzee Rwakatare.Japokuwa ilikuwa ni asubuhi,alionekana ameshalewa kama mtu aliyelala kwenye kilabu cha pombe.Bila hata salamu, mzee Rwakatare aliingia mpaka ndani alikomkuta mkewe akinywa uji alioandaliwa na mwanae.
“Karibu mume wangu,habari za asubuhi!” alimpokea kwa moyo mkunjufu mumewe.Mzee Rwakatare hakujibu kitu, akaanza kufoka.Safari hii alikuja na hoja mpya akimtuhumu mkewe kuwa anatembea na bosi wake na ndio maaana wakaandaa njama za kumfukuzisha kazi. Bi patricia hakujibu kitu akawa anamtazama mumewe usoni kwa huruma.
Geneviv alikuwa amesimama mlangoni akishuhudia yote yaliyokuwa yakiendelea. Ghafla mzee Rwakatare alimvamia mkewe pale alipokuwa amelala akiuguza majeraha yake ya kupigwa ambayo yalikuwa bado hayajapona.
“Si naongea na wewe? Mbona hunijibu…kiburi sio?”
Kabla hata Bi Patricia hajajibu lolote, alishtukia akipigwa kibao kizito usoni, damu zikaanza kumtoka masikioni,puani na mdomoni.
Geneviv alishindwa kuvumilia kitendo kile alichokiona.kwa nguvu zake zote akaibeba stuli iliyokuwa mbele yake na kuinyanyua juu, kisha akaishusha kwa nguvu kichwani kwa baba yake.Ilitua kisawasawa utosini na kumfanya mzee Rwakatare apige yowe kubwa kisha akadondoka chini na kutulia kimya…alipoteza fahamu.
“Umefanya nini Geneviv, si nilikwambia usilipe ubaya kwa ubaya?” aliongea Bi patricia huku akijikongoja kuamka kitandani na kumuinamia mumewe pale chini huku akijifuta damu zilizokuwa zinavuja baada ya kupigwa kibao na mumewe.
Geneviv alibaki akimshangaa mama yake, Pamoja na maumivu yote aliyokuwa anapewa na mumewe bado alikuwa akimtetea!
“No mum,no mum, it pain my heart, cant tolerate to see this…im walking away”
Aliongea Geneviv na kuanza kukimbia kuelekea nje akiwa haelewi anakokwenda. Hakukusudia kumuumiza baba yake,lakini pia hakuweza kuvumilia kuona mateso aliyokuwa anayapata mama yake.
Hakukumbuka hata kuvaa viatu,akatoka hivyohivyo huku akikimbia kama aliyerukwa na akili.Alikimbia umbali mrefu sana mpaka akaanza kuhisi mwili wote ukiishiwa nguvu.Akatafuta mti wenye kivuli na kujitupa chini huku machozi yakimtoka kama chemchemi.Taratibu usingizi ukaanza kumpitia…
****
Mzee Rwakatare alikuja kushtuka baada ya masaa manne tangu alipopoteza fahamu kwa kupigwa na kitu kizito kichwani. Alijikuta amelala chumbani kwake huku mkewe Bi Patricia akimpepelea kwa kanga yake na kiyoyozi alichokisogeza karibu kabisa na kitanda.
“Pole mume wangu, nisamehe kwani mimi ndio chanzo cha yote”
Alikuwa akiongea Bi Patricia kwa sauti ya chini huku machozi yakimtoka. Mzee Rwakatare alifumbua macho akiwa hakumbuki kilichomtokea, alichokihisi ni maumivu makali sehemu ya utosini.
“What happened to me!” Alihoji mzee Rwakatare kwa sauti ya chini,mkewe hakumjibu kitu, akabaki akimtazama usoni kwa huruma.Baada ya muda kumbukumbu zikaanza kumrudia upya.Alikumbuka kila kitu kuanzia siku ya kwanza alipompiga na kumjeruhi vibaya mkewe na kisha kumtelekeza chumbani akiwa amepoteza fahamu.Alikumbuka alivyoshinda kwenye baa za pombe kwa wiki mbili mfululizo huku akiwa hajui mkewe anaendeleaje ingawa alisikia kuwa alikuwa amelazwa.Alikumbuka pia jinsi alivyoingia kwa vurugu asubuhi hiyo na kuanza kumpiga upya mkewe japokuwa alijua kabisa kuwa bado hajapona.Kumbukumbu zake ziliishia hapo…
“What happened to me?....” alirudia swali lake lilelile lakini Bi Patricia hakumjibu kitu zaidi ya kuendelea kububujikwa na machozi.Kilichomshangaza Mzee Rwakatare ni kule kuzinduka na kujikuta yuko mikononi mwa mkewe.kwa matukio aliyokuwa anamfanyia aliamini isingekuwa rahisi kwa mkewe kuendelea kumpenda na kumjali kiasi kile.Alipomtazama tena usoni,aligundua mkewe alikuwa na makovu makubwa ambayo ni yeye ndiye aliyemsababishia.Alijikuta dhamira yake ikimshtaki kwa uovu aliomfanyia mkewe waliyetoka naye mbali kimaisha.
“Patricia…”
Bi Patricia alishtuka kumsikia mumewe akilitaja jina lake kwani tangu wampate mtoto wao Geneviv, mumewe aliacha kabisa kumuita jina lake…akitumia zaidi mama Geneviv au My Darling!
“Abee mume wangu!” aliitikia Bi Patricia kwa adabu huku akijifuta machozi.
“Naomba nisamehe mke wangu.Najua nimeuumiza sana moyo wako Darling, Najua nimekufanya ulie sana mke wangu…I know…I know! But please 4give me…I will never hurt you again.”
Mzee Rwakatare alishindwa kuyazuia machozi yasimtoke.Alimvuta mkewe na kumkumbatia kwa nguvu.Bi Patricia hakujibu kitu zaidi ya kumwambia kuwa yote alimwachia Mungu na alishamsamehe kwa sababu anampenda.
“Mwanangu Geneviv yuko wapi? Hebu mwite nimuombe msamaha sababu najua yeye ndiye aliyeumia zaidi”.
“Ngoja nimuangalie chumbani kwake…Aliinuka Bi Patricia kwa kujikongoja na kuelekea chumbani kwa Geneviv.Alishajua kuwa hayupo ila alitaka tu kwenda kuhakikisha.”
****
“Oyaa washkaji eeeh…huyu si ndo yule Cute Angel Geneviv wa sculi kwetu?”
“Ndo mwenyewe mwana! Halafu mi nilikuwa namtamani siku kibao useme ndio alikuwa ananimwaga kila nikimuaproch!”
“Hata mimi nilikuwa namlia taiming siku kibao ila nilikuwa namgwaya si unajua mtoto mwenyewe alivyo juu!”
“Leo kajilengesha kwenye 18 zetu…ful kujisevia”
Hayo yalikuwa ni mazungumzo ya vijana wanne waliokuwa wametoka porini kuvuta bangi baada ya kutoroka shule.Walimkuta Geneviv akiwa amelala chini ya mti kutokana na uchovu wa kukimbia juani akitoroka kwao baada ya kumjeruhi baba yake kwa kumpiga na stuli mpaka akapoteza fahamu wakati akimpiga mama yake.
Akiwa usingizini alisikia sauti za watu wakichekelea kwa furaha.Aliposhtuka alikuta vijana wapatao wanne wamemzunguka na kabla hata hajakaa sawa alijikuta akivamiwa mwilini na kubanwa pale chini kiasi cha kushindwa hata kufurukuta.Mmoja alimziba mdomo huku wengine wakimvua nguo.Kufumba na kufumbua nguo alizokuwa amezivaa zilichanwachanwa na kumuacha akiwa mtupu.Akajua kilichokuwa kinataka kutokea.
Hakuna kitu alichokuwa anakiogopa maishani mwake kama kubakwa.Tangu awe mkubwa hakuwahi kumjua mwanaume hata siku moja na aliapa kujitunza mpaka atakapokuja kuolewa.Hakuwa tayari kuamini kuwa usichana aliokuwa akiutunza kama yai ndio ulikuwa unatolewa kwa aibu na maumivu makubwa namna ile.Alijitahidi kufurukuta lakini wapi,akataka kupiga mayowe ya kuomba msaada lakini hakuweza…akashuhudia kijana wa kwanza akifungua zipu yake na kumuinamia pale chini.Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kufumba macho huku akiuma meno.Kilichofuatia ikawa ni maumivu makali kupita kiasi ambayo hakuwahi kuyapata maishani mwake.
Baada ya yule wa kwanza kumaliza, alishuhudia wa pili akijiandaa…akajua huo ndio ulikuwa mwisho wake.Alijikaza mpaka naye akamaliza, akashuhudia watatu naye akijiandaa…akajikuta fahamu zikimtoka polepole kutokana na maumivu makali aliyokuwa anayapata.
Wale vijana waliendelea kumfanyia ushetani ule Geneviv kwa zamu zamu mpaka wote wanne walipotosheka baada ya kurudia karibu mara tatu tatu.Wakamuacha akiwa amepoteza fahamu wakitokomea kusikojulikana.
Geneviv alikuja kushtuka baada ya kuhisi baridi kali ikimpiga.Aliposhtuka akajikuta yuko palepale chini ya mti, huku nguo zake zikiwa zimechanwachanwa.Alitaka kuinuka,maumivu makali yakamrudisha chini.Akawa anajaribu kukumbuka kilichomtokea,akapeleka mkono wake kwenye ikulu yake changa,kulikuwa kumeharibiwa vibaya mno…ndipo hapo kumbukumbu zilipomrudia,alikuwa amebakwa.Alibaki amepigwa na bumbuwazi akitamani hiyo iwe ndoto lakini haikuwa hivyo,ukweli ukabaki kuwa palepale,alibakwa.
Alijaribu tena kuinuka,lakini safari hii alisikia maumivu makali kupita kiasi.Akajilaza chali huku akilia kilio cha kuomboleza.Alijikuta akimchukia mno baba yake mzee Rwakatare kwani bila yeye asingepatwa na tukio baya namna ile.
“I hate my daddy! I hate men, they are Devils”
***********
Baada ya kumkosa chumbani kwake, Bi Patricia alirudi na kumpa mumewe taarifa.
“Atakuwa ameenda wapi? Maskini malaika wangu…”
Aliongea mzee Rwakatare akijifanya kumsikitikia mwanae.Kwa kifupi,zile tofauti zilizokuwepo baina ya Bi Patricia na mumewe zilionekana kama zimekwisha kabisa na sasa wote wakawa wanamfikiria binti yao Geneviv.
Muda ulizidi kwenda bila ya Geneviv kurudi nyumbani.Hawakujua yuko wapi na amepatwa na nini.
“Ningekuwa na nguvu ningeenda kumuulizia kwa wenzake,mwanangu hana tabia ya kuchelewa kurudi nyumbani namna hii! Sijui kapatwa na balaa gani maskini”
aliongea Bi Patricia kwa masikitiko baada ya kuanza kuhisi kuwa huenda mwanae amepatwa na jambo baya baada ya usiku kuzidi kuingia.Mwili wake wote ulikuwa bado una maumivu kutokana na kipigo cha mumewe kiasi cha kumfanya ashindwe hata kutoka nje kwenda kumtafuta mwanae.Saa ya ukutani iliyokuwa mle chumbani ilionyesha kuwa ni tayari saa nne za usiku.
Wasiwasi ulizidi kuwaingia kiasi cha kila mtu kubaki kimya akiwaza kivyake.
“kwani alivyoondoka aliaga anakwenda wapi?”
Mzee Rwakatare aliuliza swali la kijinga kiasi cha kumkumbusha mkewe yaliyotokea asubuhi ya siku ile na kumfanya Geneviv atoroke pale nyumbani bila kuaga.
“Si ujinga wako uliokuwa unaufanya asubuhi,unafikiri mwanao bado mtoto sio, namtaka mwanangu! Amka kamtafute mwanangu…!”
Bi Patricia alianza kucharuka na kumshinikiza mumewe aende kumtafuta Geneviv.Mzee Rwakatare naye hakuweza kutoka nje kwani bado alikuwa na maumivu sehemu ya kichwani baada ya kupigwa na stuli asubuhi.Wakabaki kulaumiana wenyewe kwa wenyewe.Mzee Rwakatare alijihisi kushtakiwa na dhamira yake sana,kwani ukweli aliujua kuwa yeye ndio chanzo cha matatizo na hata kama mwanae angepatwa na jambo baya,basi yeye ndiye aliyemsababishia.Alijikuta akisononeka sana moyoni hasa baada ya kumuona mkewe akizidi kulia kwa kuomboleza.
“Mke wangu jikaze jamani,unavyolia anamchulia mwanetu,atapatwa na matatizo bure,yote tumwachie Mungu”
Mzee Rwakatare alijifanya kuongea kwa busara.Bi Patricia hakuamini kusikia maneno kama yale kutoka kwa mumewe.Ilibidi ainue macho na kumtazama usoni kwa mshangao,alihisi mumewe anamkejeli kwani tangu aachishwe kazi hakuwahi kulitaja jina la Mungu kutoka kinywani mwake zaidi ya matusi ambayo sasa alishaanza kuyazoea.
Waliendelea kutazamana kwa muda mrefu huku kila mmoja akiwa kimya.Masaa yalizidi kuyoyoma na hatimaye saa ya ukutani ikawa inasoma saa sita za usiku. Bi patricia alishindwa kujikaza na akawa anaendelea kulia kwa kilio cha kwikwi.Pia alikuwa akisali kimoyomoyo akimuomba Mungu wake amnusuru mwanae Geneviv.
****
Manyunyu ya mvua yalianza kudondoka huku wingu zito likitanda angani kuashiria mvua kubwa inataka kunyesha.Geneviv alizinduka kutoka usingizini baada ya kuona ameanza kuloana.Aliposhtuka mwili wake ulikuwa ukitetemeka kwa baridi kali ya usiku huku akiwa hajajifunika kitu chochote zaidi ya nguo alizokuwa amezivaa ambazo nazo zilikuwa zimechanwachanwa. Alijaribu tena kuinuka kutoka pale chini na safari hii alifanikiwa kusimama kwani maumivu yalikuwa yamepungua kidogo.Alijaribu kuinua mguu na kupiga hatua lakini akajikuta akishindwa kutembea.
“I must die hard, I need to move out of this place”
(lazima nife kigumu,nahitaji kuondoka mahali hapa)
Alijiambia Geneviv kimoyomoyo wakati akijikaza na kuanza kupiga hatua fupifupi kuelekea barabarani ambako aliamini anaweza kupata msaada.Japokuwa alikuwa akisikia maumivu makali alijitahidi kujikongoja kiupande-upande na akawa anajongea taratibu kuelekea upande iliko barabara. Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiongezeka na kuanza kuuloanisha mwili wake mchanga.Kadri manyunyu yalivyokuwa yanaongezeka na kumloanisha ndivyo Geneviv alivyozidi kupata nguvu ya kutembea na kuongeza mwendo. Baada ya kitambo kirefu akawa amefika barabarani.
Hakutaka kupoteza muda zaidi,akaanza kuifuata barabara akiwa haelewi anakoelekea. Hakutamani tena kurudi nyumbani kwao kwani chuki dhidi ya baba yake ilizidi kukua na kumfanya amchukie kama shetani. Akiwa bado anazidi kusonga mbele akielekea asikokujua,aliona mwanga wa taa za gari likija kutokea mbele yake.Hakujua ni gari gani na lilikuwa likielekea wapi ila akapiga moyo konde na kuamua kulisimamisha.
“Haroo afande hebu simamisha ‘Defender’ ,naona kama kuna rimutu rinasimamisha gari,sijui ni rinani na rimetokea wapi usiku wote huu Mura!”
aliongea Koplo Marugu kwa Kiswahili kibovu akimuamuru dereva wake kusimamisha gari.Walikuwa wako katika doria ya usiku pamoja na askari wengine watatu waliokuwa wamekaa nyuma ya gari.
Geneviv aliendelea kulipungia lile gari mikono kwa nguvu zake zote na taratibu akaanza kuliona likipunguza mwendo na kusimama karibu yake.
Liliposimama Geneviv akagundua kuwa lilikuwa ni gari la polisi,alishusha pumzi ndefu na kumshukuru Mungu wake kwani aliamini angekuwa salama mikononi mwa wanausalama wale.Hakutaka kuwaambia ukweli wa kilichomtokea kwani alijisikia vibaya kueleza kuwa amebakwa kwani alihisi ni aibu kubwa kwake.Akaamua kutunga uongo…
Baada ya lile gari kusimama,askari walishuka na kuanza kumhoji ametoka wapi na anakwenda wapi usiku wote ule,ukizingatia yeye ni mtoto wa kike na hapo alipo ni porini.
“Tulikuwa tumetoka shambani na dada,tukavamiwa na watu walioanza kutupiga mpaka wakanichania nguo.Dada alikimbia na kuniacha peke yangu huku.”
Geneviv aliongea uongo mtakatifu huku akitoa machozi na kuwafanya wale askari waamini alichokuwa anakisema.Bila hata kumhoji maswali mengi,walimpakia ndani ya Defender na kuanza kurudi naye mjini ambapo alielezwa kuwa atapewa sehemu ya kulala mpaka asubuhi ambapo ataandikisha maelezo yake kituoni ili watuhumiwa waanze kusakwa.Hakuna hata mmoja aliyehisi kuwa maelezo ya Geneviv ni uongo.
Gari likawashwa na kuanza kurudi mjini.Muda mfupi baadae tayari walikuwa wameshafika kituo kikuu cha polisi cha Blaziniar ambapo Geneviv alikabidhiwa kwa askari wawili wa kiume waliokuwa zamu na wale polisi wengine wakaendelea na doria. Wale askari walimpokea Geneviv na kumuweka kaunta,huku wakijifanya kumuonea huruma. Walimuonyesha sehemu ya kukaa na wao wakaendelea na shughuli zao.
“Haloo afande haka kabinti ni kazuri mno,hebu kaangalie vizuri”
wale askari walikuwa wakinong’onezana kwa sauti ya chini na mara wote wakaanza kumtolea macho Geneviv ambaye alikuwa ameanza kusinzia pale alipokaa na hakuwa na habari kama wale askari wanamtazama kwa macho ya husda.
“Aisee kweli bwana,unajua nilikuwa sijakaangalia vizuri…halafu unajua mke wangu alisafiri wiki ya pili sasa…natamani niwe fataki japo kidogo tu!”
Waliendelea kunong’ona wale askari na wakajikuta wakicheka kwa pamoja na kugongesheana mikono.Kelele za vicheko zilimshtua Geneviv aliyekuwa anasinzia kwenye kiti alichokuwa amekalia.
Mmoja kati ya wale askari aliinuka na kumfuata pale alipokuwa amekaa na kumshika begani.
“Binti naona umechoka sana, pole! amka basi nikakuonyeshe sehemu ya kulala,usiwe na wasiwasi hapa uko mikononi mwa chombo cha dola…tutakulinda mpaka asubuhi”
Aliongea yule askari akimshika mkono Geneviv na kutoka nae nje ya jengo la kituo cha polisi. Geneviv hakuwa na wasiwasi kwani aliamini kazi ya jeshi la polisi ni kuwalinda raia wake. Wakatoka na kuelekea kwenye kibanda kidogo kilichokuwa mita chache pembeni.
****
Hakuna hata mmoja kati ya Mzee Manuel Rwakatare na mkewe Bi Patricia aliyepata hata tone la usingizi. Mpaka inagonga saa nane usiku, Geneviv alikuwa hajarejea nyumbani na hakukuwa na dalili za yeye kurudi. Bi Patricia alikuwa akizidi kulia hali iliyomfanya aanze kuhisi maumivu makali ya kichwa kwani alikuwa bado hajapona. Baada ya kuona mkewe hataki kutulia, ilibidi mzee Rwakatare ajiandae kwenda kutoa taarifa polisi usiku huohuo. Na yeye alionekana kuchanganyikiwa mno, akawa anajilaumu kwa yote aliyoyafanya ambayo ndiyo yaliyopelekea kuibuka kwa tatizo hilo.
Alipiga moyo konde na kujifariji kuwa hakuna binadamu asiyekosea. Baada ya kumaliza kujiandaa alimuaga mkewe ambaye hakumjibu kitu zaidi ya kuendelea kumwaga machozi.Alitoka na safari ya kuelekea kituo kikuu cha polisi cha Blaziniar ikaanza. Ilimbidi abebe mwamvuli kwani mvua nayo ilikuwa imechachamaa kunyesha.Baada ya safari ya takribani dakika arobaini, tayari alishawasili kwenye eneo la kituo cha polisi.
Tangu asimamishwe kazi serikalini,Mzee Rwakatare alikuwa hapendi kabisa kuonekana na polisi kwa kuhofia kukamatwa kwa makosa yake ya uhujumu ambayo bado upelelezi ulikuwa unaendelea, lakini kwa sababu ya mwanae alijikuta hofu ikimuishia. Akawa anapiga hatua za taratibu kusogelea eneo la kituo.
Akiwa hatua chache kabla ya kuufikia mlango mkubwa wa kuingilia kituoni,alisikia sauti ambayo ilimfanya mapigo ya moyo yaanze kumwenda kasi mithili ya injini ya jeti.
Ilikuwa ni sauti ambayo aliitambua vizuri kuwa ni ya mwanae Geneviv ikitokea kwenye kibanda kidogo pembeni ya kituo cha polisi.
Geneviv alikuwa akilalama kwa maumivu makali aliyokuwa anayapata wakati yule askari aliyejifanya kumpeleka kulala akimuingilia kimwili kwa nguvu. Kwa mara nyingine tena, Geneviv alikuwa akibakwa,tena safari hii na Askari polisi.
Mzee Rwakatare hakutaka kuyaamini masikio yake kuwa ile sauti kweli ilikuwa ni ya Geneviv.Ikabidi asogee mpaka karibu ya kile kibanda na kuchungulia ndani kupitia tundu dogo chini ya dirisha.
Hakuyaamini macho yake kwa alichikiona…
“Sh*t, what the hell are you doin with my daughter…im gonna kill you!”
Mzee Rwakatare aliongea kwa hasira kali, na kwa nguvu zake zote aliukanyaga mlango wa kile chumba na kuingia ndani mzima-mzima.
Yule askari alishtuka kuona mlango ukivunjwa na kumharibia starehe yake.Akawa anahangaika kuvaa suruali yake vizuri.
Mzee Rwakatare alimuwahi kwa kipigo kikali cha kushtukiza mpaka yule askari akadondoka chini.Alipotazama pembeni alikiona kipande cha bomba la chuma kilichokuwachini. Alikiokota na kuanza kumuadhibu vikali yule askari kichwani mpaka akazimia.
Kwa haraka alimuinua mwanae Geneviv ambaye bado alikuwa akilia kwa uchungu kutokana na maumivu makali aliyokuwa anayapata huku damu ikimchuruzika kutoka katikati ya miguu yake.Alimuweka begani na akatoka naye kwa spidi ya ajabu na kuanza kukimbia nae kutokomea gizani.
Hakuna askari aliyeelewa kinachoendelea.Mvua nayo ilikuwa ikizidi kupamba moto na sasa zilianza kusikika radi kali zikipiga na kuufanya usiku uzidi kutisha.Mzee Rwakatare hakujali kitu,akawa anazidi kutimua mbio huku Geneviv akiwa begani.
Akiwa umbali wa mita kadhaa,alishtukia kuona anamulikwa na taa za gari lililokuwa likiingia kituo cha polisi. Kwa haraka akamrusha Geneviv chini na yeye akarukia pembeni ya barabara kwenye mtaro.
Kutokana na mvua kubwa iliyokuwa inaendelea kunyesha ikiambatana na ukungu,hakuna mtu yeyote kutoka kwenye lile gari aliyewaona.
Gari ambalo aliligundua kuwa ni la polisi likapita na kuingia pale kituoni.Kwa haraka aliinuka na kumnyanyua mwanae na kumuweka tena begani.Akawa anatimua mbio kurudi nyumbani kwake, safari hii akipitia njia za vichochoroni kukwepa kuonekana tena na polisi.Baada ya kama nusu saa akawa ameshafika nyumbani kwake. Geneviv alikuwa akiendelea kulalama kwa maumivu na hakuelewa kilichofuatia mpaka alipojikuta anaingizwa ndani mwao.
Bi Patricia alishtuka kusikia mlango ukigongwa.
“Nini tena jamani?” Bi Patricia aliuliza kwa sauti iliyokauka kutokana na kulia, na akawa anajikongoja kwa uchovu kwenda kufungua mlango. Alishakata tamaa ya kumuona mwanae Geneviv usiku huo.
“Fungua mke wangu!”
Aliongea mzee Rwakatare kwa sauti iliyomaanisha kuna jambo. Bi Patricia aliharakisha kufungua mlango.
“Ooooh My God!.....”
Bi Patricia alishtuka kupita kiasi.
“What happened to my daughter,oooh…”
Kwa haraka akampokea Geneviv huku mwili wote ukimtetemeka. Akampeleka chumbani kwake na kumlaza kitandani huku mumewe akianza kuhangaika kutafuta huduma ya kwanza. Kila mtu akawa kama amechanganyikiwa, na zaidi Bi Patricia ambaye bado alikuwa hajajua nini kimemtokea mwanae. Kengele ya hatari ikalia kichwani mwa Bi Patricia wakati akiendelea kumchunguza Geneviv ambaye alikuwa hajitambui.
Kitu cha kwanza alichoshtushwa nacho ni kuona jinsi nguo za mwanae zimechanwa-chanwa. Akiwa bado anamchunguza akashtushwa na damu zilizoiloanisha sketi ya mwanae, mapigo ya moyo yakaanza kumwenda mbio…hakutaka kuamini haraka kuwa anachokihisi ndicho kilichomtokea mwanae.
Alitamani iwe ndoto lakini naye hakuweza kuubadili ukweli,akajikuta akipiga yowe kubwa na kuanza upya kuomboleza baada ya kubaini kuwa ni kweli mwanae alifanyiwa ushetani na wanaume.
“Cant believe this…I cant! Unaona ulichomsababishia mwanangu, haya furahi sasa malengo yako yametimia, ooh my Lord!”
Bi Patricia akawa anampiga-piga mumewe mgongoni huku akilia kwa uchungu. Akawa anamlalamikia kuwa yeye ndio chanzo cha yote.
“Mke wangu acha kunilaumu, mbona nimekiri makosa! Cha msingi kwa sasa tusaidiane kuokoa maisha ya geneviv, huu sio muda wa lawama.”
Bi Patricia alikuwa mgumu wa kuelewa na akazidi kulia kwa sauti kubwa kiasi cha kuwaamsha majirani ambao baada ya muda mfupi walikusanyika nje.Baada ya majadiliano ya muda mfupi,muafaka ukafikiwa kuwa Geneviv apelekwe hospitali haraka usiku huo huo.Kila mtu alimuonea huruma.
Jirani mmoja akajitolea kutoa gari lake na kwa haraka Geneviv akabadilishwa nguo na safari ya kwenda hospitali ikaanza mara moja. Japokuwa mvua kubwa ilikuwa inaendelea kunyesha hakuna aliyeonekana kujali, kila mtu akawa anahangaika kuokoa maisha ya Geneviv.
Baada ya kitambo kifupi, gari walilompakia mgonjwa likakwama kwenye matope kutokana na mvua kubwa iliyokuwa inaendelea kunyesha, hali iliyowalazimu mzee Rwakatare na dereva waanze kusaidiana kulitoa gari pale lilipokwama.Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila mafanikio, huku hali ya Geneviv ikizidi kuwa mbaya, Mzee Rwakatare akaamua kumbeba Geneviv na kuendelea na safari ya kuelekea Hospitali.
“Lakini mvua hii ni hatari kwa mgonjwa, ukizingatia bado radi zinapiga sana, kwanini tusiendelee kulihangaikia gari?”
Dereva alitoa ushauri ambao Mzee Rwakatare alishindwa kuuafiki. Akamuinua mwanae na kumuweka begani na safari ikaendelea. Bi Geneviv naye akashuka na kuanza kuwafuata kwa kukimbia huku akizidi kulia. Dereva akabaki ameduwaa akiwaonea huruma kwa yaliyowakuta.
Baada ya safari ndefu na ngumu, hatimaye walifika kwenye hospitali ya planet Health Aid ambako walipokelewa na manesi waliokuwa zamu na upesi upesi Geneviv akawekwa juu ya kitanda cha wagonjwa na kuanza kukimbizwa kuelekea wodini. Kwa haraka akaanza kupewa huduma ya kwanza. Baada ya muda mfupi alitundikiwa dripu za maji ambazo zilikuwa zikitiririka kwa kasi kuingia mishipani mwake. Saa ya ukutani ya pale hospitali ilionyesha kuwa tayari ni saa kumi ya alfajiri.
Mzee Rwakatare na mkewe wakabaki nje ya wodi wakiwa wamekaa kwenye viti sehemu ya mapokezi huku kila mmoja akiwa amejiinamia kimya. Baada ya muda mfupi nesi akatoka wodini akiwa na faili mkononi mwake na kumuita mzee Rwakatare pembeni.
“Pole mzee!” yule nesi alimpa pole mzee Rwakatare na kabla hata hajajibu kitu akaendelea kuongea…
“Mgonjwa anaendelea kupata huduma ya kwanza na muda si mrefu atazinduka. Uchunguzi wetu umebaini kuwa amebakwa, na kwa taratibu za hospitali zote nchini ni kwamba mgonjwa wa namna hii lazime apitie kituo kikuu cha polisi kuchukua PF3 kwanza ndipo atibiwe, ila kwa kuwa mgonjwa wenu alikuwa na hali mbaya tukaona ni bora tuendelee kumpa huduma ya kwanza, ila matibabu ataanza kupewa baada ya w ewe kuleta hiyo PF3”
Alimaliza kuongea yule nesi na kurudi wodini akimuacha Mzee Rwakatare ameduwaa asijue la kufanya.
Bi Patricia aliinuka haraka na kumfuata yule nesi kabla hajaingia ndani na akawa anamhoji hali ya mgonjwa.
“Maelekezo yote nimempa mzee, nenda atakueleza vizuri”
Aliongea yule nesi kwa kifupi huku akifunga mlango.
Bi Patricia alirudi kwa mumewe aliyeonekana kuchanganyikiwa, akamshika mkono na kumkalisha chini huku akiwa na shauku ya kutaka kujua yule nesi alimwambia nini.
Ukweli ni kwamba tangu usiku alipomuokoa mwanae, mzee Rwakatare alikuwa hajamwambia chochote mkewe juu ya jinsi alivyomuokoa na mazingira aliyomkuta kutokana na hali aliyokuwa nayo mkewe. Ilibidi aanze kumueleza tangu mwanzo jinsi alivyomuokoa Geneviv kabla ya kumwambia maelekezo aliyopewa na yule nesi.
Baada ya kumaliza maelezo marefu, wote walishusha pumzi ndefu wakabaki wakitazamana wasijue nini cha kufanya.
“Sasa tutafanya nini mume wangu, tukizidi kuzubaa tutampoteza mtoto wetu…please do something to save her.”
“Sasa wewe unafikiri mi ntafanya nini, Polisi siwezi kwenda kwa sababu hao ndio walioniharibia mwanangu, isitoshe nimesababisha madhara pale kituoni.Huoni kuwa nikienda nitakuwa nimejipeleka mwenyewe? I cant report anything to them. They are all rotten.”
Mzee Rwakatare na mkewe waliendelea kubishana kuhusu kwenda kuchukua PF3 kama walivyoelekezwa na yule nesi. Mwishowe walifikia uamuzi wa kutokwenda. Wakaamua kumueleza yule nesi ukweli kuwa mtoto wao alibakwa na Polisi haohao hivyo haikuwa na maana kwenda tena kwao kuomba kibali.
“Lakini vipimo vyetu vinaonyesha kuwa amebakwa na watu si chini ya watano, nyie mlikuwa wapi mpaka mtoto anafanyiwa ukatili mkubwa namna hii” Yule nesi alizidi kuongea kwa msisitizo huku akionekana kuwatupia lawama wazazi kwa kushindwa kumlinda binti yao.
“Nesi sio kweli, mwanangu hajabakwa na watu watano, no! mbona bado mdogo,au mmekosea vipimo…Ooh my God! I cant believe th..i…s….”
Bi Patricia alikuwa akimbishia nesi wakati akielezwa ukweli wa yaliyomkuta mwanae huku akilia. Mzee Rwakatare alibaki ameduwaa na yeye akiwa haamini alichokisikia kutoka kwa nesi.
“Anyway, cha msingi we tusaidie mtoto atibiwe,mengine tutazidi kuelekezana taratibu.”
Mzee Rwakatare aliongea kwa kukata tamaa na kwa bahati nzuri yule nesi aliwaelewa. Akarudi wodini na kuanza kumpa matibabu Geneviv ambaye fahamu zilikuwa bado hazijamrudia.
Si mzee Rwakatare wala mkewe waliokuwa tayari kuamini kuwa ni kweli mtoto wao amebakwa na watu zaidi ya watano. Mzee Rwakatare alishindwa kuyazuia machozi yasimtoke, ikawa ni zamu ya mkewe kumbembeleza. Alikuwa akijihisi mwenye hatia kubwa sana mbele ya mwanae na mkewe na zaidi mbele ya Mungu.
Alianza kuamini sasa kuwa ni kweli pombe badala ya kupunguza matatizo ilikuwa ikiongeza.Alijilaumu sana kwa ujinga alioufanya na kumsababisha madhara makubwa namna ile.
“One mistake, five goals…F*ck me because im the source…”
Alikuwa akijisemesha peke yake kama mwendawazimu huku akijipigapiga kichwani.
*****
Mpaka inafika saa mbili asubuhi Geneviv alikuwa bado hajazinduka hali iliyoanza kuwatia hofu hata wale manesi.
“It seems she has been severely damaged in her genitals, Hydro-saline therapy is over and yet the condition is still worse. Lets call the Doctor for emergency”
(Inaonekana ameumizwa sana, dawa tulizompa zinaisha lakini bado hali ni mbaya, inabidi tumuite daktari kwa huduma ya dharula)
Wale manesi waliokuwa wanamhudumia Geneviv tangu usiku walikuwa wakijadiliana nini cha kufanya baada ya kuona hali ya mgonjwa inazidi kuwa mbaya kadri muda ulivyokuwa unaenda. Ikabidi Geneviv ahamishiwe chumba cha wagonjwa mahututi I.C.U (Intensive care unit) ambako alianza kupewa huduma ya dharula ili kuokoa maisha yake.
“Inject her the Ant-spermatids serum, then add Oestrogen 20mls into Hydro-saline therapy… If this will fail to awake her, it will be out of our control”
(Mchomeni sindano ya dawa ya Ant-spermatid, kisha ongezeni mililita 20 kwenye dripu yake yenye dawa… kama bado atashindwa kuzinduka basi itakuwa nje ya uwezo wetu)
Aliongea daktari Bingwa wa magonjwa ya kina mama na watoto, Dokta Barikieli Zayumba akiwaelekeza manesi namna ya kufanya. Kwa muda wote huo, Bi Patricia na mumewe walikuwa wameshikana mikono nje wakiomba sala mfululizo, wakimuomba Mungu wao amnusuru Geneviv
****
Masaa mawili tangu Geneviv abadilishiwe dawa na kupewa dawa za mwisho za kuokoa uhai wake, mapigo yake ya moyo ambayo yalikuwa chini sana yalianza kuongezeka taratibu na kurudi kwenye hali yake ya kawaida. Mara akafumbua macho na kuanza kupepesa huku na kule kama anayejiuliza hapa niko wapi…
“Doctor, she is back to her counciousness, she is awake”
(dokta, mgonjwa amerudiwa na fahamu, ameshaamka…)
Aliongea kwa sauti nesi aliyekuwa akimhudumia akimfuata daktari ambaye naye alisogea pembeni ya kitanda cha Geneviv na kuanza kumpima mapigo ya moyo.
“Unajisikiaje binti? Daktari alimuuliza Geneviv kwa upole huku akimgusa usoni kupima joto la mwili wake!”
Geneviv hakujibu kitu, akawa kama anajitahidi kukumbuka jambo fulani.Baada ya kama dakika tatu tangu fahamu zimrudie, Geneviv alianza kuongea.
Kauli ya kwanza aliyoitoa ilikuwa ni kuuliza aliko mama yake.
“Where is my mum? I need to see her…I need to see my mum”
Aliongea Geneviv na kuanza kushinikiza mama yake aletwe.Ilibidi Bi Patricia aende kuitwa pale nje alipokuwa amekaa. Mzee Rwakatare naye hakutaka kubaki peke yake, akawa anang’ang’ania na yeye aingie wodini.
“Lakini amesema anataka kumuona mama, sio baba” yule nesi alitahadharisha kabla ya kuwaruhusu kuingia. “Hamna tatizo nesi, huyu ndio baba yake, mwache tu tuingie nae”
Aliongea Bi Patricia akimtetea mumewe.Wakaruhusiwa kuingia. Baada ya kumuona mama yake, Geneviv alianza kulia kwa nguvu, Bi Patricia akainama pale kitandani na kuanza kumbembeleza.
“Calm down my dear, everything is going to be right. We love you and we pray for you, get well soon!” (Tuliza nafsi yako mwanangu, kila kitu kitakuwa sawa.Tunakupenda na tunakuombea upone haraka)
Mzee Rwakatare alikuwa amesimama nyuma kabisa na akawa anasogea taratibu. Baada ya kubembelezwa na mama yake, Geneviv alianza kutulia. Alipomuona baba yake tu, ikawa shughuli pevu…Geneviv alianza upya kupiga kelele huku akitoa maneno makali kwa baba yake.
“Get out of here dady, I hate you, I hate men…”
( Ondoka humu ndani baba, nakuchukia, nawachukia wanaume…)
Hakuna aliyeamini kumsikia mgonjwa akitoa maneno makali namna ile kwa baba yake mzazi.Pamoja na kujitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote kuokoa maisha ya mwanae, bado Geneviv alikuwa akimchukia mno baba yake, hasa kutokana na vitendo vya kinyama alivyoshuhudia akimfanyia mama yake siku chache zilizopita, na matatizo aliyomsababishia mpaka akawa hapo hospitali.Hakujua kuwa ni baba yake huyohuyo ndiye aliyemuoka kutoka kwenye mdomo wa samba.
Mzee Rwakatare akawa anaomba radhi kwa mwanae akionyesha kuwa amebadilika na hata rudia tena kuwafanyia mabaya yeye na mama yake. Hakuna lililomuingia akilini, akawa anazidi kupiga kelele mpaka madaktari wakaingilia kati na kumtoa nje mzee Rwakatare. Alikubali kutoka huku moyo wake ukiwa umefedheheka mno. Akawa amejiinamia huku akijitahidi kuyaficha machozi.
Bi Patricia akawa na kazi ya ziada ya kumuelewesha mwanae kuwa baba yake amekiri makosa na ni yeye ndiye aliyemuokoa usiku wa manane na kumrudisha nyumbani kisha kumleta pale Hospitalini. Kidogo akaanza kuelewa, ingawa kwa shingo upande.
“Kwani umemfanya nini mwanao mpaka akuchukie kiasi hiki? Unaona baada ya wewe kutoka tu, ametulia!”
Alihoji daktari Barikieli Zayumba akiwa amesimama pale alipojiinamia mzee Rwakatare. Hakuwa na jibu la kutoa zaidi ya kumuangalia daktari kwa huruma. Wakati wanaendelea kutazamana usoni, Daktari alionyesha mshangao wa wazi-wazi baada ya kugundua kuwa kumbe aliyekuwa akiongea nae ni yule Manuel Rwakatare aliyekuwa afisa katika wizara ya madini na nishati kabla ya kusimamishwa kazi na mheshimiwa Raisi.Vyombo vyote vya habari asubuhi ile vilikuwa vikimzungumzia yeye ingawa mwenyewe alikuwa bado hajajua kinachoendelea kutokana na kumhangaikia mwanae Geneviv.
“Ebwana wewe si ndio yule mzee Rwakatare wa wizarani?” Aliuliza daktari kwa mshangao mkubwa. Mzee Rwakatare hakuelewa ni kwa nini ameulizwa swali lile. “Mimi ndiye, kwani…”
Alijibu kwa mkato akitaka kumkatisha asiendelee kumhoji maswali mengi.
“Umesikia kilichotokea usiku pale kituo kikuu cha polisi cha Blaziniar?”
Daktari Barikieli alizidi kumdadisi mzee Rwakatare. Kusikia swali lile alijikuta moyo ukimlipuka pyaaaa! “Aah aah,sijasikia kwani kumetokea nini” alidanganya mzee Rwakatare huku akibabaika. Ilibidi daktari amchukue mpaka ofisini kwake ambako baada ya kukaa, alimtolea gazeti lililotoka asubuhi ileile na kumpa asome mwenyewe.
“Mungu wangu!” Mzee Rwakatare alijikuta akitamka kwa sauti kubwa na kulidondosha lile gazeti chini. Ilikuwa ni habari ambayo hakuelewa yeye amehusishwa vipi. Ilisomeka hivi…
“UJAMBAZI KITUO KIKUU CHA POLISI- ASKARI AULIWA, SILAHA ZAIBWA! RWAKATARE AHUSIKA, ANASAKWA NA POLISI…”
Chini ya kichwa cha habari ile kulikuwa na maelezo ambayo yalieleza kuwa majambazi yenye silaha yamevamia kituo kikuu cha polisi usiku wa manane na kumuua polisi mmoja aliyekuwa zamu, kisha kuvunja stoo ya silaha na kuiba idadi kubwa ya silaha. Habari ilizidi kueleza kuwa, kitambulisho cha mmoja wa majambazi kimeokotwa eneo la tukio na mtu huyo ametambulika kwa jina la Manuel Rwakatare ambaye aliwahi kuwa muajiriwa serikalini kabla ya kusimamishwa kazi. Kulikuwa pia na picha ambayo ilimuonyesha mzee Rwakatare ikiwa na maandishi makubwa juu yake “MOST WANTED”, na taarifa ikazidi kueleza kuwa anatafutwa kwa udi na uvumba, na zawadi nono itatolewa kwa yeyote atakayesaidia polisi kumkamata jambazi huyo hatari.
Mzee Rwakatare alihisi kama akili inaacha kufanya kazi na kutengana na mwili, akawa kama anayeota ndoto za mchana. Alipojikagua mifuko yote akagundua kuwa ni kweli alipoteza kitambulisho, lakini ni wakati anamuokoa mwanae aliyekuwa akibakwa na polisi na si vinginevyo kama habari ile ilivyoeleza.
“Noo! Noo! Mimi sio jambazi, wamegeuza maneno, Noo! Sio mimi…”
Aliongea mzee Rwakatare kwa sauti kubwa huku akivua shati lake na kulitupa chini, kisha akaanza kukimbia kutoka nje ya ofisi kama mwendawazimu. Daktari Barikieli alibaki ameduwaa akimsikitikia mzee mwenzake.
Mara wakaanza kusikia ving’ora vya magari ya polisi yakija na kuizunguka hospitali yote. Mzee Rwakatare akawa kama aliyepagawa, akawa anakimbia huku na kule akitafuta sehemu ya kutokea bila mafanikio. Akajua huo ndio mwisho wake…
Akaona kitu pekee ni kurudi wodini kumuomba msamaha mwanae kwa mara ya mwisho kwani alijua hawezi kusalimika kutoka kwenye mkono wa sheria zilizopindishwa kuwalinda wachache. Kabla hata hajaufikia mlango wa wodi aliyolazwa mwanae Geneviv, alisikia amri kali kutoka kwenye kipaza sauti cha gari la polisi iliyomtaka asimame palepale alipo na kuinua mikono juu. Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kusalimu amri huku akipiga kelele,
“mimi sio jambazi, mnanionea bure! Nilikuwa namuokoa mwanangu… I was saving my Geneviv…” Alipiga kelele kwa nguvu kiasi cha kuwafanya waliokuwa wodini kushtuka.Wale Polisi hawakuonekana kujali anachokizungumza, wakamkamata na kumfunga pingu mikononi na miguuni, kisha akabebwa juu juu kama mzigo na kupelekwa lilikopaki karandinga la polisi. Akarushwa ndani kama mzigo kisha milango ikafungwa na gari likaanza kuondoka likisindikizwa na msafara mrefu wa magari ya polisi.
Alipochungulia nje kupitia nyavu za lile karandinga, alimuona mkewe akitoka nje ya wodi huku akikimbia kuyafuata yale magari.
Kwa mbali alisikia mkewe akilia kwa kupiga kelele huku akisisitiza kuwa mumewe hakuwa jambazi, lakini askari waliokuwa chini walimsukuma kwa nguvu, na akashuhudia akidondokea pembeni ya barabara. Alijikuta akimwaga machozi kama mtoto.
Msafara ule uliongoza mpaka gereza kuu la Blaziniar, ambapo Rwakatare alishushwa na kuingizwa gerezani chini ya ulinzi mkali, eneo lote likiwa limezingirwa na polisi wenye silaha na mbwa wa kijeshi. Bado alikuwa haamini kama kweli yanayotokea ni kweli, aliyafananisha na filamu za Mel Gibson.
Aliingizwa mpaka vyumba vya ndani kabisa vya gereza lile, na akafungiwa kwenye chumba kidogo chenye giza.
“Im finished… im gone! Ooh My Lord rescue me from this hell…”
Aliongea Mzee Rwakatare huku akimwaga machozi kama mtoto mdogo, akakaa chini na kuegamia ukuta mchafu wa kile chumba kilichokuwa kikitoa harufu kama choo cha stendi… alitia huruma.
Baada ya kuingizwa ndani ya gereza kuu chini ya ulinzi mkali na kufungiwa kwenye chumba kidogo chenye giza, ndani kabisa ya gereza, matumaini ya kutoka uraiani yanamuishia kabisa Mzee Rwakatare. Kwa jinsi ambavyo anazijua sheria za nchi yake, ilikuwa vigumu sana kwa yeye kuachiwa huru hata kama ukweli haukuwa kama ulivyoelezwa. Ukweli halisi usingeweza kufahamika haraka kutokana na Sheria za nchi kuwa zinachezewa na kupindishwa kwa maslahi ya wachache na kuwaacha maelfu ya raia wakiteseka bila hatia.
Matukio ambayo mwenyewe aliyatafsiri kama mikosi yalikuwa yamemwandama kiasi cha kuielemea nafsi yake. Ni ndani ya muda mfupi sana maisha yamebadilika kabisa, kila kitu kimebadilika kwa kiasi cha kusikitisha. Kwake ni kama mchezo wa kuigiza… tangu aliposimamishwa kazi kwa tuhuma ambazo bado zilikuwa zikifanyiwa upelelezi za uhujumu wa nchi akiwa kwenye ofisi ya madini na nishati, kila kitu kilipoteza mwelekeo na kuharibika mpaka alipojikuta ndani ya kuta za gereza kuu. Hakuwa na la kufanya zaidi ya kuukubali ukweli.
“Jifunze kupokea matatizo kwa moyo mkunjufu bila ya kinyongo, kama unavyopokea furaha”
Maneno hayo yalikuwa yakijirudia rudia kichwani mwake, lakini hakuweza kuhimili kuipokea misukosuko ile kwa moyo mkunjufu kwanialiona inamzidi uwezo.
“God, where are you? Why do you allow this to happen to me and my family? Why me?...”
(Mungu uko wapi?, kwa nini unaruhusu haya yanipate mimi? Kwa nini mimi?)
Alijikuta machozi yakimbubujika kama chemchemi ya maji.
Hakukuwa na matumaini tena ya kusalimika, kilichobaki ikawa ni uvumilivu kwenye mateso. Aliamini huo ndio ulikuwa mwisho wa kila kitu katika maisha yake…
Baada ya kushuhudia mumewe akiwa ndani ya karandinga la polisi akipelekwa gerezani, Bi Patricia almanusra apoteze fahamu pale hospitalini. Tangu alipoanza kuishi na mumewe miaka takribani kumi na tano iliyopita hakuwahi kuhisi kuwa itafika muda kila kitu katika maisha yao kitavurugika na kupoteza mwelekeo kama ilivyokuwa inatokea kwa sasa.
Mumewe hakuwa jambazi wala muuaji kama alivyokuwa akiandamwa na vyombo vya habari na polisi. Aliamini kwa asilimia zote kuwa Mungu alikuwa akiwapima imani na kuona ustahimilivu wao katika mapito magumu kama yale. Hakuyaamini yale aliyoyaona yameandikwa kwenye gazeti kumhusu mumewe. Alirudia tena na tena kuisoma habari ile lakini haikumuingia akilini. Alishindwa kuficha kilichokuwa kinaendelea moyoni mwake, huzuni ya kuonewa.
Dokta Barikieli Zayumba ilibidi aingilie kati na kuanza kumdadisi kwa undani Bi Patricia. Ni kweli kuwa tayari mzee Rwakatare alikuwa mikononi mwa dola na matumaini ya kutoka hayakuwepo kutokana na uzito wa kesi aliyobebeshwa. Lakini je
yaliyosemwa na kuandikwa na vyombo vya habari ndiyo yaliyokuwa yametokea?
Kwa haraka haraka hata raia asiyejua sheria angeweza kubaini kilichokuwa kinaendelea, sheria ilikuwa inapindishwa. Geneviv alikuwa hospitalini kwa matatizo aliyosababishiwa na wanaume (wakiwemo polisi), na hakukuwa na mtu mwingine zaidi ya manesi na madaktari waliofahamu ukweli wa kilichomsibu. Leo harakati za kuokolewa kwake zinageuzwa na kuripotiwa kuwa ni ujambazi…Ilikuwa ni utata mtupu.
Bi Patricia ilibidi amueleze daktari Zayumba kilichotokea kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Baada ya kumueleza kwa undani hali halisi ilivyokuwa, alipata picha kamili.
“Lakini hawa polisi wataendelea kunyanyasa raia wasio na hatia mpaka lini? Kazi yao ni kutulinda au kutukandamiza?”
Alikuwa akihoji kwa masikitiko Dokta Barikieli Zayumba . Alijikuta akiingiwa na huruma ya kibinadamu.
“Tunaweza kuwashinda hawa, cha msingi twende tukaongee na binti yenu Geneviv kama atakuwa tayari kutoa ushahidi wa kumkomboa baba yake, basi tutashinda, Mungu yu pamoja nasi…”
Alitoa ushauri Daktari, lakini Bi Patricia alishindwa kuafiki kwa jinsi alivyomfahamu Geneviv.
“Dokta ahsante kwa kuonyesha kuwa upo pamoja nasi. Nimjuavyo mwanangu hawezi kumsaidia baba yake kwani bado anamchukia mno… tuache tu mungu ndiye atakayejua namna ya kutunusuru”
Kauli ile haikumvunja nguvu daktari ambaye sasa alionesha nia ya kutaka kuwasaidia. Waliendelea kuzungumza kwa muda mrefu na hatimaye daktari Zayumba ikabidi achukue jukumu la kumpa tiba ya kisaikolojia Geneviv, kwani ilionekana anamchukia baba yake kwa sababu ya kuumia mno kisaikolojia.
Daktari alizidi kumweleza Bi Patricia kuwa hali kama ya mwanae huwatokea watoto wengi wanaoshuhudia mateso ya kikatili wanayofanyiwa mama zao na kama wasipopata msaada wa kisaikolojia huja kuwa hatari katika maisha yao ya baadae. Baada ya mazungumzo ya muda mrefu, hatimaye Daktari na Bi Patricia walitoka ofisini na kwenda wodini alikolazwa Geneviv ambaye sasa alikuwa amepata nafuu kubwa na aliweza hata kukaa kitandani mwenyewe. Daktari Zayumba alitumia mbinu zake zote za kidaktari na kisaikolojia kumshawishi Geneviv kutomchukia tena baba yake, na baada ya kuzungumza naye kwa muda mrefu hatimaye chuki yote aliyokuwa nayo kwa baba yake iliisha. Kwa muda wote huo walikuwa bado hawajamwambia kuwa baba yake tayari yuko gerezani.
“Do you hate your daddy anymore?”
Aliuliza Bi Patricia huku akimkumbatia mwanae ambaye sasa alianza kuonyesha kuchangamka.
“I love my daddy, I don’t hate him anymore! I’ve learn to forgive and forget…I love him!”
Aliongea Geneviv kwa furaha huku naye akimkumbatia mama yake. Daktari Zayumba alikuwa amesimama pembeni akifurahia mafanikio mazuri ya kazi yake aliyoifanya. Hiyo ilikuwa ni hatua muhimu sana katika safari ya kumkomboa mzee Rwakatare kutoka mikononi mwa sheria zilizopindishwa. Kwa pamoja walimtanguliza Mungu kuhakikisha kuwa haki inachukua mkondo wake na kumuacha huru mzee Rwakatare. Baada ya kumuweka sawa Geneviv, Daktari na Bi Patricia walitoka tena nje na kuelekea ofisini ambako bila ya kupoteza muda walianza kuandaa ushahidi wa kitaalamu ambao ungemtoa gerezani mzee Rwakatare. Walipanga kufichua uovu wa jeshi la polisi kwa kitendo walichomfanyia Geneviv.
Mpango madhubuti ukaanza kuandaliwa chini ya usimamizi wa daktari Zayumba. Kitu cha kwanza walichokifanya ilikuwa ni kutafuta vielelezo muhimu kama cheti cha daktari na vipimo vya awali alivyochukuliwa Geneviv wakati alipofikishwa hospitalini hapo akiwa hajitambui.
“Lakini vipimo vinaonyesha kwamba alifanyiwa kitendo hicho na watu zaidi ya watano, hebu kajaribu kumuuliza kama anaweza kuwakumbuka wote vizuri ili maelezo yetu yasije kupishana”
Daktari Zayumba alitoa hoja ya msingi ambayo Bi Patricia aliiona kuwa inafaa kufanyiwa kazi mapema. Akatoka na kwenda wodini alikokuwa amelazwa Geneviv. Ilibidi atumie mbinu za kiutu uzima kuweza kuufahamu ukweli wa wahusika halisi wa tukio bila ya kumuumiza tena mwanae. Alianza kwa kumueleza yaliyomsibu baba yake mpaka akapelekwa gerezani. “Alikuwa anakuokoa wewe kwa hiyo wewe ndio mtu pekee unayeweza kusaidia akaachiwa huru, nakuomba sana mwanangu tusahau yote aliyotufanyia daddy, tuungane kumsaidia atoke gerezani”Bi Patricia alikuwa akimsihi mwanae.
Geneviv alimuonea huruma baba yake kiasi cha kutoa machozi na akaahidi kufanya kila linalowezekana kumsaidia baba yake.
“Nimekuelewa mumy, niko tayari kufanya lolote kumtoa daddy Gerezani. Mwalimu wetu alitufundisha kuwa gerezani ni kubaya, kuna chawa, viroboto na kunguni, halafu hakuna hewa ya kutosha…daddy akikaa sana atakuwa na upele na magonjwa ya ngozi…” Aliongea Geneviv kwa huzuni. Ni wazi kuwa naye alifahamu hatari iliyokuwa inamkabili baba yake.
Lakini Bi Patricia alipozidi kumdadisi kama anawakumbuka wote waliohusika, Geneviv alisita kusema ukweli ambao hakuna mtu mwingine aliyekuwa anaufahamu zaidi yake. Kabla ya kufanyiwa unyama ule na polisi, tayari alikuwa amefanyiwa na wanafunzi wenzake anaosoma nao Shule moja. Kueleza kila kitu kulimaanisha kuwa hata wale wanafunzi nao lazima wangesakwa na kutiwa mikononi mwa sheria kitu ambacho hakutaka kitokee.
Aliamini wale walifanya vile kwa sababu ya uvutaji bangi ambao kwao ilikuwa adhabu tosha. Kama angewataja ingemaanisha kuwa wangefukuzwa shule na kufungwa miaka mingi Gerezani hivyo kuwaachia huzuni ya kudumu wazazi wao na wanafunzi wenzao. Alijikuta akiwaonea huruma kiasi cha kudondosha machozi. Hakutaka jambo lolote baya liwatokee hasa baada ya kujifunza kuwa usilipe ubaya kwa ubaya kwani madhara yake huwa makubwa kuliko unavyotarajia. Akaapa kuwalinda kwa kutowataja.
Lakini bado alishaahidi kuwa atasaidia baba yake atolewe gerezani, hilo lilikuwa jambo lingine zito lililousumbua moyo wake. Alichokifanya ni kumbembeleza mama yake kuwa Daktari asiandike kama alibakwa na watu watano kwani hiyo ingefanya watu wazidi kumuonea huruma na wengine wazidi kumdharau hasa wanafunzi wenzake. Bi Patricia alimkubalia mwanae bila kujua kuwa ameficha siri nyingine.
Akamuomba amsimulie tukio zima jinsi lilivyokuwa ili na yeye amsaidie mawazo ya namna ya kujieleza.
Geneviv alianza kueleza…
“Siku ile nilivyoondoka nyumbani nilikimbilia porini na nikawa sitaki kurudi nyumbani kwa sababu nilimchukia baba halafu nilidhani nimemuumiza sana nilipompiga na stuli kichwani. Nikawa nakimbia kuelekea nisikokujua mpaka nikafika mbali na nyumbani. Nilipoona nimechoka nikaamua kupumzika chini ya mti…”
Alipofikia hapo kuelezea ilibidi aongee uongo kidogo ili kuuficha ukweli wa wale wanafunzi wenzake.Akaendelea…
“Nilipokuja kushtuka nikakuta giza limeshaingia na mvua inanyesha. Nikaamka na kukimbilia barabarani ambako nilianza kutembea kufuata barabara. Baadae nikaona gari linakuja nikaamua kulisimamisha, kumbe lilikuwa ni la polisi. Nikawaambia kuwa wanisaidie nirudi nyumbani… wakanipakiza kwenye gari mpaka pale kituo kikuu cha polisi”
Geneviv alikuwa akieleza kwa ufasaha kabisa, Bi Patricia akawa anamsikiliza kwa makini huku akiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kilichoendelea.Akaendelea tena…
“Tulipofika kituoni walinishusha na kunikabidhi kwa polisi wengine wawili tuliowakuta pale ndani. Wale wengine wakaondoka na kuniacha na wale wawili. Baadae mmoja alikuja akanishika mkono akidai anaenda kunionyesha sehemu ya kulala.Tukaingia kwenye kichumba cha nje pembeni ya kituo. Tulipoingia ndani alifunga mlango na kuniambia nikipiga kelele ataniua na bunduki. Mi sikujua anataka kufanya nini, nikaona anavua suruali yake halafu akaniziba mdomo. Akawa anani… Geneviv alishindwa kumalizia na akawa analia kwa kwikwi. Alikuwa amekumbuka maumivu yaliyoanza kupoa moyoni mwake. Bi Patricia akawa anambembeleza mwanae huku naye akijifuta machozi.Baada ya kutulia akaendelea kusimulia…
“Yule mmoja alipomaliza alitoka nje akanifungia mlango, halafu akaja mwenzake. Na yeye akanifanyia kama yule wa kwanza…nilishindwa kuvumilia nikaanza kulia kwa sauti lakini akaendelea. Mara nikasikia sauti kama ya daddy nje, halafu mlango ukavunjwa. Kweli alikuwa ni daddy na hata sijui alitokea wapi. Akaanza kumpiga yule polisi mpaka akaanguka chini. Daddy akanibeba begani tukatoka nje ambako mvua ilikuwa ikinyesha sana.
Akaanza kukimbia huku amenibeba begani… baada ya hapo sikumbuki kitu mpaka nikajikuta niko Hospitali nimelezwa kwenye kitanda…” Alimalizia kueleza Geneviv huku akijifuta machozi yaliyokuwa yameuloanisha uso wake. Ulikuwa ni ushahidi mzito ambao yeyote ambae angeusikia angemwonea huruma na kulilaani jeshi la polisi lililopewa jukumu la kuwalinda raia na badala yake likageuka na kuwafanyia ukatili mkubwa kama huo wa Geneviv.
Bi Patricia akawa anaendelea kumbembeleza na kumsisitiza kuwa mtu mwingine akija kumuuliza aeleze kama alivyomueleza bila ya kusahau kitu.
Baada ya hapo Bi Patricia alitoka na kwenda ofisini kwa daktari Zayumba ambako alimueleza kwa undani mkasa mzima ulivyokuwa na wakawa wanaendelea kujadili nini cha kufanya.
“Mi nafikiri tumfuate Raisi Ikulu tukamweleze hali halisi labda atatusaidia kwa sababu Raisi huyu mpya ni mpenda haki na huwa hachagui maskini au matajiri,anawasikiliza wote wenye shida.”
Wazo hilo lilipingwa vikali mno na Daktari Zayumba ambaye alieleza wasiwasi wake peupe kuwa swala hilo lisingeshughulikiwa zaidi ya kuanza kuhangaishana mahakamani ambapo mwisho wa siku lazima watuhumiwa wangeachiwa huru kwa kukosekana kwa ushahidi wa moja kwa moja...
“Nakubaliana na wewe kuwa Rais wetu James Kahungo (the JK) ni mpenda haki, lakini tatizo lipo kwa wasaidizi wake ambao kila mmoja anawaza kujinufaisha yeye, kama hiyo haitoshi wana tabia ya kulindana wanapoona mwenzao amefanya maasi…Watateteana na mwisho hakuna lolote litakaloendelea. Mwanao atakuwa ameshaharibiwa na mumeo ataendelea kuozea gerezani.”
Alichokizungumza daktari Zayumba kilikuwa ni kweli kwani nchi ya Blaziniar kwa sasa ilikuwa imetawaliwa na urasimu na hujuma karibu kila idara tofauti na zamani .Viongozi wa juu walikuwa wakifanya maasi na wakikaribia kubainika walikuwa wakiwatumia raia wa kawaida kama ngao kwao.Walikuwa wakipeana kazi wao kwa wao na kulipana mishahara minono huku mwananchi wa kawaida akizidi kuteseka.Kibaya zaidi walikuwa wakijihusisha na vitendo viovu kama ujambazi kwa kuunda makundi yao, huku wengine wakijihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya. Zaidi ya yote, ufisadi na uhujumu uchumi ulikuwa ukizidi kupamba moto. Kwa kifupi serikali ya Blaziniar ilikuwa imepoteza kabisa mwelekeo.
“Sasa wewe unafikiri tutafanya nini? Kinachotakiwa hapa ni kuwafichua wote waliohusika na hatimaye ukweli halisi ufahamike na mume wangu aachiwe huru” Aliongea Bi Patricia kwa masikitiko huku akionekana kukata tamaa.
Kuna mbinu mbili ambazo naamini zitafaa sana… ya kwanza ni kumtafuta mwanasheria ambaye atatusaidia kuendesha kesi…lakini tutahitajika kuwa na pesa nyingi za kumlipa na kuendesha kesi na kuna uwezekano njia hii ikachukua muda mrefu sana mpaka hukumu ya mwisho itolewe.
Lakini hii njia ya pili nadhani ndio inafaa zaidi…Bi Patricia alitega masikio yote mawili kwa makini kutaka kuisikia njia hiyo ya pili ni ipi.
“Njia ya pili ni kutumia vyombo vya habari kama sauti yetu sisi wanyonge.Tutakachokifanya ni kuandaa taarifa zote muhimu kuhusu namna tukio lilivyotokea tukiambatanisha na taarifa ya ushahidi wa kidaktari na kuupeleka kwenye vyombo vya habari ili wananchi wote wa nchi hii wafahamu ukweli unaofichwa na serikali juu ya unyama waliomfanyia Geneviv.”
Njia hii ndio iliyoonekana inafaa zaidi na wote wakaiafiki. Wakaanza kutafakari ni chombo gani cha habari kinachoweza kuwa msaada kwao.
“ Mi nadhani twende pale kwenye ofisi za kampuni ya Planet Link Media, unajua wale wanachapisha magazeti yanayosomwa karibu nchi nzima, halafu Redio yao inasikika pande zote za nchi na kama hiyo haitoshi mmiliki wake ni mtu wa Mungu na anapenda siku zote kuona haki ikitendeka. Naamini atakuwa msaada mkubwa kwetu.”
Baada ya makubaliano hayo, walianza kujiandaa bila kupoteza muda. Geneviv akaandaliwa na kwa kutumia gari la Dokta Zayumba safari ya kuelekea Mwenge zilipo ofisi za Planet Link Media ikaanza. Walipofika waliomba kukutana na mkurugenzi, Bwana Samson Liganga ambapo walionyeshwa ofisi yake ilipo na katibu muhtasi (secretary wake). Baada ya salamu, walianza kueleza kilichowapeleka. Bwana Liganga aliwasikiliza kwa makini huku akinote’ mambo ya msingi kwenye kitabu chake cha kumbukumbu. Walieleza kila kitu kuanzia mwanzo mpaka mwisho, na Geneviv akahitimisha kwa ushahidi mzito ambao ulimuacha bwana Liganga ameduwaa. Alipokuwa akimtazama Geneviv, aligundua kuwa hakustahili kufanyiwa unyama kama ule kwani ukiachilia mbali urembo, bado alikuwa msichana mbichi kabisa.
“Oooh My Lord, pole malaika. Hukustahili kupatwa na yaliyokupata, ila kwa kuwa yameshatokea basi Mungu ndio anayejua.”
Aliongea bwana Liganga kwa masikitiko na baada ya hapo ukimya ukatawala ofisini. Kila mtu akawa amezama kwenye mawazo kivyake… zaidi bwana Liganga ambaye alionekana kuumizwa zaidi. Ilibidi awaombe wafumbe macho ili wasali kwa Mungu wao awaongoze katika vita ile kali iliyokuwa mbele yao. Baada ya sala iliyodumu kwa takribani dakika ishirini ikiongozwa na bwana Liganga mwenyewe, wote waliitikia Aaamen! Wakiwa na imani kubwa kuwa Mungu wao angewatangulia na kuwaonyesha njia ya kupita.
Baada ya hapo bwana Liganga aliitisha mkutano wa dharula na waandishi na watangazaji wa kampuni yake. Sekunde chache baadae wakawa wamekusanyika kumsikiliza bosi wao. Aliwaeleza kitu cha kufanya na muda mfupi baadae kazi ikaanza mara moja. Geneviv akachukuliwa na kuingizwa chumba cha habari ambapo alianza kuhojiwa mara moja huku akirekodiwa na mitambo ya kisasa iliyokuwa ndani ya chumba cha habari.
Masaa machache baadae taarifa ile ikaanza kurushwa hewani na kuwafanya raia wote waanze kuufahamu ukweli halisi wa tukio. Shughuli ilikuwa pevu kwani kila aliyeisikia habari ile alibaki mdomo wazi kwa namna ambavyo jeshi lilikuwa limefanya unyama na kisha kuwadanganya wananchi.
“Tumechoka na serikali ya kibabiloni, tuliwapigia kura ili watutetee, ona sasa na wao wanaungana na polisi kupindisha sheria, mimi nashauri wananchi wote tuandamane mpaka haki itakapochukua mkondo wake, tumechoka, tumechoka….”
Alisikika mwananchi mmoja akitoa maoni yake redioni baada ya kuusikiliza kwa makini mkasa ule. Watu walizidi kutoa maoni yao ambapo kila mmoja alisisitiza kuwa lazima wananchi wote waandamane kumtetea binti yule na baba yake na kuwashikisha adabu wote waliohusika.
Habari ile ilizigusa hisia za watu wengi mno kiasi cha kusababisha vuguvugu kali miongoni mwa raia wote wa Blaziniar.
****
Mambo yameanza kuchangamka, wananchi wamekuja juu mno baada ya kuubaini ukweli na sasa wanaishinikiza serikali…
“Huu ndio unaoitwa mchezo mchafu, iweje hawa polisi watuchezee akili kama watoto wadogo? Kumbe matangazo yale yote waliyokuwa wanadai kituo kimevamiwa na silaha zimeibwa ilikuwa ni uzushi mtupu wakijaribu kuficha uozo wao, haiwezekani…”
Hayo yalikuwa ni mazungumzo ya mmoja kati ya watu wengi waliokuwa wameanza kujikusanya makundi makundi karibu nchi nzima wakifuatilia kwa makini kilichokuwa kikitangazwa redioni kuhusu yaliyomsibu binti mdogo Geneviv.
“Enough is enough, inatosha sasa…tumechoka kuonewa! No more tears…”
Aliongea mzee maspedi kwa mbwembwe na kushangiliwa na wenzake waliokuwa wakimsiliza.
Vuguvugu lile liliendelea kushika kasi na kusambaa nchi nzima kama moto wa nyikani huku kila mmoja akilipokea kwa hisia tofauti. Wengi walionekana kuchoshwa na uonevu wa serikali yao kupitia vyombo vyake kama polisi, mahakama na bunge.
Ikawa “nkhondo igwa” nchi nzima. Watu wakaanza kujiandaa kufanya mgomo mkubwa nchi nzima kuishinikiza serikali iwachukulie hatua kali wote waliohusika na wafungwa wote wanaoshikiliwa kiuonevu wakiongozwa na mzee Rwakatare waachiwe huru.
Hakuna aliyeonekana kufanya mzaha tena, kila mtu alidhamiria kuukomesha uonevu wa serikali kwa wananchi wake. Wengi walianza kuamini ule msemo usemao wanaokwenda jela sio wote wana hatia…na sasa kila mmoja alianza kuona ukweli.
“Ndiyo mchezo wao hao, mbona wengine tulishashtuka siku nyingi kabla, tuungane tuukomeshe unyanyasaji kama huu, tatizo na sisi wananchi tumezidi woga, tunaona mambo ya ajabu yanafanyika nchini mwetu tunabaki kimya na kuwa watazamaji, sote tuamke....” Ilikuwa ni kelele mtindo mmoja huku watu wakishangilia kila hoja ilipokuwa inatolewa.
*****
Habari zilizidi kuenea kwa kasi ya ajabu mpaka zikamfikia Raisi ikulu. Ilibidi awaite wasaidizi wake mapema kabla mambo hayajaharibika zaidi kwani kulikuwa na ripoti kutoka sehemu mbalimbali za nchi kuhusu wananchi kutaka kuandamana nchi nzima.Kikao cha dharula kikaitishwa ndani ya Ikulu na maafisa wote wa polisi na usalama wakaitwa.
Raisi alionekana kuchanganywa na habari zilizokuwa zimetapakaa nchi nzima na sasa akawa anahangaika kutuliza mambo kwani alijua kuwa kama atazembea na kutanguliza kujuana na uswahiba angezidi kuwaudhi wapiga kura wake ambao nao walishapoteza imani naye na serikali yake. Ilibidi awe mkali sana ili kuhakikisha ukweli unapatikana haraka sana.Tofauti na maraisi waliokuwa wamemtangulia ambao walikuwa wakipenda kuunda tume kufuatilia mambo kama yale na kupoteza pesa nyingi za walipa kodi na muda, yeye aliamua kulivalia njuga swala lile mwenyewe na kuingia kazini.
Alianza na maafisa wa juu wa polisi ambapo aliwataka waeleze ukweli ni upi kati ya taarifa waliyokuwa wameitoa wao kwa vyombo vya habari na ile waliyoitoa waathirika wa unyanyasaji ule wa mtoto Geneviv na baba yake.
“Hii ni aibu kubwa sana kwangu na kwa serikali nzima. Wananchi wanatulaumu na sasa tumepoteza imani kabisa kutoka kwa wapiga kura wetu.Sijui tufanye nini ili warudishe imani yao kwetu… Mimi kama mkuu wa nchi siwezi kuvumilia kuona hadhi yangu na umaarufu mkubwa niliojijengea unachafuliwa kwa ujinga wa wachache kati yenu.
Lazima niufahamu ukweli mara moja… na ikigundulika kuna uzembe wa aina yoyote hapa, wote mliohusika mtawajibishwa vikali mara moja”
Alikuwa akifoka Raisi James kahungo wakati akiendelea na kikao chake cha dharula na maafisa wakuu wa jeshi la polisi. Baada ya kuongea kwa kifupi, raisi aliamua kuongozana na maafisa wa polisi mpaka kituo kikuu cha polisi ambako iliripotiwa kuwa ndio kile walichokitangaza polisi kama ujambazi ulitokea.
Msafara ule mrefu ulifika kituoni ukiongozwa na raisi mwenyewe na alipofika tu aliwataka Maafisa wa polisi na mkuu wa kituo waeleze na kuonyesha ushahidi wa namna ambavyo kituo hicho kilivamiwa, ghala ya silaha ikavunjwa na polisi kuuwawa kama walivyokuwa wametoa taarifa kwenye vyombo vya habari siku chache zilizopita.
Si mkuu wa kituo wala maafisa waliokuwa tayari kutoa maelezo yaliyonyooka mbele ya Raisi ambaye sasa alikuwa amefura kwa hasira. Wote wakawa wanajikanyaga huku wakitetemeka.
Ukweli ambao ulimshangaza hata Raisi mwenyewe ni kwamba hakukuwa na dalili yoyote ya kuvamiwa kwa kituo kile.
Ghala la silaha lililodaiwa kuvunjwa na majambazi halikuwa na alama yoyote ya kuthibitisha kama ni kweli lilivunjwa ingawa walipoingia ndani waligundua kuwa silaha nyingi hazikuwemo.
Hili nalo halikupata jibu la haraka na la kuridhisha na maafisa wale na mkuu wa polisi kila walipokuwa wakiulizwa hawakuwa na majibu zaidi ya kuanza kutetemeka kila mmoja kivyake.
“Nataka maelezo kuhusu hili, sio kuchekecheka hapa. Unamchekea nani wakati wananchi wangu wanalia…na nchi inaangamia?”
Raisi alikuwa akimfokea mkuu wa kituo ambaye alionekana kuleta mizaha kwenye maelezo yake. Hakuwa na majibu yenye kujitosheleza na badala yake akawa anatanguliza samahani nyingi kwa Raisi.
Baada ya kutoka kwenye Ghala la silaha, Raisi aliomba kupelekwa nyumbani kwa askari aliyedaiwa kuwa aliuawa na majambazi ambapo pia hakuna aliyeweza kuonyesha wala kuthibitisha kuwa ni kweli kuna askari aliuliwa.
Alipoona wote wanatupiana mpira akaomba kutajiwa jina lake, lakini pia hakupata jibu. Akagundua kitu ingawa hakupenda kuwa na maelezo mengi.
Alipoenda kukagua vyumba vya nje ambavyo mtoto Geneviv wakati akihojiwa redioni alieleza kuwa ndiko alikofanyiwa ukatili ule, aligundua kuwa ni kweli mlango ulikuwa umevunjwa na alipoingia ndani alishuhudia mwenyewe kwa macho yake, damu nyingi zikiwa zimeganda na kukauka juu ya kitanda kidogo kilichokuwa mle ndani na pale chini sakafuni.
Alipoomba ufafanuzi wa hilo, pia hakukuwa na majibu zaidi ya kila mmoja kuonekana akijikanyaga kwa hofu.
Raisi alipotoka aliingia mpaka ofisini kwa mkuu wa kituo ambako aliomba majina ya askari wote waliokuwa doria na wale waliokuwa zamu siku ya tukio.
Katika hali ya kushangaza mkuu wa kituo alianza kuwatetea kuwa wao walikuwa kazini na kama yalitokea makosa basi kwa niaba yao anaomba wasamehewe kwani wao ni binadamu na hukosea.
Kwa hali aliyokuwa nayo Raisi Kahungo, alishindwa kuzizuia hasira zake na akajikuta amerusha ngumi iliyompata sawia mkuu wa kituo na kumfanya apepesuke huku akitaka kuanguka kabla ya kudakwa na wenzake. Mara moja Raisi akatoa amri ya mkuu yule wa kituo kuwekwa chini ya ulinzi.
Wanajeshi wa jeshi la watu wa blaziniar (Blaziniar Force Unit) wakapewa jukumu hilo. Ndani ya muda mfupi mkuu wa kituo akawa ndani ya karandinga la jeshi chini ya ulinzi mkali.
Raisi aliwazuia wasimpeleke kwanza kwenye gereza la kijeshi mpaka atoe maelezo ya askari waliokuwa zamu siku ya tukio. Akawa anashindwa kueleza huku akilia kama mtoto. Alikuwa amezoea kunyanyasa sana Raia lakini leo ilikuwa zamu yake.
Rais kahungo hakuwa na masihara tena. Alikuwa amechukia na kuvimba mithili ya nyoka koboko mwenye sumu kali.
Akaitwa msaidizi wa mkuu wa kituo na kuamriwa kutoa majina ya watu waliokuwa zamu siku ya tukio. Baada ya kuona hali aliyokuwa nayo rais, alianza kutetemeka na kutafuta faili lililokuwa na kumbukumbu zote za wafanyakazi.
Akatoa karatasi lenye majina ya watu kumi, ambao wawili kati yao ndio waliokuwa pale kituoni usiku wa siku ya tukio na wengine nane walikuwa Doria.
Akaagiza wote kumi watiwe nguvuni na bila kupoteza muda jeshi likaanza kuwasaka na muda mfupi baadae wakapatikana. Baada ya kupatikana wote, mmoja alionekana kuwa na jeraha kubwa kichwani ambalo alilificha kwa kuvaa kofia kubwa.
Raisi akawa anapita mbele ya kila mmoja akiwakagua na kuwahoji maswali makali.
Alipofika kwa yule mwenye jeraha, alimvua kofia kwa nguvu na akaanza kukumbuka maelezo ya mtoto aliyefanyiwa ukatili wakati akihojiwa redioni.
Akagundua kuwa huyo ndio yule aliyekutwa na baba wa mtoto mzee Rwakatare kisha akapigwa kichwani na kitu kizito. Alipomhoji huku akimkazia macho kuwa lile jeraha kichwani lilisababishwa na nini, alishindwa kujibu na akajikuta akiachia haja ndogo.
Wote waliomshuhudia waliangua kicheko baada ya kumuona yule polisi akiwa hana ujanja mbele ya Raisi mpaka kushindwa kujizuia.
Pamoja na watu karibu wote kucheka, Rais alionekana kuvaa sura ya kazi akiwa hana hata chembe ya mzaha.
Aliendelea kukunja sura huku akizidi kumsogelea yule polisi. Katika hali nyingine, Rais alishindwa kuzuia hasira zake na akajikuta akirusha kibao kizito ambacho kilimpata na kumfanya aanguke mzimamzima kama mzigo mpaka chini.
Wenzake wakamuinua na akawa anaendelea kumhoji maswali magumu. Watu wote walipigwa na mshangao wakiwa hawaamini kama ni yule Raisi waliyemzoea ndio alikuwa mkali kiasi kile, wakajua kuwa kweli moto unawaka.Akatoa amri kuwa wale polisi wote kumi waliokuwa zamu siku ya tukio nao waunganishwe na mkuu wao wa kituo na wapelekwe gereza la kijeshi kwa ajili ya kushikishwa adabu.
Muda mfupi baadae karandinga la jeshi likiwa na watu kumi na moja likaanza safari ya kuwapeleka watuhumiwa kweye gereza kuu la kijeshi.Raisi na msafara wake wakaelekea hospitali alikolazwa mtoto Geneviv akiendelea kupata matibabu. Alitaka kwenda kumuona mwenyewe mtoto aliyefanyiwa ukatili ule wa kutisha.
Muda mfupi baadae msafara ulikuwa tayari pale Hospitali na Raisi akafikia ofisini kwa Daktari mkuu, Barikieli Zayumba ambaye alienda kumuonyesha wodi aliyolazwa Geneviv. Hakutaka mtu mwingine yeyote aingie nae wodini zaidi ya Daktari Zayumba.
Raisi akakutana ana kwa ana na Geneviv na mama yake Bi Patricia aliyekuwa aamejiinamia pembeni ya kitanda alicholala mwanae. Kwa ile hali ambayo Rais James kahungo aliishuhudia pale wodini, ilitosha kumdhihirishia namna ambavyo wananchi wake walikuwa wakiteseka.
“Pole binti kwa yote yaliyokukuta! Pole sana”
Rais alikuwa akimpa pole Geneviv huku akimsikitikia sana. Alisalimiana pia na Bi Patricia na akawahakikishia kuwa ameamua kulifuatilia swala lile yeye mwenyewe na haki lazima ingepatikana baada ya muda mfupi. Alikaa juu ya kitanda cha Geneviv na kumuomba amsimulie hali halisi jinsi ilivyokuwa.
Geneviv bila wasiwasi alimsimulia kila kitu kama alivyosimulia redioni.
Hakuacha kitu. Pamoja na ukakamavu aliokuwa nao Rais, alijikuta akishindwa kuyazuia machozi yasimtoke. Alimuonea huruma mno na hata yeye alikiri kwamba hakustahili kutendewa namna ile kutokana na jinsi alivyokuwa. Baada ya kumaliza kumsikiliza Geneviv, aliaga na akaahidi atarudi tena kumjulia hali binti Geneviv.
Alipotoka nje, wafuasi wake wote walikuwa wakimsubiri mlangoni na wote walishuhudia namna alivyobadilika usoni. Macho yalikuwa mekundu sana kuonyesha kuwa alikuwa akilia. Wakajua hukumu iliyokuwa mbele ya wahusika isingekuwa ya mchezo.
Wote walikuwa wakinong’onezana chini chini kwamba kama Rais angekuwa hivyo kufuatilia mambo yote, hakika nchi ingefika mbali sana kimaendeleo na kidemokrasia.
Baada ya kutoka hospitali msafara uliongoza mpaka gerezani alikokuwa amefungwa Mzee Rwakatare.
Mzee Rwakatare alikuwa amefungiwa ndani kabisa ya gereza kiasi cha kutotambua kilichokuwa kikiendelea katika ulimwengu wa kawaida. Aliamini huo ndio ulikuwa mwisho wake na akawa analia kwa kuiacha familia yake bila mwongozo.
Kule ndani alikofungiwa kulikuwa na giza muda wote kiasi cha kushindwa kutofautisha mchana na usiku. Alikuwa hajui chochote kinachoendelea Uraiani kwa kuwa alizuiwa kukutana na mtu yeyote kutoka nje hata mke wake.
Alijua kuwa kipindi chake cha maisha aliyobakiza hapa duniani kingeishia mle gerezani na akawa hana mategemeo kabisa ya kunusurika. Alichokuwa akikifanya muda wate ilikuwa ni kumlilia Mungu wake amsamehe dhambi zake zote na azidi kuilinda familia yake ambayo sasa ilibaki bila baba.
Baada ya kufika eneo lilipo Gereza kuu, Rais James Kahungo aliamuru mzee Rwakatare atolewe kwa ajili ya kufanya naye mahojiano maalum. Mzee Rwakatare alikuja kushtuka kutoka kwenye lindi zito la mawazo baada ya kusikia mlango mkubwa wa chuma wa kuingilia kule alikokuwa amefungwa ukifunguliwa. Akajua siku ya kwenda kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka imefika.
Akabaki amekaa vilevile kama alivyokuwa, akimwangalia askari magereza aliyekuwa akihangaika kufungua mlango. Tofauti na alivyotarajia, yule askari magereza alimletea nguo zake alizovuliwa wakati akiingizwa mle gerezani na kwa upole akamwambia kuwa ajiandae haraka kwani kuna mtu muhimu sana amekuja kumtembelea.
Mzee Rwakatare akabaki akijiuliza maswali mengi bila majibu. Kwanza kitu cha kwanza alishangaa kwa jinsi yule askari magereza alivyokuwa mpole kwake tofauti kabisa na siku zote.Pili alishangaa ni nani aliyeruhusiwa kuja kumuona wakati mkuu wa gereza alishatoa amri kuwa asiruhusiwe mtu yeyote kuja kumtembelea. Alipomtazama yule askari usoni alisoma kitu, ikabidi aendelee kuvaa kama alivyoambiwa. Ieleweke kwamba gereza hili lilikuwa na utaratibu mgumu na wa ajabu kwani baada ya mtu kuingizwa ndani, huamriwa kuvua nguo zote na kisha kupewa kaptura chafu ya magereza yenye chawa wengi huku ukiachwa kifua wazi. Kwa muda mfupi tu aliokaa mle ndani, mzee Rwakatare alikuwa amedhoofika sana kiasi cha mbavu zake kuanza kuhesabika.
“Tafadhali fanya haraka mzee!”
Yule askari alizidi kumhimiza mzee Rwakatare kwa sauti ya upole.
Baada ya kuwa tayari, walitoka na kuanza kuelekea ofisini kwa mkuu wa gereza. Akiwa anazidi kwenda alishtushwa na umati mkubwa wa watu ambao aliwatambua kwa haraka kuwa ni viongozi wa juu wa serikalini, huku nje kukiwa na msururu mrefu wa magari. Alishindwa kuificha hofu yake na sasa akawa anatetemeka mwili mzima.
Baada ya kuingia ofisini huku akiwa bado anatetemeka, macho yake yalikutana ana kwa ana na Raisi James Kahungo. Akajua swala lake limekuwa kubwa sana, mpaka Rais amekuja gerezani. Aliona huo ndio muda muafaka wa kujitetea kwa kadri ya uwezo wake wote mbele ya mkuu wa nchi.
“Lakini mimi sio jambazi wala muuaji mheshimiwa Raisi, wamenisingizia tu…sio kweli”
Alianza kujitetea hata bila salamu wala kuruhusiwa kuongea. Mheshimiwa Raisi alisimama na kuamuru watu wote waliokuwa mle ofisini watoke nje na kumuacha na mzee Rwakatare. Baada ya sekunde kadhaa, wakabaki wawili tu.
“Pole sana kwa yaliyokukuta, nimeshaujua ukweli wote na hivi unionavyo nimetoka Hospitali alikolazwa mwanao. Amini nakuambia jogoo hatawika asubuhi ya kesho kabla hujaungana na familia yako.”
Mzee Rwakatare hakuamini alichokisikia kutoka kwa Raisi wake. Alikuta moyo ukimlipuka kwa furaha kiasi cha kuruka juu na kumkumbatia Rais james Kahungo kwa nguvu.
“Kwa kuwa umekisikia kilio changu na kuja kunifungua minyororo ya uonevu na kuniahidi uhuru, nami ntakupa siri nzito ambayo hakuna anayeweza kukwambia.”
Kwa Furaha aliyokuwa nayo, Mzee Rwakatare alijikuta akianza kuropoka na kutoa siri.
Rais alitega sikio na kuanza kumsikiliza kwa makini.Akaendelea…
“Natambua kwamba wewe ni mwanamapinduzi halisi na ndio maana leo uko hapa.
Nitakachokuambia kifanyie kazi na utaubaini ukweli. Kati ya watu zaidi ya mia tatu uliotusimamisha kazi serikalini kwa tuhuma za ufisadi na uhujumu uchumi nikiwepo na mimi,umetuonea kabisa. Ukweli ni kwamba sisi tumegeuzwa ngao ya wakubwa ambao bado wako madarakani na unashinda nao ikulu.
Mafisadi ni hawa ulioongozana nao na niko tayari kukusaidia kuufahamu ukweli wa namna wanavyokuzunguka na mwisho wa siku wanatubebesha sisi watu wa chini misalaba…amini nakwambia, una kazi ngumu sana ya kujisafisha kwani tayari wananchi wamepoteza imani. Nipe nafasi nikusaidie na hii itakuwa kama shukrani yangu kwako kwa kunitoa gerezani.”
Mzee Rwakatare alihitimisha maelezo yake na kumuacha rais akiwa ameduwaa. Mzee Rwakatare alionyesha kuwa na siri nzito sana…na hili lilidhihirishwa na lugha ya macho aliyokuwa akimuonyesha raisi.
“Ok nimekuelewa vizuri na baada ya kutoka humu jioni ya leo nitakuhitaji usiku uje ikulu ili unipe taarifa rasmi. Usimwambie mtu mwingine yeyote na uwe kimya mpaka nitakapotuma mtu kuja kukuchukua usiku wa leo.”
Rais aliinuka na kumuita mkuu wa gereza ambaye aliingia akiwa anakimbia.
Alimuachia maagizo kuwa Mzee Rwakatare aachiwe huru mara moja na ahakikishe anapewa ulinzi na kupelekwa mpaka nyumbani kwake.
Safari ya kurejea ikulu ikaanza huku Rais James Kahungo akiwa na mawazo tele kichwani. Alishindwa kuamini kama kweli watu wake aliowaamini kwa kiasi kikubwa wanaweza kumgeuka na kumsababishia ugumu wa kazi namna ile.Aliapa kuendeleza vita mpaka imani yake kwa wananchi irejee.
Wakati mzee Rwakatarea akimtonyaRaisi kuhusu siri nzito aliyokuwa nayo kuhusu uhujumu nchi na ufisadi, Baadhi ya mashushushu wa viongozi wakubwa waliokuwa nje, walikuwa wakisikiliza mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea ndani kwa kutumia mitambo maalumu iliyokuwa imetegwa ndani ya chumba cha mkuu wa gereza.
Baada ya kufika ikulu na kumuacha Rais apumzike kwa kuwa alikuwa amechoka, taarifa za chinichini zikaenea miongoni mwa vigogo ambao waliitisha mkutano wa siri haraka sana.Ajenda kubwa ikawa ni kumuwahi mzee Rwakatare kabla hajatoa siri kubwa kwa Raisi.“Yule bwana tusipokuwa makini atatuharibia kila kitu kwa sababu anafahamu siri zetu nyingi na hasa wizara ya nishati na madini alikokuwa anafanyia kazi.Inabidi tumuwahi na kumpoteza kabla ya usiku hajakutana na Raisi.”
Alitoa hoja kigogo mmoja na kuungwa mkono na wenzake.
“Lakini lazima tuwe makini sana, kwa sababu Raisi akigundua mchezo huu tumekwisha… si mmemuona alivyokuwa leo? Halafu hata wananchi nao wameshaanza kushtuka, lazima tuwe makini”
Kigogo mwingine alitahadharisha hatari iliyokuwa mbele yao na kuwafanya wenzake wakune vichwa. Ilikuwa ni lazima mpango kabambe wa kumuua Mzee Rwakatare uandaliwe siku ileile kabla hajaenda kukutana na Raisi ili kuzidi kuuficha ukweli. Kikao cha siri kiliendelea kwa muda wa masaa matatu mfulilizo na hatimaye muafaka ukafikiwa…ikabakia utekelezaji.
Baada ya muda mfupi kupita tangu mkuu wa gereza aachiwe maagizo na ya kumuachia huru mzee Rwakatare, kweli alitekeleza alichoambiwa.Mzee Rwakatare aliachiwa huru na kupewa ulinzi wa kumrudisha mpaka nyumbani kwake salama.Alipofika nyumbani kwake alikuta nyumba ikiwa kimya kabisa, akajua bado mkewe na Geneviv wako Hospitali, bila kupoteza muda akaingia bafuni kutoa uchafu wote wa gerezani na baada ya hapo alizichoma moto nguo alizokuwa amezivaa na akawa anajiandaa kuelekea Hospitali.Alikuwa bado haamini kama ni kweli ameachiwa huru…alijihisi kama yuko ndotoni. Akiwa bado anajiandaa alisikia mlango ukigongwa. Akatoka kwenda kufungua.
“Ooooh my Lord, welcome back home! God is great…”
Walikuwa ni Bi Patricia na mwanae Geneviv baada ya kuruhusiwa kutoka Hospitali. Ilikuwa ni furaha isiyo kifani kukutana tena pamoja baada ya misukosuko mizito. Walikumbatiana pale pale mlangoni huku wakiwa wameshikana mikono. Wote walikuwa wakitokwa na machozi ya furaha wakiwa hawaamini kilichotokea. Waliendelea kukumbatiana kwa muda mrefu huku kila mmoja akiendelea kulia kwa furaha.
“Haya twendeni ndani, yote yametimia…Mungu akiwa nasi nani wa kutuzuia?”
“Hakunaa!” wote waliitikia na kuinuka kuelekea ndani. Walipofika sebuleni walianza upya kumshukuru Mungu wao kwa kuwakutanisha upya. Waliendelea kusali huku wakiwa wameshikana mikono. Walikaa kwa muda mrefu sana mpaka giza likaanza kuingia. Walisitisha maombi na wakaanza kusimuliana yote yaliyotokea kipindi ambacho walikuwa wametengana. Zilikuwa ni taarifa za kusisimua mno.
Baada ya kusimuliana sana, Mzee Rwakatare aliwapa taarifa juu ya mwaliko wa Rais wa kwenda ikulu jioni hiyo.
“Lakini kwani ni lazima uende leo, mi nafikiri usiku mzima wa leo tungeendelea kumuomba Mungu kwa miujiza aliyotufanyia, tutulie ndani mume wangu, huko utaenda hata siku nyingine..”
Bi Patricia alitoa hoja ya msingi sana, lakini mzee Rwakatare akawa mbishi na wakaanza kubishana kila mmoja akitetea wazo lake.
“Lakini lazima ujue kwamba mheshimiwa Rais ndiye aliyenisaidia mpaka muda huu tuko pamoja, lazima tumlipe fadhila.”
“Ni sawa mume wangu,lakini Mungu ndiye aliyewezesha yote haya. Tumlipe fadhila kwanza Mungu halafu siku nyingine ndio uende huko. Kwani cha msingi kinachokupeleka huko ni nini?”
“Naenda kuwafichua wote wanaoihujumu nchi yetu hasa kwenye ofisi niliyokuwa nafanya kazi, Nawafahamu wote na nazijua mbinu wanazozitumia, nimeshamwahidi Rais kuwa nitamsaidia…na amesema atamtuma mtu kuja kunichukua usiku huu” Alizidi kusisitiza mzee Rwakatare huku aking’ang’ania hoja yake.
“Mungu wangu, yaani hili halijaisha vizuri unataka kutuletea matatizo mengine, wewe hao mafisadi unafikiri watakuangalia vizuri unapoenda kuwachoma mbele ya Rais, tafadhali mume wangu…mambo ya siasa za nchi yetu achana nayo,bado tunakuhitaji…please don’t go!”
Wakiwa bado wanabishana, mara wakasikia muungurumo wa gari likija pale nyumbani kwao. Walipofunua pazia na kuchungulia nje,waliliona gari kutoka ikulu likipaki nje ya nyumba yao. Wakatazama…
“Niruhusu niende tu mke wangu, nilishamuahidi mkuu kuwa lazima niende na kama unavyoona ameshatuma mtu kuja kunichukua, haitakuwa busara kukaidi na ataona kama tumemdharau…please niruhusu!”
Mzee Rwakatare alikuwa akizidi kumshawishi mkewe amruhusu. Moyo wa Bi Patricia ulikuwa mgumu sana kumruhusu mumewe kuondoka. Yeye mwenyewe hakuelewa ni kwa nini hali ile ilimtokea, lakini ni kwamba moyo ulikuwa mgumu sana na akajikuta akiingiwa na hofu juu ya usalama wa mumewe. Geneviv alikuwa kimya akisikiliza mazungumzo ya wazazi wake. Hakuweza kuchangia chochote kwani alikuwa bado hajarudiwa na nguvu zake vizuri baada ya kutoka Hospitali.
Baada ya kuona mumewe akizidi kushikilia msimamo wake, ilibidi amruhusu kwa shingo upande.
“Daddy don’t delay…we will be missing you, and I got something special to let you know this night..” (Baba usichelewe kurudi, bado tunahitaji kukaa na wewe halafu kuna kitu maalum nataka nikuambie ukirudi)
Geneviv aliongea kwa sauti ya chini huku akimsindikiza baba yake kwa macho wakati akitoka kuelekea pale lililopaki gari kutoka ikulu. Alipofika nje aligeuka na kumwangalia mkewe aliyekuwa amejiinamia mlangoni, akampungia mkono na kuingia ndani ya gari. Safari ikaanza kuelekea ikulu.
Kichwani mwake alikuwa akishangilia ushindi kwa jinsi ambavyo angeenda kuwafichua wote wanaoihujumu nchi yao na kuwafanya kila siku wananchi wake wazidi kuwa maskini. Nitaeleza kila kitu… hata kama wakija kuniua bora kufa kishujaa kuliko kuishi kama ng’ombe. Bora kujitoa sadaka kwa ajili ya nchi yangu. Nitasema kila kitu bila kujali litakalonikuta. Mimi ni mwanaume kamili na lazima niutetee uanaume wangu kwa kuushinda woga na kuufichua uozo wa viongozi wetu…Do it or die”
Mzee Rwakatare alikuwa akijisemea moyoni peke yake. Kweli alidhamiria kutoka ndani ya moyo wake kuwa chachu ya mabadiliko nchini mwake. Safari iliendelea na sasa wakawa wameingia barabara kuu ya kuelekea ikulu.
“Dereva tafadhali punguza mwendo, unakimbilia wapi saa hizi? Twende taratibu na tut…
Kabla hata hajamalizia kusema sentensi yake, mzee Rwakatare kwa macho yake aliona roli kubwa lililobeba mawe likiingia barabarani mita chache mbele yao na kuzuia njia. Kufumba na kufumbua walishuhudia gari lingine kama lilelile likija kwa kasi ya ajabu likitokea nyuma yao, wakawa katikati… kufumba na kufumbua kikasikika kishindo kikubwa kama bomu na gari walilopanda mzee Rwakatare na dereva kutoka ikulu likawa kama chapati. Lilikuwa limegongwa vibaya na kukandamizwa katikati ya maroli mawili yote yakiwa yamejaza vifusi vya mawe ya kujengea. Hakukuwa na uwezekano wa mtu kutoka salama.
*****
“Bosi kazi yenu tayari imekamilika tunachokitaka ni mzigo wetu”
Kiongozi wa kundi hatari la majambazi ya “Bandidu killers” alikuwa akiongea kwa simu na mmoja wa vigogo waliokuwa wamekaa nao kikao cha siri cha kumpoteza mzee Rwakatare. Waliahidiwa mamilioni ya dola za kimarekani kama wangemuwahi kabla hajafika ikulu.
“mnasema kweli? Kwa hiyo safari ya ikulu imeshakuwa ya kuzimu? Kazi nzuri sana vijana, tunakuja sasa hivi palepale tulipokutana mchana. Mzigo wenu uko tayari na bila shaka mtafurahi wenyewe.” Ulisikika upande wa pili ukijibu kwa furaha na bila kupoteza muda wakaendaa kukutana pale walipokuwa wamekaa kikao cha siri mchana.
“Kwa hiyo mna uhakika hakuna hata mmoja kati yetu atakayehusishwa na kifo chake” Alihoji mmoja wa vigogo wakati akiwakabidhi Bandidu killers mfuko uliojaa dola za kimarekani.
“Ile ni ajali na tumefanya kama mlivyotuagiza. Hakuna hata mmoja kati yenu atakayehusishwa kwa sababu ajali ni ajali na inaweza kumkumba yeyote muda wowote”
Alijibu kwa sauti nzito kiongozi wao na baada ya makabidhiano kila mmoja akatawanyika wakila kiapo cha kila mmoja kutunza siri ile.
Raisi James kahungo alikuwa tayari ameshaingia kwenye ofisi yake ndogo akimsubiri dereva wake amlete mzee Rwakatare ili ampasulie siri nzito. Alikuwa na hamu kubwa ya kutaka kuwajua hao wanaomzunguka na alijiapiza kuwashikisha adabu bila kujali vitambi vyao.
Akawa anaendelea kungoja. Muda nao ukawa unazidi kuyoyoma huku kukiwa hakuna dalili ya mtu yeyote kuingia ndani. Akaanza kupatwa na wasiwasi. Akainua simu ya mezani iliyokuwa pale mezani kwake na kujaribu kumpigia dereva wake, lakini hakupatikana.
“Whats wrong with them?” Utulivu ulimuisha na akawa anazunguka huku na huko mle ofisini kama anayetafuta kitu. Aliirudia tena ile namba ya dereva wake lakini bado ikawa haipatikani. Ikabidi amtafute mmoja kati ya vijana wake aliokuwa anawaamini kutoka kitengo cha usalama wa taifa. Akampa jukumu la kufuatilia kujua ni nini kilichotokea mpaka muda ule dereva aliyetumwa kumchukua mzee Rwakatare hajarudi na simu yake haipatikani. Hakujua kinachoendelea. Muda huo tayari ilishafika saa tano za usiku.
Wakati akiendelea kumsubiri yule kijana aliyemtuma arudishe majibu, alisikia taarifa ya dharula” Breaking news” ikisomwa kutoka kituo cha redio cha Planet Link fm, ikiripoti kuwa magari matatu likiwemo gari la ikulu yalikuwa yamepata ajali mbaya ya sana ya kugongana na kwamba polisi walikuwa wakiendelea kuhangaika kuwaokoa watu waliokuwa ndani ya magari yale ingawa taarifa iliendelea kueleza kuwa shughuli ya uokoaji imekuwa ngumu kutokana na mawe yaliyokuwa kwenye malori mawili kulifunika gari la ikulu na kulifanya liwe “nyang’anyang’a”.
“Mungu wangu! Whats the hell is this, ntawaambia nini wananchi kama mzee Rwakatare amekufa kwenye ajali? Bila shaka wataamini mimi ndie niliyemuua…”
Rais James Kahungo alipata mshtuko mkubwa sana baada ya kusikia taarifa ile, na akajikuta mwili ukimuisha nguvu na akili ikiacha kufanya kazi. Akadondoka chini na kupoteza fahamu.
Taarifa ile pia ilisikiwa na Bi Patricia ambaye baada ya kusikia tu, alitoa kauli moja tu…
“Nilijua lazima kuna njama za kumuua mume wangu,ona sasa…”
Naye akajikuta mapigo ya moyo yakimwenda mbio na mwili ukikosa nguvu, vikifuatiwa na kizunguzungu kikali kilichomfanya apoteze fahamu.
*****
Usiku ule ule habari zilienea kwa kasi huku kila aliyesikia akihisi kuna njama kali ambazo zilikuwa zimepangwa za kumuangamiza, kila mtu alikuwa haamini masikio yake. Vuguvugu ambalo lilikuwa limeanza kutulia likaanza kulipuka upya.
Shughuli za uokoaji ziliendelea mahali ilipotokea ajali mbaya baada ya magari matatu kugongana, likiwemo gari la ikulu ambalo ndani yake kulikuwa na watu wawili, dereva kutoka ikulu na mzee Rwakatare.
Taarifa za awali zilionyesha kuwa hakuna uwezekano wa mtu yeyote kutoka akiwa hai kwenye ajali ile kwa jinsi ambavyo gari la ikulu lilikuwa limebondeka baada ya kubanwa katikati ya maroli mawili yaliyokuwa yamejaza mawe makubwa. Ajali ilitisha na ikageuka kuwa gumzo la nchi nzima. Hiyo ilimaanisha kuwa huo ndio mwisho wa mzee Rwakatare na safari yake ya kuelekea ikulu ikawa imegeuka na kuwa ya kuzimu.
Ilikuwa ni kama simulizi isiyokwisha. Wananchi walikuja juu hasa baada ya ajali yenyewe kuonekana dhahiri ilikuwa imepangwa na wakawa wanamshinikiza Raisi ajiuzulu huku wengine wakimtaka avunje baraza lake lote. Hata baada ya uokoaji kukamilika, miili iliyopatikana ilikuwa haitamaniki kutokana na jinsi ajali ilivyokuwa mbaya na huo ndio ukawa mwisho wa kusikitisha wa mzee Manuel Rwakatare.
Bi Patricia alikuwa hajitambui na kila fahamu zilipomrudia, alikuwa akizimia tena, akiwa haamini kama ni kweli mumewe ndio ametangulia mbele za haki kwa namna ile. Maelfu ya watu walikusanyika nyumbani kwa mzee Rwakatare na mipango ya mazishi ikaanza kuandaliwa. Kila mtu alizungumza lake lakini ukweli ukabaki kuwa palepale. Mzee Rwakatare alikuwa ameshatangulia mbele za haki.
“Rest in peace daddy! May God grant you eternal light… R.I.P”
Pumzika kwa amani baba, Mungu akujaalie mwanga wa milele, pumzika kwa amani”
Alikuwa aliongea Geneviv na kuwafanya waombolezaji waliokuwa wamejaa pale nyumbani kwao kuzidi kulia kwa simanzi kubwa.
Kwa Geneviv hali ilikuwa mbaya zaidi kwani sasa matukio ya ajabu na mikosi yalikuwa yamekolea. Pengo la kuondokewa na baba yake likawa ni pigo jingine lililozidi kumfanya atoe machozi…Soo many tears(Machozi mengi sana).
Mambo yalikuwa mabaya zaidi kwa Rais ambaye mshtuko mkubwa alioupata baada ya kusikia habari ile ulimfanya apoteze fahamu kwa muda mrefu hali iliyosababisha akimbizwe hospitali usiku uleule kuokoa maisha yake. Hata baada ya kuzinduka siku iliyofuatia, shinikizo la juu la damu lilikuwa limemuelemea kiasi cha kumfanya awe taabani. Aliamini kila mtu angehisi kuwa yeye ndiye mhusika wa kifo cha Manuel Rwakatare kutokana na mazingira ya kutatanisha ya namna ambavyo kifo kile kilitokea.
Taratibu za mazishi zilipokamilika mwili wa marehemu ulipelekwa makaburini tayari kuuhifadhi kwenye nyumba ya haki mpaka siku ya hukumu. Si Geneviv wala Bi Patricia ambaye aliamini kama kweli huo ndio ulikuwa mwisho wa baba yao. Walitia huruma sana kwa jinsi walivyokuwa wakiomboleza kwa huzuni. Wanawake kadhaa walipewa jukumu la kuwasimamia na kuwafariji kwa karibu, lakini bado hakuna aliyeweza kuwatuliza. Bi Patricia alikuwa amemkumbatia mwanae Geneviv huku wakilia kwa pamoja… walihuzunisha sana.
“Jikaze mpendwa, Mungu ana makusudi yake kwetu, tujifunze kumshukuru kwa kila jambo hata liwe la kuumiza sana kama hili…tumwachie yeye kila kitu kwani yeye anafahamu atakavyotufariji na kutulinda katika kipindi kigumu kama hiki.” Yalikuwa ni maneno ya faraja kutoka kwa mmoja wa marafiki wa karibu wa Bi Patricia.
Ilibidi jitihada za ziada zitumike kuwatuliza katika kipindi kile, ambacho kwao kilionekana kuwa kigumu zaidi ya vyote. Baada ya mazishi, maelfu ya waombolezaji walirudi nyumbani kwa mzee Rwakatare ambako msiba uliendelea.
Wakati haya yote yanatokea, Geneviv alikuwa yuko jirani kabisa kufanya mtihani wake wa mwisho wa kumalizia elimu ya msingi na huo ndio ulikuwa mwezi wa mwisho wa kujiandaa. Kutokana na matatizo yaliyokuwa yamemwandama mfululizo, alishindwa kuhudhuria shule kwa siku nyingi na kumfanya ashindwe kujiandaa vizuri. Hata baada ya msiba wa baba yake kuisha, bado hakuweza kwenda kuendelea na shule kutokana na muda mwingi kuwa na majonzi, wakishinda kulia na mama yake. Hakuna aliyeweza kumfariji mwenzake, ikawa ni machozi na maombolezo yasiyoisha. Kila kitu kilipoteza maana na akawa anajiona kama mtu aliyeandikwa matatizo tu chini ya jua. Machozi yalikuwa hayamuishi...Soo many tears.
Wiki tatu tangu Mzee Rwakatare azikwe, Bi Patricia alianza kusumbuliwa na shinikizo la chini la damu, ambapo moyo wake ulikuwa ukifanya kazi chini ya kiwango na kusababisha shinikizo la damu kushuka chini ya kiwango cha kawaida. Wataalamu waliielezea hali hii kuwa inasababishwa na mtu kuelemewa na msongo ambao huzaa huzuni kali, na kama mgonjwa asipopata matibabu ya haraka nay a uhakika athari zake zilikuwa mbaya sana. Tatizo hili lilimfanya Bi Patricia ashindwe kurejea tena kazini hata baada ya likizo ya kufiwa aliyopewa kuisha. Akawa muda mwingi akishinda amelala na mwanae Geneviv wakiwa hawaelewi nini hatma yao baada ya kuondokewa na nguzo yao, mzee Rwakatare.
Pamoja na kuendelea kutibiwa palepale nyumbani kwa msaada mkubwa wa daktari Zayumba, bado hali ya Bi patricia ilikuwa ikizidi kuwa mbaya, huku shinikizo la damu likizidi kushuka siku baada ya siku. Maisha yakaanza kuwa na sura tofauti kabisa na waliyoizoea.
****
Baada ya Rais Kahungo kurejea kwenye hali yake ya kawaida, alijikuta akishindwa kuendelea kuiongoza nchi baada ya wananchi kuendelea kulalamika sana juu ya yaliyotokea huku wakimtupia lawama zote yeye kwa kushindwa kuiongoza nchi kiasi cha kuwapa nguvu wahujumu na mafisadi kuipeleka nchi shimoni.
“I think I have to resign for the benefit of my people and my countrty” (Nafikiri natakiwa kujiuzulu kwa manufaa ya watu wangu na nchi yangu)
Rais Kahungo aliamua kuweka wazi msimamo wake mbele ya mwanasheria mkuu, mkuu wa majeshi na spika wa bunge la watu wa Blaziniar.
“Lakini mheshimiwa kwa nini usiendelee kuwa Rais mpaka kipindi hiki cha kwanza kiishe ndio uchukue uamuzi mwingine? Bado watu wanakuhitaji uendelee kuwaongoza”
Alitoa ushauri mwanasheria mkuu akiungwa mkono na spika wa bunge. Msimamo wa wa James Kahungo ukawa palepale.
“Nijuavyo mimi uongozi wowote ule ni imani ya wale unaowaongoza kwako, kama ikitokea imani hiyo imepungua au imeisha kabisa, huwi tena kiongozi bora ila unabaki kuwa bora kiongozi. Kwa hili sina la kufanya zaidi ya kuwapisha wengine nao wajaribu.” Aliendelea kusisitiza Rais james Kahungo na baada ya majadiliano mazito, walimkubalia alichokitaka kwa maslahi ya taifa na wananchi wake.
Siku iliyofuatia Raisi james Kahungo akatangaza rasmi kujiuzulu wadhifa wake kama Rais baada ya wananchi wake kukosa imani naye na kwa serikali yake. Alivunja baraza lote la mawaziri aliowateua na kumkabidhi Madaraka yote mwanasheria mkuu, bwana Sebastian Manyika. Kwa mujibu wa sheria za nchi ya Blaziniar, baada ya Rais kutangaza kujiuzulu, nchi huongozwa na mwana sheria mkuu akisaidiwa na mkuu wa majeshi mpaka uchaguzi mpya utakapofanyika.
Wengi waliipokea taarifa ya kuvunjwa kwa baraza la mawaziri kwa shangwe kubwa na wakazidi kumpongeza Raisi kwa uamuzi wa kishujaa wa kulinda hadhi yake aliouchukua na zaidi kwa kuiokoa nchi yake. Baada ya kuachia Madaraka, raisi na familia yake walirudi kijijini kwao Mtae iliko asili yao ambako walianzisha mashamba na kuendelea na shughuli za kilimo cha kisasa na ufugaji. Nchi ikawa inaongozwa na mwanasheria mkuu akisaidiana kwa karibu na mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama.
******
Hali ya Bi Patricia ilizidi kuwa mbaya siku baada ya siku, huku shinikizo la damu likizidi kushuka chini. Ilibidi apelekwe hospitali ambako angepatiwa huduma kwa ukaribu zaidi. Daktari Zayumba alijitolea kumsaidia mpaka ahakikishe anapona. Geneviv akajikuta ameanza upya shughuli ya kumuuguza mama yake mpendwa. Alishindwa kuelewa kwa nini yeye tu ndio anaandamwa na mikosi mikubwa namna ile. Alikuwa akilia sana akikumbuka yote yaliyompata ndani ya muda mfupi tu.
Akawa anamuomba Mungu usiku na mchana amsaidie mama yake kupona kwani yeye ndio alikuwa msaada pekee uliosalia maishani mwake . Hakutaka kuamini kabisa kuwa maisha yake ndio yalikuwa yakianza kupoteza mwelekeo kwa kasi namna ile. Ni ndani ya miezi michache sana, mambo yote yalikuwa yamebadilika kwa kiasi ambacho kingemshangaza kila mtu. Kutoka kuwa mtoto wa afisa wa juu wa serikali mpaka kuwa yatima asiye na baba akishinda hospitali kutwa nzima kumhudumia mama yake.
Hakufahamu ataishi vipi ndani ya ulimwengu uliojaa kila aina ya mabaya, tena akiwa bado binti mdogo kabisa. Alikuwa akitokwa na machozi kila alipomtazama mama yake ambaye hali yake ilikuwa ikizidi kuwa mbaya licha ya madaktari kuendelea kumhangaikia. “Kwani tatizo la my mum ni hilo tu la shinikizo la chini la damu au kuna jingine?, mbona mnampa dawa kila siku lakini haponi au kuna kingine, niambieni nijue please…”
Alikuwa akilalama Geneviv akionyesha kupoteza matumaini ya mama yake kupona.
“usiwe na wasiwasi Geneviv, Mungu atamsaidia mama na bila shaka atapona. Endelea kumuomba mungu usiku na mchana… Atapona tu umesikia eeeh!” alikuwa akiongea Daktari Zayumba akimtia moyo Geneviv. Alijitahidi kumpa msaada mkubwa wa kisaikolojia kwani ilionyesha dhahiri akili yake imeshindwa kuhimili matatizo makubwa yaliyokuwa yakimuandama akiwa bado na umri mdogo sana. Alijikuta akimuonea huruma sana.
“Nini hatma ya mama yangu? Mbona amepewa dawa nyingi sana lakini bado haamki?”
Aliuliza Geneviv akionyesha kuanza kukata tamaa ya mama yake kupona. Daktari Zayumba akawa anazidi kumpa moyo kuwa mama yake atapona tu, hata kama atachelewa. Pamoja na kuendelea kupewa kila msaada, Bi Patricia alishindwa kuzinduka na akawa ni mtu wa kulala masaa ishirini na nne. Hata kujigeuza pale kitandani alikuwa hawezi, Geneviv akabaki kuwa msaada wake wa mwisho.
Baada ya kuona hakuna nafuu inayopatikana, madaktari walishauri kuwa bora arudishwe nyumbani ili kupunguza gharama za kulala hospitali ambazo sasa zilikuwa kubwa. Geneviv hakuwa na la kufanya zaidi ya kuukubali ushauri ule. Daktari Zayumba akawasaidia usafiri wa kuwarudisha nyumbani na akaahidi kuzidi kutoa misaada kila mara.
Geneviv akawa amerudi na mama yake nyumbani, akitakiwa kufanya kila kitu ili mama yake aendelee kuishi. Ni yeye ndiye aliyetakiwa kuhakikisha mama yake anakula, anabadilishwa nguo na kufanyiwa usafi kila siku. Hakukuwa na mtu mwingine aliyeendelea kuwasaidia zaidi ya daktari Zayumba. Hata wale ndugu ambao kipindi maisha yao yakiwa mazuri walikuwa wakija kuwasalimu mara kwa mara na kujazana pale kwao, hawakuonekana tena. Ikawa ni Geneviv na mama yake, peke yao.
“Me and my mum…”
Alikuwa akiongea Geneviv kwa sauti ya kunong’ona akiwa amekaa pembeni ya kitanda cha mama yake akimtazama kwa huruma. Alionekana kupoteza kabisa matumaini ya mama yake kupona… akawa anangoja chochote kitakachotokea. Bi Patricia alikuwa amelala kimya akiwa hajui chochote kinachoendelea. Alikuwa amefumba macho na kupoteza nuru ya maisha. Kifo cha mumewe kilikuwa kimemmaliza kabisa, akawa ni kama anayengojea siku yake ifike akaungane na mumewe. Hali hii ilikuwa ikimfanya Geneviv alie usiku kucha. Hakuelewa nini hatma ya maisha yake baada ya nguzo zake zote kupotea, tena akiwa bado na umri mdogo kabisa. Alitia huruma.
Kadri siku zilivyokuwa zinasonga, ukali wa maisha ukaanza kujionesha dhahiri. Pesa ya akiba iliyokuwepo pale ndani iliisha na kusababisha aanze kushindwa kumpatia mahitaji muhimu mama yake. Mwisho chakula nacho kikaisha na kumfanya Geneviv aanze kuhaha huku na kule kuomba misaada. Hakutaka kuona mama yake anakosa mahitaji muhimu kama chakula, akawa anasumbuliwa na mawazo ya nini cha kufanya kuhakikisha mama yake anaendelea kupata huduma.
Akawa anaamka asubuhi na kuanza kuzunguka mitaani kwa kwa ndugu na majirani kuhakikisha wanapata japo chakula cha yeye na mama yake. Wote waliokuwa wakimfahamu walikuwa wakimuonea huruma sana. Siku za mwanzo wakawa wanamsaidia mahitaji madogomadogo lakini kadri siku zilivyokuwa zinasonga, misaada nayo ikapungua na maisha kuzidi kuwa makali. Ilifika mahali akawa anashindia uji siku nzima.
Alipoona mambo yanazidi kuwa magumu, ilibidi aende kwa rafiki yake wa siku nyingi waliyekuwa wakicheza pamoja siku za nyuma, Alice. Tofauti na yeye, mwenzake Alice hakusoma hata darasa la kwanza kutokana na wazazi wake kukosa kabisa uwezo wa kumsomesha. Lakini japokuwa hakusoma, Alice alikuwa akiishi maisha ya kujitegemea na alikuwa amepanga chumba ambacho alikuwa akikilipia kodi yeye mwenyewe. Alionekana kuyamudu maisha yake licha ya umri wake kuwa mdogo na haikufahamika mara moja alikuwa akifanya kazi gani.
“Nimekuja shosti, mwenzio maisha yamenishinda. Tangu baba afariki, mama anaumwa na wala haponi. Tumetumia hela zote za akiba kumtibia lakini bado hapati nafuu na saizi hata chakula tunakosa. Naomba unisaidie mawazo ya kazi ya kufanya ili niendelee kumtunza mama, mwenzio roho inaumaa…”
Aliongea Geneviv huku machozi yakimtoka. Alice alikuwa akimsikiliza kwa makini, na akajikuta akimuonea huruma. Alijua fika jinsi ugumu wa maisha unavyoumiza kwani na yeye alipitia maisha magumu sana.
“Jamani pole shosti, lakini nasikitika sana kukuambia siwezi kukusaidia kwani kazi ninayoifanya na inayoniwezesha mimi kuishi maisha mazuri kama haya wewe huiwezi. Ni kazi ya hatari sana. Hutaiweza Geneviv…” Aliongea Alice huku akimkumbatia Geneviv ambaye urafiki wao ulianza tangu wakiwa wadogo kabisa.
Geneviv alishangaa kwa nini Alice anasema vile, na akawa hajaelewa anamaanisha nini. Akaendelea kusisitiza kuwa ataweza tu kwa kuwa anashida.
“Kwani wewe umewezaje mpaka uniambie mimi siwezi? Na mimi nimekuwa mkubwa, nitaweza tu. Niambie tafadhali, nitajitahidi na nitaweza tu. Na mimi nataka niishi vizuri kama wewe. Nataka kumtunza mama yangu kwa uwezo wangu wote.”
Baada ya Geneviv kumbembeleza sana, ilibidi amwambie ukweli ila akamsihi asimwambie mtu yeyote.
Ukweli ni kwamba Alice alikuwa akifanya biashara ya kujiuza na hiyo ndiyo iliyomuwezesha kuishi maisha mazuri kama yale. Aliweza kulipa kodi, kununua vitu vya thamani kama makochi, redio kubwa, Tv na vingine vingi ambavyo vilikifanya chumba chake kionekane kama anaishi mtu mwenye uwezo mkubwa sana. Ni biashara hiyohiyo ya kujiuza ndiyo iliyomfanya amudu kufanya yote hayo.
“ Whaaat! Alice unajiuza? Siwezi…siwezi mimi bora nife maskini” Geneviv aliongea kwa sauti akiwa ameshtushwa mno kusikia rafiki yake akifanya biashara ya hatari kama ile. Kwa haraka aliinuka na kukimbia kutoka nje…huku nyuma akamuacha Alice akimkejeli
“Lakini nilikwambia hutaweza ukang’ang’ania, sasa unashangaa nini? Kama huwezi basi kaendelee kushinda na njaa na mama’ako. Utakufa maskini na uchumi umeukalia… utashaa…”
Baada ya kutoka kwa rafiki yake, Geneviv alikimbia mpaka chumbani alikolala mama yake. Akakaa pembeni ya kitanda na kuanza kumwaga machozi. Alikuwa katika wakati mgumu sana wa kuamua nini cha kufanya. Hakuna kitu alichokilaani maishani mwake kama uchangudoa. Lakini alipomtazama mama yake akiwa hoi pale kitandani, alijikuta akizidi kuchanganyikiwa zaidi. Alihitaji kupata pesa ili amsaidie mama yake, lakini hakuwa na namna ya kuzipata pesa hizo. Akawa anajiuliza mara mbilimbili juu ya alichoambiwa na rafiki yake Alice.
“Yaani mimi nikajiuze? No, No! haiwezekani. I wont dare it!” Aliongea kwa sauti na akaanza kulia tena. Hakuna aliyekisikia kilio chake… hakuna aliyeweza kumfariji. Akamuinamia mama yake pale kitandani huku akizidi kumwaga machozi. Bi Patricia alikuwa amefumba macho akiwa hajui chochote kinachoendelea. Aliendelea kulia kwa muda mrefu huku akizidi kutafakari alichoambiwa na rafiki yake Alice. Mpaka muda wa kulala unafika, alikuwa bado hajapata jibu. Mawazo yalikuwa yakishindana akilini mwake kiasi cha kumfanya aanze kuhisi kichwa kimekuwa kizito.
Akiwa amelala usiku, wazo jingine likamjia. Alifikiria sana jinsi ambavyo thamani yake ilitolewa kikatili baada ya kubakwa. Alijiuliza tena kama aliweza kubakwa na watu wengi kwa wakati mmoja, tena bila kupewa kitu, kwa nini asihalalishe kile alichoanza kufanyiwa ili amnusuru mama yake? Mawazo yalikuwa yakishindana kichwani na mwisho akafikia uamuzi wa mwisho. Aliamua kuuweka utu wake pembeni ili amnusuru mama yake. Akapania kuwa asubuhi na mapema atawahi kwa rafiki yake Alice kumwambia kuwa yuko tayari.
Asubuhi na mapema, Geneviv aliamka na kumtayarishia mama yake uji. Baada ya kumnywesha, alitoka na kueleka kwa rafiki yake Alice. Alipofika, Alice alikuwa bado amelala kutokana na kurudi usiku sana, ikabidi amuamshe na kumueleza kuwa amejifikiria usiku kucha kuhusu walichoongea jana yake, na ameamua kukubaliana naye.
“Kwa hiyo tutakuwa pamoja etii! Shaka ondoa, nitakufundisha kila kitu usijali. Cha msingi ondoa woga na utazoea sasa hivi.”
Alice alimpokea kwa furaha na kumuahidi kumfundisha kila kitu kuhusu kazi yake. Wakaandaa kifungua kinywa kwa pamoja na kuanza kula huku wakipiga stori zao za kawaida.
“Yaani Geneviv ulivyo mzuri mpaka nakuonea wivu. Usiku tukienda kazini utaona watakavyokugombania. Yani utapata hela nyingi sana mpaka mwenyewe utashangaa.”
Aliongea Alice na kumfanya Geneviv atabasamu. Hakufurahishwa na sifa zile, akilini mwake alikuwa akiwaza namna atakavyoianza kazi ya hatari usiku. Baada ya kunywa chai nzito kwa Alice, walitoka na kwenda kumuangalia mama yake Geneviv. Waliendelea kukaa pale nyumbani mpaka jioni ambapo Alice alimuelekeza Geneviv kuwa amuandalie kila kitu mgonjwa kabla hawajaondoka.
“Sasa mama atabaki na nani? Hatutachelewa kweli kurudi?” Geneviv alikuwa bado anasitasita, Alice akawa anamtoa hofu kuwa hawatachelewa.
Baada ya kuweka kila kitu sawa, Geneviv alifunga milango na madirisha akimuacha mama yake akiwa amelala na kuondoka kuelekea kwa Alice. Walipofika bila kupoteza muda walianza kujiandaa kuelekea kazini, kujiuza. Alice alikuwa mzoefu sana na kazi ya uchangudoa kwani aliianza tangu akiwa mdogo. Alikuwa akimuelekeza Geneviv kila kitu, kuanzia namna ya kujipodoa usoni, kichwani na mwilini na pia namna ya kuvaa nusu uchi. Geneviv alikuwa mgeni wa kila kitu. Alikuwa akishangaa kila kitu hali iliyomfanya Alice awe anamtania mara kwa mara kumcheka.
Ilipotimia saa tatu za usiku, walikuwa tayari wameshajiandaa kila kitu na wakawa wanatoka. Geneviv alikuwa akijishangaa kwenye kioo kilichokuwa mle ndani kwa jinsi alivyobadilika. Alikuwa akionekana mrembo kupita kawaida. Nguo alizoazimwa na Alice zilimfanya aonekane tofauti kabisa, zikimuacha sehemu kubwa ya mwili ikiwa wazi. Walipofika barabarani Alice aliita taksi na kumpa maelekezo dereva.
Tupeleke Valentino cassino tafadhali… Aliongea kwa manjonjo Alice na akafungua mlango akimuonyeshea Geneviv kwa ishara kuwa waingie ndani.
Safari ikaanza kuelekea Valentino Cassino, kilipokuwa kituo kikuu cha makahaba na machangudoa.
Ndani ya Valentino Cassino, kulikuwa kukifurika wasichana na wanawake wanaojiuza, wakubwa kwa wadogo, wamama kwa vibinti vidogo wote wakiwa wamevalia mavazi ya ajabuajabu ili kutangaza biashara.
“Full time mpaka asubuhi elfu thelethini, short time tunaelewana, hata ukiwa na buku tano poa tu!”
Dada mmoja wa makamo alikuwa akiongea biashara na kijana mmoja wakiwa wamesimama kwa upande wa nje. Geneviv aliyasikia mazungumzo yale na akabaki ameduwaa. Hakuwahi kufikiri kuwa uzinifu unaweza kuzungumziwa kibiashara namna ile, huku watu wakiwa hawana hofu kabisa. Wateja wa biashara ile walikuwa ni wanaume, vijana, wazee, wanafunzi na wahuni wa mitaani, lakini wengi wakiwa ni wale ambao tayari wana familia zao, na walikuwa wakiwafuata palepale na kuchagua mizigo kisha kuondoka na wanaempenda. Pombe aina zote zilikuwa zikiuzwa, madawa ya kulevya na kila aina ya uovu ulikuwa ukipatikana, sauti ya muziki ilikuwa kubwa sana muda wote. Palionekana kama Jehenum ndogo.
Geneviv alikuwa akitetemeka mwili mzima kwani hakuwahi hata mara moja kuingia kwenye kumbi za starehe, tena usiku kama huo. Vurugu za mle ndani zilimtia hofu akawa kama anayeota, Alice alilitambua hilo na akawa jirani kabisa kumuondoa wasiwasi. Ile wanaingia tu mlangoni, wote waliokuwa ndani waliwakodolea macho na zaidi kwa Geneviv ambaye uzuri sura yake na umbo lake ulimfanya kila mmoja kummezea mate.
Dakika chache baadae walikuwa wamezungukwa na wanaume kibao, kila mmoja akitaka kuondoka na Geneviv. Kwa kuwa Alice alikuwa mzoefu, alisimamia kisawasawa biashara na akataka anayetaka kuondoka na Geneviv atoe kwanza hela alizonazo na mwenye dau kubwa ndio atakaeondoka nae. Muda mfupi baadae mdau mwenye mihela kibao alishinda tenda kwa kutangaza dau kubwa kuliko wote, Geneviv akabebwa juu juu na wakaingia ndani ya gari moja la kifahari sana na kupotelea gizani. Kiumri yule mwanaume alikuwa sawa na baba yake, lakini kwa kuwa ndiye aliyetoa dau kubwa Geneviv akawa hana ujanja. Akaenda kugeuzwa kitoweo.
Mpaka inafika asubuhi, Geneviv alikuwa ameingiza pesa nyingi sana mpaka mwenyewe akawa anashangaa. Japokuwa kazi ile hakuipenda, alijikuta akitabasamu wakati Alice akimhesabia mauzo ya usiku.
“Ama kweli Geneviv una bahati. Yaani usiku mmoja tu umeingiza hela ambayo kwangu ningejiuza wiki nzima ndio nifikishe kama hii. Kweli kizuri hujiuza..”
Aliongea Alice na wote wakacheka na kugongesheana mikono. Bila kupoteza muda waliingia bafuni kuoga na baada ya kujiandaa Geneviv aliondoka huku akikimbia kwenda kumuangalia mama yake. Alipofika alianza kumuandalia kifungua kinywa mgonjwa, na kwa kutumia hela aliyoipata usiku, aliweza kununua na kuandaa chakula kizuri sana.
Huo ndio ukawa mwanzo wa kuzama kwenye tabia ya uchangudoa. Ikawa kila siku usiku, Alice anakuja kumchukua na wanaenda nyumbani kwake kujiandaa na baada ya hapo wanaingia mawindoni mpaka asubuhi.
Pamoja na kufanya yote hayo, Geneviv alikuwa hamsahau mama yake. Alikuwa akijitahidi kumlisha chakula kizuri na kumnunulia mashuka mazuri ya kisasa pamoja na nguo. Pale ndani kwao pakaanza kubadilika na taratibu Geneviv akaanza kuzoea kila kitu na kuona kama hakuna cha ajabu. Japokuwa nafsi yake ilikuwa ikimshtaki, hakuwa na la kufanya zaidi ya kujilazimisha kuzoea.
***
Baada ya mwezi mmoja baadae, Geneviv tayari alikuwa mzoefu na aliweza kukusanya pesa nyingi sana. Akaamua kuzitumia kumpeleka tena mama yake hospitali. Safari hii hakutaka kumrudisha tena palepale Planet health care, akaamua kumpeleka kwenye kliniki ya kisasa iliyokuwa imefunguliwa siku za karibuni, ikitoa huduma kwa wagonjwa wa moyo na matatizo ya kisaikolojia. Japokuwa matibabu katika kliniki ile yalikuwa ghali sana, Geneviv aliweza kumudu kutokana na pesa nyingi alizokuwa anazipata kwenye mchezo wao na Alice. Mama yake akaanza kupewa huduma bora huku akiangaliwa kwa ukaribu zaidi. Pesa ilikuwa ikifanya kazi yake.
Wakati hali ya mama yake ikianza kuwa nzuri, Geneviv alianza kujisikia dalili za ajabu. Alikuwa akisikia kichefuchefu na kutapika kila baada ya kula au kusikia harufu ya chakula. Tumbo lake nalo likaanza kuongezeka ukubwa taratibu.
“What the hell is this, mbona tumbo linazidi kuwa kubwa?” Geneviv alikuwa akijiuliza maswali peke yake akiwa bafuni kuoga baada ya kuona tumbo lake linazidi kuwa kubwa. Ilibidi amwambie rafiki yake Alice.
“Hiyo itakuwa ni mimba tu, lakini hilo ni tatizo dogo sana. Ntakupeleka kwa mtaalamu aiporomoshe, wala hata usiwe na wasiwasi”
Geneviv alishangaa namna ambavyo Alice alikuwa akirahisisha mambo. Alivyoelewa yeye, utoaji mimba ulikuwa ni hatari sana kwani huweza hata kusababisha kifo kwa mhusika. Pia ilikuwa ni dhambi kwa Mungu na hata vitabu vya dini zote vilipinga kabisa suala hilo.
Huo ukawa mtihani mwingine kwenye maisha ya Geneviv. Lakini alipofikiria kwa undani, aliona ni bora tu kufanya alichoshauriwa na Alice kwani hata kama angekataa, asingeweza kuzaa kwani umri wake ulikuwa bado mdogo na hata hivyo hakujua baba wa mtoto huyo ni nani kwani alishakuwa amekutana na wanaume wengi tayari, tena bila tahadhari yoyote. Akaamua kuufuata ushauri wa Alice, kutoa mimba.
***
Huwezi kuamini, baada ya Bi Patricia kufikishwa kwenye kliniki ile na kupewa tiba ya uhakika alianza kupata nafuu kwa haraka sana.Wiki moja tu baadae alishaanza kupata nguvu za kuinuka mwenyewe ingawa bado alikuwa hawezi kuongea chochote.
“Cant believe it, kweli Mungu mkubwa, yani mama leo unaweza hata kucheka…tulishakata tamaa, kweli Mungu mkubwa”
alikuwa akiongea Geneviv huku akimkumbatia mama yake kwa furaha pale kitandani.
Hali ya Bi Patricia ilishakuwa ya kuridhisha na sasa aliweza hata kuongea, ingawa bado alikuwa akiongea kwa shida. Geneviv aliendelea kumhudumia kwa kila kitu mpaka hali yake ikawa nzuri kabisa. Wale waliokuwa wamemkatia tamaa Bi Patricia kuwa lazima afe, walikuwa hawaamini kusikia kuwa amepata nafuu na karibu ataruhusiwa kurudi nyumbani. Wakawa wanaenda Hospitali kuhakikisha kama ni kweli alikuwa amepona.
“Kweli Mungu mkubwa, yaani yule mwanamke amepona, mi nilishamuhesabia kuwa tayari ni marehemu”Alisikika mama mmoja akiwahadithia wenzake baada ya kutoka hospitali. Upande wa pili Geneviv alikuwa akijiandaa kwenda kuitoa ile mimba kabla watu na hasa mama yake hajamshtukia kwani alihisi huenda akamuumiza zaidi mama yake atakapogundua kuwa ni mjamzito. Hakutaka hilo litokee, akawa anafanya maandalizi ya mwisho kabla ya kupelekwa kwa mtaalamu wa Abortion.
“Lakini mwenzio naogopa sana, nisije nikafa nikamuacha mama yangu peke yake, bwana mi siendi!”
Alikuwa akilalamika Geneviv kwa Alice.
“Sasa umeanza mambo ya ajabu, ntaacha kukusaidia mimi! Unafikiri mama yako akikuona na akigundua una mimba si ndio atakufa kabisa kwa presha? Fanya mambo kiutu uzima, acha ushamba” alikuwa akiongea Alice akionekana kughadhabishwa na woga wa Geneviv.
Baada ya Bi Patricia kupona, aliendelea kubaki hospitali kwa matibabu zaidi ili kuhakikisha tatizo lake halijirudii tena. Alimshukuru sana Mungu wake kwa kumuokoa kutoka kwenye shimo la mauti kwani alishafikia hatua ambayo hata yeye mwenyewe hakuwa na matumaini ya kupona. Alimshukuru zaidi mwanae Geneviv kwa yote aliyomfanyia kuokoa maisha yake.
Pamoja na hayo yote, Alishangazwa na mabadiliko ya mwonekano na tabia za Geneviv. Alishangaa kugundua kuwa Geneviv ameanza kutumia vipodozi vikali, ameanza kuseti nywele na anavaa mavazi ya ajabu ambayo hakujua ameyapata wapi kwani hakuwahi kumnunulia hata mara moja. Pia alikuwa akimiliki simu ya kisasa ya mkononi na zaidi urafiki wake na Alice ulionekana kushamiri na kila walikokwenda walikuwa wanaongozana.
Alitambua kuwa mwanae na Alice walikuwa marafiki tangu enzi wakiwa bado wadogo, lakini wakaja kutengana kutokana na Geneviv kuwa bize na shule. Pamoja na hayo alikuwa akizifahamu vizuri tabia za Alice na hasa ile ya uchangudoa. Akaanza kuingiwa na wasiwasi juu ya mwanae. Hakutaka kuendelea kuumiza kichwa kwa kumhoji maswali Geneviv kwani alihisi huenda akajikuta akirudi kwenye ugonjwa wake wa moyo. Akawa anangoja apone kabisa ndio akae na binti yake, lakini moyoni alishaanza kuhisi kitu.
Pamoja na hayo alikuwa akijiuliza ni nani aliyemleta kwenye Hospitali ya gharama namna ile ambayo imeokoa maisha yake. Alikuwa bado hajajua kuwa ni jitihada za mwanae kujitoa sadaka ndio zimemfanya apone. Alikuwa akimshukuru zaidi mungu kwa kumpa nguvu mpya na kumrudishia uhai. Mawazo juu ya kuondokewa na mumewe yalishaanza kupotea na akawa anawaza jinsi atakavyoanza maisha mapya na mwanae Geneviv.
*****
Geneviv na Alice walikuwa wakielekea kwenye Dispensari moja ya uchochoroni iliyokuwa ikisifika kwa kufanya kazi ya utoaji mimba. Machangudoa wote na wanafunzi wa kike waliokuwa wakipata mimba bila kutarajia pale ndio kilikuwa kituo chao cha kufanyia mauaji ya vichanga. Daktari Maguru alikuwa akipata pesa nyingi sana kwa kazi ile haramu. Japokuwa kila mtu alikuwa anafahamu kuhusu kinachofanyika pale, bado hakuna sheria zozote zilizokuwa zinachukuliwa dhidi yake.
Mabinti wengi walikuwa wakipoteza maisha kila uchao wakati wakitolewa ujauzito na wengine walikuwa wakiachwa na vilema vya maisha. Mapigo ya moyo ya Geneviv yalikuwa yakienda mbio kupita kawaida walipokuwa wakiikaribia Dispensari ile. Alice alimshika mkono na wakaingia mpaka ndani ambako walikuta foleni kubwa ya wasichana wengine nao wakiwa wanasubiri huduma. Kidogo wasiwasi ulipungua baada ya kuona kuwa hakuwa peke yake, na zaidi kulikuwa na wasichana wengi ambao kiumri walikuwa wadogo kwake.
Alibaki akijiuliza bila kupata majibu inakuwaje watoto wadogo kama wale aliokuwa anawaona mle ndani tena wengi wakiwa ni wanafunzi, walikuwa hawaogopi kufanya dhambi kama ile ambayo yeye aliiona kama mbaya zaidi na ni sawa na kuua kiumbe kisicho na hatia. Baada ya kungoja kwa muda mrefu kwenye foleni, hatimaye zamu yao ya kukutana na daktari Maguru ilifika.
Chumba cha daktari kilikuwa kikitoa harufu kali ya damu kama machinjioni. Kitanda kilikuwa kimeloa damu na hata nguo alizovaa daktari zilikuwa na damu. Kilichomtisha zaidi Geneviv ni vifaa vilivyokuwa vinatumika. Mikasi mikubwa, visu na vyuma vya ajabu-ajabu vilivyokuwa vimetapakaa damu vilimtisha mno.
“Mungu wangu… im finished! Alice mi naondoka, siwezi, siwezii”
Aliongea Geneviv kwa sauti kubwa na akawa anataka kukimbia na kutoka nje. Daktari Maguru alimuwahi na kumrudisha ndani. Alice akaanza kuwaka baada ya kuona Geneviv anataka kumwaibisha.
“Ni mara yake ya kwanza etii” daktari Maguru alimuuliza Alice huku akiwa anasafisha vifaa vyake tayari kwa kumshughulikia Geneviv. Alice aliitikia kwa ishara na wote wakacheka. Geneviv alikuwa akitetemeka kupita kiasi, hakuamini kama angeweza kutoka hai kwenye kile chumba kilichokuwa kinatisha kama machinjioni. Baada ya kumtuliza, daktari Maguru alianza kumhoji maswali machache huku akiendelea kuandaa vifaa vyake na kuvisogeza karibu na kitanda…
“Wenzio wanatoa hata zaidi ya mara nne na bado wanadunda mitaani ndio itakuwa wewe. Tulia nikufanyie mambo, mimi ndio Maguru mtaalamu mwenyewe, hakiharibiki kitu hapa.” Alikuwa akijisifia yule daktari huku akivaa gloves ndefu tayari kwa kazi. Alimtoa Alice nje na kubaki na Geneviv. Akamuamuru kuvua nguo na kubaki kama alivyozaliwa ili afanye kazi yake vizuri. Kwa kuwa alikuwa na shida, Geneviv alitii huku akijificha uso wake kwa aibu.
“Mtoto mzuri huyu sijapata kuona, lazima nimuonje kwanza kabla ya kazi… nikimuachia watanicheka sana.” Daktari Maguru alikuwa akijisemea kimoyomoyo huku udenda ukimtoka. Ikabidi atumie mbinu uchwara za kidaktari kumuweka sawa Geneviv. Alimdanganya kuwa njia yake ilikuwa ndogo hivyo ilikuwa ni lazime ailainishe kwa kumuingilia ndio aendelee na kazi. Geneviv hakuwa mbishi,
akamuacha afanye anachokitaka mradi mimba itoke. Baada ya kumfaidi bila huruma, Daktari Maguru aliendelea na kazi yake. Masaa mawili baadae alikuwa ameshamaliza kazi. Akafungua mlango na kumuita Alice aje amchukue Geneviv.
“Pole shosti huo ndio ukubwa. Ulikuwa unaogopa nini,mbona hujafa sasa!” alikuwa akiongea Alice kwa masihara hali iliyozidi kumkasirisha Geneviv. Alikuwa akisikia maumivu makali kupita kiasi. Akajikaza na kushuka kitandani, Alice akamshika mabegani na kuuzungusha mkono mwingine kiunoni, wakawa wanatoka huku Geneviv akichechemea. Walipofika nje ilibidi wakodi taksi kwani Geneviv alishindwa kabisa kutembea. Ikawapeleka mpaka kwa Alice ambako baada ya kufika tu, Alice alimchemshia maji ya moto na kuanza kumkanda. Geneviv alikuwa akilia sana kutokana na maumivu aliyokuwa akiyasikia
**********
Bi Patricia alishangaa kuona muda wa chakula cha mchana unapita bila ya Geneviv kumpelekea chakula wakati haikuwa kawaida yake. Akawa anaangaza macho huku na kule akidhani labda atamuona akija. Mpaka jioni inafika alikuwa hajafika. Muda mfupi baadae Alice alienda kumpelekea chakula akiwa peke yake. “Mwenzio yuko wapi, mbona hata mchana hakuja?” Bi Patricia alimdaka juu juu Alice na kuanza kumhoji maswali mfululizo. Ikabidi Alice adanganye…
“Geneviv anajisikia vibaya mama, kichwa na tumbo vinamuuma tangu asubuhi tulivyotoka hapa. Nimemuacha amepumzika lakini anaendelea vizuri”
Bi patricia hakutaka kuhoji zaidi, akaishia palepale ingawa alipomkazia macho Alice alisoma kitu kwenye macho yake. Muda ulipoisha akondoka na vyombo kurudi nyumbani. Bi patricia alishaingiwa na wasiwasi juu ya mwanae Geneviv, akabaki kumuachia Mungu.
Tumbo liliendelea kumuuma Geneviv bila kupata nafuu. Japokuwa alikuwa amepewa dawa za kumaliza maumivu na kusafisha tumbo, aliugulia usiku kucha akijigalagaza kitandani kwa Alice. Alikuwa akisikia maumivu makali sana ambayo yalikuwa yakiongezeka kadri muda ulivyokuwa unaenda. Mpaka kunakucha, alikuwa hajapata hata tone la usingizi. Kutokana na maumivu, alishindwa kumuandalia kifungua kinywa na kumpelekea mama yake hospitalini. Ikabidi Alice aende tena peke yake.
“Vipi mbona umekuja tena peke yako, ina maana bado Geneviv hajapata nafuu, au ni malaria? Lakini bahati nzuri na mimi nimesharuhusiwa, nisubiri tuondoke wote”
Aliongea Bi Patricia wakati akipata kifungua kinywa alicholetewa na Alice. Wasiwasi ulianza kumuingia Alice baada ya kusikia mama yake Geneviv ameruhusiwa kurudi nyumbani. Alijua lazima siri yao ingefichuka… “Sijui itakuwaje huko nyumbani akienda kumuona Geneviv, leo tumepatikana” alikuwa akijisemea Alice wakati akimsaidia mama Geneviv kufungasha vitu vyake tayari kurudi nyumbani baada ya kupona na kuruhusiwa kutoka hospitali.
Bi Patricia alikuwa tayari amekusanya vitu vyake vyote tayari kwa safari ya kurudi nyumbani baada ya kukaa Hospitali kwa muda mrefu. Alice alikuwa akimsaidia na muda mfupi baadae wakawa ndani ya gari tayari kwa kurudi nyumbani.
Alice alishindwa kuificha hofu yake kwani alikuwa akifahamu fika hali aliyomuacha nayo Geneviv. Alijua lazima tatizo lingine kubwa lingetokea baada ya Bi Patricia kufahamu mchezo mchafu walioucheza na Geneviv. Akaamua kufanya kitu ili kunusuru shari iliyokuwa jirani kutokea.
Geneviv alikuwa akiendelea kuugulia maumivu makali ya tumbo. Mara ujumbe mfupi wa simu uliingia kwenye simu yake ya mkononi aliyoinunua siku za karibuni. Ulikuwa umetoka kwa Alice na ulisomeka hivi…
… “Shosti leo tumepatikana, sijui utamweleza nini mama yako…lazima atagundua tu kuwa umefanya abortion. Hivi saizi ndio tunatoka nae hospitali, amesharuhusiwa. Anza kujiandaa kwa msala!”
Baada ya kumaliza kuusoma ujumbe ule kwenye simu yake, Geneviv alijikuta ameshtuka
Kupita kawaida. Hakutegemea kuwa mama yake angetoka Hospitali siku ile, na zaidi kilichomchanganya ilikuwa ni hali aliyokuwa nayo.
Alijua lazima mama yake angemgundua na alijua ataumia sana akiufahamu ukweli. Akajikuta amepona ghafla… alijitahidi kuinuka kitandani na kwa haraka akavaa vizuri.
Lengo lake ilikuwa ni kumkimbia mama yake ili kuepusha matatizo mengine ambayo yangetokea baada ya mama yake kuujua ukweli.
Alipokuwa tayari alitoka mpaka ndani mwao na kwa haraka akachukua kalamu na karatasi na kuandika ujumbe akimdanganya mama yake kuwa kichwa na tumbo vimemzidia hivyo ameenda hospitali. Akili yake ilikuwa ikifanya kazi kwa spidi ya ajabu. Alipomaliza kuandika uongo alitoka na akawa anajivuta kuelekea mtaa wa nyuma. Alipohakikisha amefika mbali na kwao, alimpigia simu dreva teksi aliyekuwa anakuja kuwachukua usiku na Alice, na akamwambia aende haraka kumchukua.
Muda mfupi baadae akawa ameshafika na kumfungulia Geneviv mlango. Akaingia ndani ya gari nakumuamuru dereva aondoe gari upesi.
“Mbona leo mapema aunt, si nikupeleke kiwanja kilekile cha sikuzote?” Aliuliza dereva Taksi wakati akiwasha gari na kuondoka. Alikuwa amezoea kuwachukua Alice na Geneviv na kuwapeleka kwenye biashara yao ya Uchangudoa, akajua na muda huo ndiko Geneviv alikokuwa anaenda.
Geneviv hakujibu kitu zaidi ya kuendelea kuugulia tumbo. Alipanga kwenda gesti yoyote na kupanga chumba mpaka apate nafuu ndio arudi kwa mama yake. Alijua yale maumivu ni ya muda mfupi na yangeisha kama daktari Maguru alivyokuwa ameahidi na kumpa moyo.
“Nishushe hapo kwenye hiyo gesti…aliongea Geneviv kwa sauti ya chini akionyesha namna alivyokuwa akisikia maumivu. Alimlipa dereva pesa yake na akajikongoja mpaka ndani alikochukua chumba self contained na kujifungia. Tumbo liliendelea na sasa alishindwa kuvumilia, akawa analia kimyakimya.
“Eeeh Mungu nisamehe dhambi zangu! Niponye tumbo langu nirudi nyumbani kwa mama, why me my Lord!” alikuwa akiongea Geneviv huku akilia.
*****
Bi Patricia aliongozana na Alice mpaka nyumbani, na akamsaidia kushusha mizigo na kuingia ndani. Alipoingia tu alianza kuita…
“Geneviv….Genny… where are you my dear, im back…uko wapi?” Alikuwa akiita Bi Patricia huku akizunguka huku na huko kumtafuta Geneviv, nyumba ilikuwa kimya.
Alienda mpaka chumbani kwake lakini hakumkuta. Akiwa huko alishangaa jinsi chumba cha mwanae kilivyobadilika. Alikuwa amenunua vipodozi vingi na kuvijaza mezani, pia alikuwa amenunua nguo nyingi alizozijaza kwenye begi kubwa. Mashuka na mablanketi nayo yalikuwa mapya…Bi Patricia akabaki mdomo wazi.
Alishindwa kuelewa ni nani aliyemnunulia Geneviv vitu hivyo ambavyo kwa harakaharaka aliviona kuwa na thamani kubwa. Akiwa bado anashangaa mabadiliko makubwa aliyokuwa nayo Geneviv, aliona ujumbe kitandani na kwenda kuusoma. Ulikuwa umeandikwa na Geneviv akieleza kuwa ameenda Hospitali.
Bi Patricia hakutaka kuamini kwa haraka kama ni kweli Geneviv ameenda Hospitali kama alivyoandika. Akiwa bado anaendelea kukisanifu kile chumba, aliona kiboksi kidogo chenye dawa kikiwa pembeni ya kitanda. Akakisogelea na kukichukua. Alipokitazama vizuri alijikuta akisisimkwa na mwili kupita kawaida.
Zilikuwa ni dawa ambazo alizigundua haraka kuwa ni za kusafisha kizazi na nyingine zikiwa ni vidonge vya kuzuia mimba, Alijikuta akiishiwa nguvu. Mpaka hapo alishapata picha kamili ya kilichokuwa kikiendelea.
Akatoka na kurudi sebuleni ambako alimkuta Alice akiendelea kusafisha na kupanga vyombo. Alimtazama kwa hasira akiamini yeye ndie chanzo cha Geneviv kuharibika.
“Hebu niambie ukweli, mwenzio yuko wapi?” Bi Patricia alimbana Alice na kutaka amueleze ukweli aliko Geneviv. Alice akawa anatetemeka kwa hofu. Akazidi kubanwa kwa maswali mfululizo na mwisho akajikuta akitoa siri.
“mama ukweli ni kwamba Geneviv anaumwa sana tumbo…Tusamehe ni shetani alitupitia, mimi ndio niliempeleka kutoa mamba tukiogopa kukuumiza zaidi kwa kuwa ulikuwa bado hujapona vizuri, tusamehe”
Whaaat! Geneviv ametoa ujauzito, Mungu wangu wee, ni nani aliyempa? Bora angejifungua tu ningelea mjukuu, si ameshaharibika moja kwa moja sasa, Oooh My Lord, kwanini matatizo hayaniishii mimi? Nimekosa nini kwa Mungu maskini mimi!”
Bi Patricia aliongea kwa uchungu na kuanza kulia.
“Mama usilie, utaanza kuumwa tena, Geneviv atapona tu, mbona hata mimi iliwahi kunitokea na nikapona” alikuwa akiongea Alice akimbembeleza Bi Patricia. Kauli ile ilimfanya Bi Patricia amtazame usoni Alice kwa hasira. Pamoja na kuwa yeye ndio alikuwa chanzo, alijikuta akimuonea tena huruma. Hakuna kitu ambacho kilikuwa kikimuogopesha kama kutoa ujauzito.
Akajikuta akijifikiria jinsi watoto wa siku hizi walivyoharibika. Enzi wakati yeye akikua, ilikuwa ni vigumu sana kwa watoto wadogo kama Alice kujihusisha na umalaya na kujikuta wakitoa mimba zisizohesabika. Ilikuwa ni kama laana.
Akapiga moyo konde na kuamua kuangalia njia ya kumsaidia Geneviv ingawa tayari alikuwa amechelewa. Wakaanza kumtafuta na kazi haikuwa ngumu kwani Alice alimpigia simu na kumuuliza alipo huku mama yake akisikiliza.
Geneviv alijibu huku akilia kuonyesha kuwa hali yake ndio inazidi kuwa mbaya. Kwa haraka Bi patricia akiongozwa na Alice wakatoka na kuanza kukimbia kuelekea kule walikoelekezwa na Geneviv.
Kila aliyemuona Bi Patricia akikimbia mitaani alishangaa na wengine wakawa wanahisi kuwa labda amerukwa na akili kwani ni siku hiyohiyo ndio alikuwa ametoka Hospitali. Baadae wakafika pale walipoelekezwa. Wakaingia mpaka mapokezi ambapo baada ya kuulizia waliambiwa kuwa binti huyo aliingia muda mchache uliopita ingawa alikuwa akionekana amezidiwa sana.
“Yuko chumba gani jamani, ni mwanangu…” Aliongea Bi Patricia huku akihema kwa nguvu. Nguo alizozivaa aliziona kama mzigo, akawa anahaha huku na kule kama aliyepagawa. Yule mhudumu wa mapokezi alitoka na kuwapeleka chumba alichoingia Geneviv. Walipofika karibu na mlango walisikia Geneviv akilia kwa uchungu na ghafla akanyamaza, kukawa kimya…
“Geneviv! Geneviv! Fungua mlango, ni mimi mama yako… fungua please, sikufanyi chochote mwanangu…”
Bi Patricia alikuwa akigonga mlango kwa nguvu huku akimsihi mwanae Geneviv afungue kwani alikuwa amejifungia kwa ndani. Pamoja na kugonga kwa nguvu kwa muda mrefu, bado kulikuwa kimya kabisa.
“Tuvunje mlango…inawezekana amepoteza fahamu ndani. Tumuwahi asije akapoteza maisha.”
“Ngoja nikachukue funguo ya akiba,msivunje kwanza mlango.”
Mhudumu alitoka mbio kwenda kuchukua ufunguo wa akiba. Bi Patricia alikuwa hajiwezi kwa wasiwasi. Hakujua mwanae ana hali gani mle ndani. Sekunde chache baadae mhudumu alirejea na funguo mkononi. Wakafungua mlango na wote wakaingia ndani.
“Mungu wangu weee! Mwanangu jamani…uuuuwii!” Bi Patricia alianza kupiga mayowe kwa sauti. Geneviv alikuwa amejilaza sakafuni akiwa amelalia tumbo,mwili wake ukiwa umetulia tuli. Ilionekana kama maumivu yalikuwa yamemzidia kiasi cha kumfanya apoteze fahamu.
Alipomsogelea na kusikiliza mapigo yake ya moyo, yalikuwa bado yanapiga kuonyesha alikuwa bado yuko hai. Mama usilie, cha msingi hapa tumuokoe Geneviv…
Harakati nyingine zikaanza haraka mno. Akabebwa juu juu mpaka nje ambako taksi iliitwa haraka na akapakiwa. Safari ya kumkimbiza Hospitali ikaanza mara moja. Ongeza mwendo dereva, mwili wake umeanza kuwa wabaridi… dereva akanyoosha mguu kwenye excretor na kukanyaga mafuta mpaka mwisho.
Muda mfupi baadae wakawa tayari wameshafika Hospitali. Akabebwa juu ya kitanda cha wagonjwa na kukimbizwa ndani na manesi.
“Huyu mgonjwa si ndio yule binti Geneviv aliyekuwa anamuuguza mama yake hapa, imekuwaje tena… na werwe mama si umeruhusiwa kutoka hapa Hospitali asubuhi ya leoleo, imekuwaje tena.
“jamani wasaidieni kwanza kumuokoa mtoto, maswali mengine baadae” Ilibidi wote wawili, Geneviv na mama yake waingizwe upya wodini kwani Bi Patricia naye alianza kuhisi tatizo lake linamrudia baada ya kuona hali aliyokuwa nayo Geneviv. Mama wewe usipanic kwa sababu utakosa yote sasa, daktari alikushauri ukifika nyumbani upumzishe mwili…jikaze kama mwanamke, mwanao atapona.
Ilibidi kazi ya ziada itumike kumtuliza Bi Patricia na kuokoa tatizo lake la shinikizo la chini kulipuka upya, ilibidi wamchome kwanza sindano ya usingizi huku wengine wakijitahidi kuokoa maisha ya Geneviv. “Jamani huyu binti ameharibiwa vibaya sana! It seems amefanya abortion, hebu ona…” manesi waliokuwa wakimhudumia Geneviv walikuwa wakishangaa hali waliyoiona kwa Geneviv.
“Hata akipona sijui kama ataweza kupata mtoto maishani mwake, she got the loose cervix (Mlango wake wa uzazi umefunguka na kubaki wazi) ”
“Maskini, mbona hafanani na kufanya umalaya, usoni anaonekana mpole kumbe muuaji”
“Tusimhukumu bure, hatuwezi kujua kilichofanya atoe , kwanza hayatuhusu sisi tufanye kazi yetu hayo mengine atajua mwenyewe na wazazi wake.”
Wale manesi walikuwa wakizidi kuulizana maswali wenyewe kwa wenyewe huku wakiendelea kumhudumia Geneviv. Baada ya muda mrefu, Geneviv alizinduka na kurudiwa na fahamu zake. Mama yake naye alishazinduka muda mwingi na akawa amekaa juu yaq kitanda chake akimtazama mwanae kwa huruma. Baada ya kurudiwa na fahamu, Geneviv alianza kuangaza macho huku na kule kama anayeshangaa amefikaje mahali pale. Mara akageukia upande alikokuwa mama yake. Bi Patricia alikuwa kimya akimtazama.
“Mum im sorry, ni shetani alinipitia… samahani mama! Sikukusudia kufanya hivi, basi tu imetokea…” Geneviv alianza kuloloma akimuomba msamaha mama yake. Hakujionea huruma yeye kuliko mama yake.
Bi Patricia alijibu kwa upole…”Mwombe msamaha Mungu wako kwa dhambi kubwa uliyoifanya, na wala si mimi”
“Mama ni Alice ndio alinidanganya, mi nisingeweza kabisa, kwanza nilikataa”
“Yaani hapo ulipo una utoto gani wa kudanganywa na wewe unakubali.Kila mtu atabeba mzigo wake…Alice wa kwake na wewe wa kwako, ila nina wasiwasi na afya yako baada ya kufanya dhambi kama uliyoifanya…inawezekana hata ukipona ukakosa uwezo wa kuzaa, soo sorry for you”
Geneviv alizidi kupatwa na uchungu baada ya kuambiwa kuwa kuna uwezekano wa kuja kushindwa kuzaa akiwa mkubwa, alibaki kujilaumu mno… “Ninge…” alishindwa kumalizia na akawa analia. “Hata ukilia sana mwanangu huwezi kuubadili ukweli. Tunamsikitikia mtu anayepatwa na jambo kama hilo bila kutegemea, lakini wewe ulikusudia…unastahili matokeo yake na wala hakuna wa kumlaumu” Bi Patricia alizidi kumchoma Geneviv kwa kumpa ukweli.
“But mum I did it for the sake of you (Lakini mama nilifanya haya yote kwa ajili yako)” aliongea Geneviv kwa sauti ya juu ikiambatana na kilio. Bi Patricia alishtuka kusikia kauli ile, hakuelewa Geneviv ana maana gani. Ilibidi ashuke kitandani alipokuwa amelazwa na kusogeleaa pale alipolala Geneviv. Ikumbukwe kwamba walikuwa wamelazwa vitanda viwili vilivyofuatana na Bi Patricia hakupata mshtuko mkubwa kama awali kwa hiyo hali yake ilirejea kuwa nzuri mara tu baada ya kurejewa na fahamu.
Ilibidi amsogelee jirani kabisa ili aweze kuelewa vizuri alikuwa na maana gani kwa kauli ile aliyoitoa( But mum I did it for the sake of you). “Hebu nieleze vizuri nini kilichokusibu na unamaanisha nini kusema hivi…” Ilibidi Bi Patricia awe mpole ili apate ukweli. Geneviv alifuta machozi na kukaa vizuri tayari kuanza kumueleza mama yake kila kitu. “mama kipindi kile wakati unaumwa na umezidiwa kabisa, hakuna mtu aliyekuwa ananisaidia kukuuguza. Ilifika kipindi hata chakula kikaisha nyumbani, nikawa nashindwa hata kukuandalia uji na mimi nikawa nalala bila kula au siku nyingine nakunywa uji siku nzima.
Nilipoona hali inazidi kuwa mbaya na wewe unazidi kuteseka, niliamua kuanza kuomba misaada kwa majirani na wapiti njia, lakini bado walinisaidia kidogo tu na hali iakzidi kuwa mbaya. Niliukuwa naumia sana kwa hali ulivyokuwa nayo na hasa nilipokumbuka kuwa baba tayari ametutoka. Ikabidi niende kwa rafiki yangu Alice kuomba ushauri…” Alpofika hapo, Geneviv alikatisha kusimulia na akawa analia kwa kwikwi.
Hapo kidogo Bi Patricia alianza kupata picha ya matukio yaliyoendelea wakati akiwa kwenye usingizi wa nusu kifo. Alijikuta akianza kumuonea huruma mwanae. “Nyamaza usilie, endelea kueleza…”
Geneviv akaendelea kusimulia “Nilipoenda kwa Alice alinifundisha kutafuta hela kwa kujiuza usiku, nikawa nafanya uchangudoa” … “Whaaat, yaani na wewe ukakubali kumsikiliza, si bora ungetafuta msaada sehemu nyingine, ungetafuta hata kazi ya uhausigeli mwanangu…kwa hiyo ukawa changudoa? My God…”
Geneviv aliendelea kusimulia kila kitu jinsi alivyofanya kazi hiyo na mpaka akapata pesa za kutosha kumpeleka mama yake hospitali ya kisasa mpaka akapona.Bi Patricia alijikuta akisisismka mwili mzima. Hakutegemea kuwa mwanae anaweza kujitoa sadaka namna ile kuokoa uhai wake. Alibaki ameduwaa akimkodolea macho Geneviv akiwea kama haamini kile alichokisikia. Geneviv hakuishia hapo, akaendelea kueleza mpaka alivyopata ujauzito akiwa anaendelea na kazi ya kujiuza na jinsi ambavyo Alice alimpeleka kuitoa. Hakuficha kitu, alieleza yote. Bi Patricia akawa anajihisi kama yuko ndotoni, aliona kuwa kumbe alikuwa akimlaumu Geneviv kimakosa, akaanza kujisikia vibaya kwa kuwa hakuwa amemtendea haki kumshutumu kuwa alijitakia wakati bila msaada wake asingekuwa hai mpaka muda huo.
Basi mwanangu, yaliyopita tuyasahau tumwombe Mungu atusamehe dhambi zetu zote na tumshukuru kwa kutufanya tuwe hai mpaka muda huu kwani tuliyopitia yeye ndio anajua”
Wakashikana mikono na kuanza kusali kwa pamoja. Muda mfupi baadae nesi aliingia na kumuita Bi Patricia wazungumze pembeni.
“Nasikitika sana mama kukwambia juu ya hali ya mwanao kiafya. Najua utaumia zaidi lakini sina jinsi zaidi ya kukwambia ukweli” Aliongea yule nesi wakiwa wameytoka nje ya wodi alikolazwa Geneviv. Kuna nini tena nesi, niambie tu nitajikaza. Afya yake imefanya nini, niambie tu yule ni mwanangu… niko tayari kusikia chochote, usinifiche kitu tafadhali. Bi Patricia alianza kutetemeka wakati nesi akijiandaa kumwambia alichomuitia.
Nesi alimtazama Bi Patricia alivyokuwa amechanganyikiwa wakati akitaka kuelezwa hali ya afya ya mwanae. Akagundua kuwa amehisi kitu tofauti na alichotaka kuambiwa, akajikuta akitabasamu.
“Kwani we unafikiria mwanao ana nini? Mbona umeshtuka sana wakati ni suala la kawaida? Okey, mwanao amegundulika kuwa ana…”
Nesi alishindwa kumalizia kauli yake kwa hali aliyokuwa nayo Bi Patricia. Alivyoonekana alihisi kuwa nesi anataka kumwambia kuwa Geneviv ameambukizwa ugonjwa hatari wa Ukimwi, lakini haikuwa hivyo. Alihisi vibaya na kujikuta akipata majibu tofauti akilini mwake hata kabla ya kuambiwa. Geneviv hakuwa na Ukimwi kama mama yake alivyodhani…
“Punguza hofu mama tuangalie namna ya kumsaidia mtoto. Vipimo vinaonyesha ameambukizwa ugonjwa wa Kaswende lakini ondoa hofu kwani ugonjwa huu unatibika na atapona kabisa!”
“Sio Ukimwi nesi, au unanificha?” Bi Paticia alikuwa haamini kama ni kweli mwanae amesalimika kupata gonjwa hatari la Ukimwi. Alijikuta akiinua mikono mbele ya nesi na kumshukuru Mungu kwa sauti… “Oooh! Ahsante Mungu, umetenda miujiza yako kwa kumnusuru mwanangu kutoka kwenye mdomo wa Jehanum, Amen”
Kwake tatizo la mwanae kuja kushindwa kupata mtoto tena halikumpa taabu akaamini Mungu atafanya maajabu yake tena, cha msingi mwanae yuko salama na anaendelea kuishi. Akarudi wodini huku akikimbia, akaenda kumkumbatia mwanae pale kitandani na wakaendelea kusali na kumshukuru Mungu. Geneviv alianzishiwa dozi ya Kaswende aliyoendelea nayo kwa muda wa wiki mbili. Hatimaye alipona kabisa na wakaruhusiwa kurudi nyumbani.
“Mwanangu inaonekana shetani anatunyemelea sana kutaka kutuangamiza kwa sababu matatizo ndani ya familia yetu hayaishi, likiisha hili linaanza jingine, yaani kila siku sisi ni watu wa matatizo tu! Inabidi tufanye kazi ya ziada ya kumuomba Mungu.” Bi Patricia alikuwa akiongea na mwanae Geneviv usiku kabla ya kulala. Wakaona njia bora ni kufunga kwa wiki nzima wakikesha kusali usiku na mchana.
“mama mi siwezi kufunga, sijawahi hata siku moja halafu bado mwili hauna nguvu!” Geneviv alianza kutoa visingizio kukwepa kazi ngumu ya kufunga. Bi Patricia alikuwa mkali katika hilo na ikawa ni lazima kufunga na kusali. Siku nzima walikuwa wakijifungia ndani mwao wakisali na kutubu dhambi zao mbele za Mungu wao. Waliendelea hivyo kwa muda wa siku saba mfululizo.
Baada ya siku saba kuisha, mabadiliko makubwa yalianza kutokea. Kwanza Bi Patricia alipokea barua kutoka kazini kwake ikimtaka kurudi kazini na kuendelea na kazi. “The storm is over my dear! Umeamini kuwa Mungu yupo na anasikia maombi yetu eeeh?”
Bi Patricia alikuwa akiongea na mwanae mara baada ya kuisoma ile barua ya kumtaka arudi kazini. Kesho yake akaanza kujiandaa kurudi kazini.
Matumaini mapya yalianza kurejea na lile giza lililotanda kwa muda mrefu maishani mwao likaanza kupotea na maisha kujawa na nuru mpya. Hawakuacha kumshukuru Mungu wao kwa kila kitu. Siku iliyofuata, Bi Patricia alijiandaa tayari kwa kwenda kazini baada ya siku nyingi kupita. Geneviv ilibidi abakie pale nyumbani. “Usiondoke mwanangu umesikia, ukae hapahapa maana huko mitaani kumejaa matatizo, we mwenyewe unafahamu…kosa sio kosa ila kurudia kosa,Mungu akulinde”
Bi Patricia alikuwa akimuaga mwanae wakati akitoka kuelekea kazini. Baada ya kuondoka, Geneviv alijifungia ndani na akachukua Biblia na kuanza kuisoma. Hakuwa na mazoea ya kusoma Biblia lakini kwa miujiza aliyotendewa na Mungu hadi akawa hai mpaka muda huo, alijikuta akimpenda Mungu. “Thank you my Lord…” aliongea Geneviv kwa sauti ya chini akiwa amejifungia chumbani kwake.
Muda mfupi baadae akasikia mlango wa nje ukigongwa, akanyanyuka huku ameshikilia Biblia yake mkononi na kwenda kufungua mlango… Alikuwa ni Alice.
“ Vipi shosti, naona saizi umeshapona na kuwa fit kabisa…basi leo kuna bonge la stori nataka kukupa.”
Aliongea Alice kwa manjonjo na uchangamfu kama kawaida yake, lakini Geneviv hakumuonyesha uchangamfu kama walivyozoeana. Akamkaribisha ndani wakakaa sebuleni. Alice alishtushwa na hali aliyokuwa nayo Geneviv na alipomtazama vizuri mkononi alikuwa ameshika Biblia.
“He Geneviv umeanza lini kusoma Biblia? Mbona makubwa! Unajizeesha bure shosti, achana na mambo ya kizamani,weka huo mbiblia wako pembeni nikupe stori yenyewe”
Alice aliongea na kumpokonya Geneviv Biblia na kuitupia juu ya meza. Akaanza kumhadithia Geneviv kilichomleta.
“basi leo usiku kutakuwa na bonge la tamasha pale Valentino cassino, kiwanja chetu. Unaambiwa muziki utakesha mpaka asubuhi, halafu leo ni watu wenye hela zao ndio watakaoruhusiwa kuingia…wazungu, wahindi na mapedeshee, jiandae ntakuja kukuchukua tukale bata… mwenzio nishapata mtu wa kutoka nae ameniambia atanipa dola mia moja mpaka asubuhi, wee usipime mtoto wa kike…”
Alice alikuwa akiongea maneno mengi mno mfululizo. Alikuwa anampa taarifa Geneviv kuwa usiku wa siku hiyo waende kwenye eneo lao walilokuwa wakifanyia uchangudoa kwa kuwa kuna sherehe kubwa imeandaliwa. Geneviv alimtazama kwa dharau Alice bila kujibu chochote. Akainuka na kwenda kuichukua tena Biblia yake, akafungua na kuendelea kusoma akimuacha Alice akizidi kuongea.
“Yaani mi nakupa dili la maana unajifanya uko bize sio, dharau au kitu gani. Umeshawahi kusikia wanajeshi wakiwa vitani halafu mmoja akaasi huwa wanamfanya nini? Kama umeamua kuokoka wewe ni muasi kwetu, ntakushikisha adabu.”
Alice alinyanyuka na kutoka huku akibamiza mlango kwa nguvu. Geneviv alitikisa kichwa kwa kumsikitikia, akaenda kuufunga mlango na kurudi chumbani kwake. Hakutaka kumpa tena shetani nafasi ya kumtawala, aliamua kubadilika kwa moyo wake wote.
Geneviv aliendelea kumwomba Mungu ambadili rafiki yake Alice ili siku moja na yeye aachane na tabia ya uchangudoa. Hakutishika na vitisho alivyoachiwa na Alice, zaidi akawa anamuombea mema kwa Mungu. Muda mfupi baadae alisikia mlango ukigongwa na alipotoka kufungua, alikutana na rafiki yake wa kiume waliyekuwa wakisoma darasa moja, Joackim au Kim kama waliovyozoea kumuita shuleni. Geneviv alishtuka kumuona Kim amekuja nyumbani kwao kwani hakuwahi kufika hapo kabla.
“Karibu ndani kaka Kim, vipi habari za siku nyingi” Geneviv alimkaribisha Joackim ndani kwa uchangamfu na wakaanza stori zao za shule. Joackim alikuwa amekuja kutaka kufahamu kwa nini Geneviv aliacha shule ghafla na hata mtihani wake wa mwisho hakufanya. Alikuwa hafahamu chochote kilichomtokea zaidi ya kusikia juu juu kuwa alikuwa anaumwa na alifiwa na baba yake mzazi, mzee Rwakatare.
Geneviv alijisikia aibu kidogo kwani alihisi Kim anafahamu yote yaliyomtokea na hasa lile la kubakwa na mwisho uchangudoa na alikuwa amekuja kumsanifu. Alikuwa mgumu wa kueleza kilichomfanya mpaka akaacha shule zaidi ya kueleza kwa kifupi kuwa alikuwa na matatizo makubwa likiwemo la kuondokewa na baba yake. Kim hakutaka kuzidi kumdadisi maswali mengi kwani alihisi anamkumbusha machungu aliyoanza kuyasahau. Kim akamsimulia yote yaliyotokea baada ya yeye kuacha shule mpaka walipofanya mtihani wao wa mwisho wa kuhitimu elimu ya msingi.
Alimueleza kuwa wao tayari wameshaanza kidato cha kwanza na katika darasa lao hakuna aliyefeli, wote walikuwa wamechaguliwa kuendelea na sekondari. Taarifa zile zilimuumiza sana Geneviv akajikuta akishindwa kuyazuia machozi. Kim alipoona Geneviv analia, alimsogelea jirani na akawa anambembeleza.
“bado una nafasi ya kuendelea mbele dada Geneviv, unaweza kuwaomba walimu ukarudia tena darasa la saba halafu mwakani na wewe ukaanza sekondari. Pole usilie…yote yana mwisho”
Kwa mara ya kwanza Geneviv alihisi akifarijika mno. Uwepo wa Kim pale na jinsi alivyokuwa akimbembeleza kwa upole ulimfanya ajihisi kama anaingia kwenye dunia mpya.
Wakatazamana usoni na macho yao yakagongana, Geneviv akahisi kama moyo unamwenda mbio, akaangalia pembeni kwa aibu za kike. Alijikuta akisahau matatizo yote aliyopitia na taratibu tabasamu lililopotea kwa miaka mingi usoni mwake likaanza kuchanua upya.
“Ahsante kaka Kim, Mungu akubariki kwa kunifariji…sio siri siku ya leo imekuwa tofauti sana kwangu, sina cha kukulipa kwa wema wako kwangu.”
Waliendelea na mazungumzo ya kawaida kwa muda mrefu na baadae Kim akaaga na kuondoka. Geneviv alibaki akijiuliza maswali mengi kichwani bila kupata majibu. Kim alikuwa amemfanyia ‘Surprise’ kubwa kwani tangu aanze kuandamwa na mikosi, hakuna rafiki yake hata mmoja kutoka shule aliyewahi kuja kumtembelea. Kim ndio alikuwa wa kwanza.
Kingine kilichomfanya ajiulize maswali mengi ni jinsi alivyokuwa akijihisi wakati akibembelezwa na Kim. Alikuwa akijihisi kama amehama kutoka kwenye dunia aliyoizoea na kuingia ulimwengu mpya. Alijikuta akitaabasamu peke yake. Akachukua Biblia yake na kuendelea kujisomea.
Jioni mama yake alirudi na kumkuta akiwa amejifungia chumbani. Tofauti na siku zote, leo alionekana kuwa na furaha huku sura yake ikiwa imejawa na tabasamu. Alimpokea mama yake kwa furaha, na akamhadithia juu ya ujio wa wageni wawili, Alice na Joackim.
“Huyo Alice amefuata nini tena hapa, sitaki kabisa kumuona hapa nyumbani. Akija tena umwambie sitaki kumuona akikanyaga hapa”
Alikuwa akiongea Bi Patricia kwa jazba.
“Mum lakini mi naona tutafute jinsi ya kumsaidia kwani na yeye hapendi kufanya anayoyafanya ila ni hali ya maisha ndio inamlazimisha kujiuza. Tumsaidie atabadilika”
Aliongea Geneviv kwa busara sana kiasi cha kumfanya mama yake amuunge mkono. Lakini alitoa onyo kuwa Alice asiruhusiwe kuingia ndani kama yeye hayupo na hata mazungumzo yao wawe wanayafanya na yeye akiwepo. Geneviv alimkubalia mama yake.
“Na huyo mwingine aliyekuja ni nani?” Bi Patricia alizidi kumdadisi Geneviv. Alitoa tabasamu pana kabla ya kujibu. Alimueleza kuwa ni rafiki yake wa siku nyingi waliyekuwa wakisoma pamoja na alikuwa amekuja kumtembelea kumjulia hali. Alieleza kila kitu walichozungumza naye.
“Kumbe ndio maana leo una furaha hivyo, natamani kumfahamu huyo Kim aliyekufanya ufurahi namna hiyo, ikibidi nimpe zawadi! Yaani naona amekusahaulisha machungu yako yote… huyo ndio rafiki mwema anayekukumbuka hata ukiwa na shida.”
Wote walifurahi na wakawa wanacheka wakionekana kusahau yote yaliyowapata siku za nyuma. Wakaanza kuandaa chakula cha jioni na baada ya kula, waliingia chumbani wakaanza kusali na kumshukuru Mungu kwa yote aliyowafanyia. Baada ya kusali kwa muda mrefu hatimaye walilala.
Aubuhi na mapema, walisikia mlango ukigongwa… “nani tena asubuhi yote hii?” aliongea Bi Patricia kwa sauti ya chini akimuamsha mwanae Geneviv. Wote waliamka na kwenda kufungua.
“Hee, kumbe ni wewe shemeji, karibu sana…habari za nyumbani? Baba na mama hawajambo?”
Alikuwa ni mdogo wa marehemu mzee Manuel Rwakatare, alikuwa akiitwa Magafu, waliyezaliwa tumbo moja na baba yake Geneviv. Alikuwa amefunga safari ndefu kutoka Musoma nchini Tanzania waliko wakwe wa Bi Patricia kuja kuleta ujumbe aliotumwa kutoka kijijini kwao. Baada ya kukaribishwa na kuingia ndani, Bwana Magafu Rwakatare alitoa barua aliyopewa kutoka kijijini kwao na kumkabidhi Bi Patricia.
Hakuifungua kwanza, wakawa wanaendelea na mazungumzo mengine. Katika mazungumzo yale, Bi Patricia aligundua kitu ambacho kilimfanya aishiwe nguvu. Ilivyoonekana ujumbe uliokuwa ndani ya ile barua haukuwa mzuri. Tangu kifo cha mumewe, hakuna ndugu hata mmoja aliyewahi kuja kuwajulia hali ingawa walikuwa wakifahamu fika kuwa baada ya kuondokewa na mumewe Bi Patricia na mwanae Geneviv hawakuwa na msaada mwingine.
Akainuka na kuingia chumbani kwenda kuifungua ile barua na kusoma kilichomo ndani yake. Geneviv alibaki sebuleni na baba mdogo wake wakiendelea na mazungumzo ya kawaida. Baada ya kuufungua ule ujumbe, Bi Patricia alikutana na kitu ambacho kilimmaliza nguvu kabisa.
“Mungu wangu, yaani bado hatujatulia yameanza mengine! Sijui nitafanya nini mimi…huu mtihani siuwezi, bora kufa!”
Alijikuta machozi yakianza kumtoka. Baada ya Geneviv kuona mama yake anachelewa, aliamua kumfuata kule chumbani alikomkuta amejiinamia huku akitiririkwa na machozi.
“Mum what’s wrong? Umepatwa na nini?...”
Baada kuona mama yake anachelewa, ilibidi Geneviv amfuate kulekule chumbani. Alimkuta akiwa amechanganyikiwa baada ya kuisoma ile barua na ilivyoonekana ujumbe uliokuwa ndani yake ulikuwa ni shari tupu. Geneviv alitamani kujua Kilichokuwa ndani yake.
Akauchukua na kuanza kusoma. Wazazi na ndugu wa marehemu mzee Rwakatare, baba yake Geneviv walikuwa wamekaa kikao cha ukoo na kufikia maamuzi yafuatayo:
Bi Patricia alitakiwa kurithiwa na mdogo wa marehemu mume wake, bwana magafu Rwakatare ambaye tayari alikuwa na mke na watoto wengi kijijini kwao. Pia nyumba waliyokuwa wanaishi ilitakiwa iuzwe halafu wao, Bi Patricia , mwanae Geneviv na “mumewe mpya” walitakiwa kwenda kuishi kijijini kwa mzee Rwakatare.
Ama kwa hakika lilikuwa ni jambo la ajabu. Bi Patricia alishindwa kuamini kama ni kweli bado kuna jamii katika ulimwengu wa leo zilizokuwa zimepitwa na wakati kiasi kile.
Kurithi wajane? Kujimilikisha mali za marehemu ilhali familia yake bado inateseka?
“Yaani mimi nirithiwe, tukaishi kijijini…haiwezekani! Siko tayari bora kufa kuliko mchezo kama huu.” Bi Patricia na mwanae Geneviv waliendelea kukaa chumbani wakimuacha mgeni peke yake pale sebuleni.
Kwa jinsi hali ilivyoonyesha, kama Bi Patricia angeendelea kunyamaza kimya, ni kweli ndugu zake wangetekeleza kile walichokipanga.
Kwa jinsi mila zao zilivyokuwa, baada ya baba wa familia kufa, mke alitakiwa kurithiwa na kaka au wadogo wa marehemu na mali zote alizoacha huuzwa na wanandugu kugawana. Mke na watoto hawakuwa na haki yeyote ya kurithi zaidi ya kuwa watazamaji.
“What can we do mum? We need to act very soon, I promise I will support you!”
(Tutafanya nini mama, inabidi tuchukue hatua za haraka sana, naahidi nitakuunga mkono kwa kila kitu). Baada ya kuongea hayo, Geneviv alitoka mpaka sebuleni alikomuacha baba mdogo wake. Akakaa jirani naye na kuanza kumhoji maswali.
“ mwalimu alitufundisha kuwa mila za kurithi wajane ni mbaya kwa kuwa zinaweza kuwa chanzo kikuu cha magonjwa kama Ukimwi, mbona wewe unataka kumrithi mama?”
Bwana Magafu alicharuka na kuanza kuwa mkali baada ya kuulizwa swali lile na Geneviv.
“Ndio mama yako alivyokutuma uje kusema siyo? Haya mambo hayakuhusu kwanza we bado mtoto usiingilie mambo ya kikubwa, nyamaza”.
Muda mfupi baadae Bi Patricia alitoka chumbani na kukuta shemeji yake akifoka. Hakutaka kulaza damu, akaamua kuweka wazi msimamo wake.
“Shemeji nakuheshimu sana na pia nawaheshimu ndugu zangu wote, lakini kuhusu haya mnayoyataka niseme wazi kuwa siko tayari, sihitaji msaada wa mtu kuiongoza familia, naamini ninaweza kila kitu kwa hiyo mniache na mwanangu…” kauli ile iliamsha hasira za bwana Magafu kwani aliamini angepokelewa kwa mikono miwili kama baba mpya, na wangefaidi baada ya kuuza nyumba na kuhamia kijijini.
Alishangaa ni kwa nini Bi Patricia alikuwa na ujasiri wa kumjibu vile kwani kwa mila za kwao zilivyokuwa mwanamke hakuruhusiwa kujibu kitu au kupinga maamuzi ya wana ukoo. Aliendelea kufoka na kutoa kauli za vitisho kuwa ni lazima watii maamuzi ya wana ukoo na kama wakiendelea kubisha watakiona cha mtema kuni.
Bwana Magafu aliinuka na kubeba mizigo yake kwa hasira na akawa anatoka huku akiendelea kutoa vitisho kuwa atarudi tena baada ya siku chache kufanya utekelezaji wa yale yaliyoamriwa.
Alitoka na kubamiza mlango kwa nguvu akiwaacha Geneviv na mama yake wameduwaa. Huo ulikuwa ni mtihani mwingine ambao ama kwa hakika ulikuwa mgumu kwa Bi Patricia. Walishikana mikono wakapiga magoti na kuanza kumuomba Mungu wao awaonyeshe njia sahihi.
Baada ya sala iliyodumu kwa mrefu, hatimaye Bi Patricia na mwanae Geneviv walianza kujadiliana nini cha kufanya.
Hakuna aliyekuwa na jibu la haraka la juu ya nini kifanyike kabla mambo hayajaharibika. Kila mbinu ilionekana kuwa na matatizo.
“Mi nafikiri tufunge safari na kumfuata Raisi aliyejiuzulu, bwana Kahungo…si unakumbuka kipindi kile alitusaidia sana!” Lakini yeye sio Raisi tena, we unafikiri atatusaidia nini?”
“Hata kama sio Raisi tena, yule ni mwanamapinduzi wa kweli na lazima atatusaidia hata kwa mawazo na ushauri juu ya nini cha kufanya.”
Wazo la kumfuata raisi mstaafu likaonekana ndio bora.
Hakuna aliyekuwa tayari kuona wanarudishwa kwenye matatizo kwa sababu ya tamaa ya ndugu zao. Walijizatiti vilivyo kupambana mpaka dakika ya mwisho.
Ngoja kesho nikaombe ruhusa kazini na wewe jiandae, nikirudi tu tunaanza safari.
********
Baada ya Bwana Magafu kufikisha ujumbe aliotumwa kutoka kijijini na kukataliwa na Bi Patricia na mwanae Geneviv, aliondoka akiwa na hasira kupita kawaida. Katika maisha yake hakuwahi kugomewa kitu na mwanamke hasa huko kijijini kwao.
Aliona kama amedhalilishwa kwa sababu aliamini kuwa anazo haki zote za kumrithi mke wa marehemu kaka yake kwani mila za kwao zilikuwa zimehalalisha jambo hilo.
Na zaidi alitegemea kuwa baada ya yeye kufanikisha nyumba ile kuuzwa, angepata pesa nyingi za bure na heshima yake kijijini kwao ingeongezeka. Hakutaka kurudisha jibu kijijini kuwa ameshindwa kufanya kazi aliyotumwa na wanaukoo kwani hiyo ingekuwa aibu kwake.
Alijiapiza kuwa ni lazima afanikishe alichotumwa, kuuza nyumba na kurudi na mkewe mpya Bi Patricia kijijini.
Baada ya kuondoka pale nyumbani kwa vurugu, Bwana Magafu Rwakatare alienda kupanga chumba gesti na kuanza kuandaa mipango ya namna ya kurudi upya na mashambulizi makubwa zaidi.
Hakutaka kupoteza muda…siku ileile akaanza kutafuta mteja wa kununua nyumba kupitia kwa madalali.
Mpaka jioni giza linaingia alikuwa ameshapata wateja watatu ambao wote walikuwa na nia ya kununua nyumba, na wakaelewana kuwa asubuhi na mapema wawahi ili aende kuwaonyesha mahali nyumba ilipo na wakubaliane bei.
Alijikuta akijipongeza hata kabla hajamaliza kazi kwani aliamini hiyo ndio dawa ya mwanamke mbishi anayejifanya amesoma. Hakufikiria kuwa anaweza kupata upinzani kama aliokutana nao asubuhi ile.
Bi Patricia na mwanae hawakupata hata tone la usingizi usiku ule. Walikuwa wakizidi kumuomba Mungu wao awalinde kwani wa hakika vita iliyokuwa mbele yao ilikuwa si ndogo.
Kulipokucha tu, Bi Patricia aliwahi kuondoka lengo lake likiwa ni kwenda kuomba ruhusa kazini ili aweze kushughulikia kisawasawa hatua za kuwazuia ndugu wa mumewe wasisababishe madhara kwake na kwa mwanae Geneviv. Hakuwa tayari kuona anarithiwa wala nyumba yake inauzwa.
“Mum usikawie kurudi, mi naanza kujiandaa…” Geneviv alikuwa akimsihi mama yake wakati akitoka. Muda mfupi baadae baada ya Bi Patricia kuondoka, Bwana Magafu alirudi pale nyumbani akiwa ameongozana na watu watatu na hata bila kuingia ndani, akaanza kuwaonyesha ile nyumba na wakawa wanazunguka kuithaminisha.
Alikuwa amekuja na wateja wa kununua nyumba ile, na hakutaka kumshirikisha kitu chochote Bi Patricia.
Geneviv alishtuka kusikia watu wakizunguka nyumba yao huku wakianza kuelewana bei.
“Mungu wangu, yaani baba mdogo kweli ameenda kuleta wateja, mi nilifikiri anatania! Tutakuwa wageni wa nani sisi kama kweli atauza nyumba yetu? People are no good, I hate them…”
Geneviv alijikuta akiongea peke yake wakati akiwachungulia wale wateja wakipatana bei na baba yake mdogo. Alitamani kufanya kitu kuwazuia lakini hakujua afanye nini kwa wakati ule.
Alitamani mama yake arudi nyumbani haraka ili aje ajionee mwenyewe maajabu ya walimwengu. Akajikuta akipatwa na ujasiri wa ajabu na akatoka mpaka nje na kuwafuata pale walipokuwa wamesimama wakiendelea kupatana bei.
Alipowasogelea hata bila ya kuwasalimu, alianza kuongea kwa sauti ya juu akiwaeleza kuwa hiyo nyumba sio ya yule waliyekuwa wakielewana nae bei, bali ni ya mama yake na yeye… na kwamba baba yake ndiye aliyeijenga akisaidiana na mama yake.
Hakuna aliyemjali, walimpuuza na wakaendelea na maelewano yao. Walimchukulia kama mtoto asiyeelewa anachokizumgumza.
Alipoendelea kupiga kelele, Bwana Magafu alimvuta pembeni na kumshikisha adabu kwa kumtandika vibao mfululizo vya usoni mpaka Geneviv akawa anahisi kizunguzungu. Alikimbilia ndani ambako alijifungia chumbani kwake na kuanza kulia akimtaja marehemu baba yake.
Baada ya makubaliano yao kumalizika, baba mdogo Magafu aliondoka na wale watu wakaelekea kusikojulikana.
Muda nfupi baadae Bi Patricia alirudi baada ya kuruhusiwa kazini kwake na alipofika alimkuta Geneviv amejifungia chumbani akilia huku usoni akiwa na alama za kupigwa.
“Hee! imekuwaje tena, mbona hivyo…what’s wrong with you?”
Ilibidi aeleze kila kitu kilichoendelea baada ya yeye kuondoka.
Alibaki mdomo wazi baada ya kusikia kuwa shemeji yake amerudi akiwa na wateja na tayari wameshakubalia na kupatana kuhusu nyumba ile bila ridhaa yao. Alijikuta nguvu zikimuishia.
Bila kupoteza muda wakajiandaa na kutoka kuelekea nyumbani kwa Raisi mstaafu kwenda kuomba msaada wa kisheria. Ilikuwa ni safari ndefu kwani baada ya kujiuzulu, Bwana James Kahungo aliamua kuhamia kijijini kabisa alikokuwa anaendelea na shughuli za kilimo na ufugaji pamoja na familia yake yote.
Muda mfupi baada ya kuondoka, yule mteja aliyeshinda kununua ile nyumba alienda kumkabidhi bwana Magafu kiwango kikubwa cha pesa kama walivyokubaliana.
Akaandaa barua ya notisi na kwenda kuibandika mlangoni mwa ile nyumba akiwataka wote wanaoishi ndani ya nyumba ile wawe wameondoka baada ya masaa 72 (siku tatu) ili kupisha ukarabati aliokuwa akitaka kuufanya kabla ya kuhamia.
******
Safari ilikuwa ndefu sana na iliwachukua zaidi ya masaa 6 kufika kijijini alikokuwa anaishi Raisi mstaafu. Walipofika walipokelewa na wafanyakazi wa ndani na wakakaribishwa mpaka ndani.
“Sijui kama tunaweza kuongea na mheshimiwa?” aliuliza Bi Patricia kwa sauti ya chini akimuuliza mmoja wa wafanyakazi wa ndani wa Bwana James Kahungo. Jibu walilopewa lilizidi kuwamaliza nguvu kabisa, waliambiwa kuwa Bwana Kahungo alikuwa ameenda nje ya nchi kwa mapumziko marefu na angechelewa kurudi.
“Whaaat?... Ameondoka lini na atarudi lini? We are Finished… tutafanya nini sasa mwanangu? Yote tumwachie Mungu”
Bi Patricia aliongea kwa kuhamaki kiasi cha kuwafanya wale wafanyakazi waanze kuulizana kulikoni. Wakaondoka hata bila kuaga wakiwa wamechanganyikiwa kupita kiasi. Ilivyoonekana ni kuwa juhudi zao za kupambana na ndugu wa marehemu zilikuwa zikielekea kugonga mwamba.
Walianza safari ya kurudi nyumbani kwao wakiwa hawaelewi nini hatma yao. Safari nzima hakuna aliyekuwa akimsemesha mwenzake, kila mmoja alikuwa kimya akiwaza ya kwake.
Hatimaye walirudi mpaka nyumbani kwao, na walipofika tu, walikutana na tangazo mlangoni likiwataka kuhama ndani ya masaa 72 ili kupisha ukarabati.
Bi Patricia alihisi kichwa kikimchemka kama amemwagiwa maji ya moto. Alishindwa kuelewa nini cha kufanya na akajikuta taratibu shinikizo la damu likianza kushuka na mwili kukosa nguvu. Ilibidi apitilize moja kwa moja chumbani kwenda kulala.
Geneviv akabaki amekaa mlangoni akiwa amejiinamia. Ilikuwa tayari ni jioni na jua lilikuwa likianza kuzama. Akiwa bado amejiinamia pale mlangoni, alikuja kushtuliwa na rafiki yake Joackim “kim” aliyekuwa amekuja kumtembelea.
“Vipi dada Geneviv mbona unaonekana una mawazo namna hiyo, are you okay?” Aliongea Kim na kukaa jirani na Geneviv kwenye ngazi za pale mlangoni. Geneviv alijilazimisha kufurahi lakini alishindwa kuificha huzuni iliyokuwa moyoni mwake. Kim aliligundua hilo na akawa anamdadisi kwa upole kilichomsibu.
Geneviv hakujibu kitu zaidi ya kumuonyesha lile tangazo pale mlangoni.
Kim aliinua macho na kuanza kulisoma. Hapo ndipo alipogundua kwa nini Geneviv alikuwa na hali kama ile. Alirudia kulisoma zaidi ya mara tatu kisha akawa anamtazama Geneviv kwa huruma.
“Kwani ni nani aliyeandika hivi na kwa nini amefanya hivi?” Aliuliza Kim akiwa na shauku ya kutaka kujua. Ilibidi Geneviv amueleze kila kitu kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Geneviv alijikuta akidondosha upya machozi baada ya kumaliza kumsimulia Kim.
“Shed no more tears Geneviv…everything gonna be alright! (Usilie tena Geneviv, kila kitu kitakuwa sawa)…
Kim alikuwa akimbembeleza Geneviv kwa sauti ya chini huku akimfuta machozi. Alimhakikishia kuwa yuko tayari kuwasaidia kwa kuwa baba yake ni mwanasheria na ameshawahi kushughulikia kesi kama hizo mara nyingi sana na mara zote lazima alikuwa akishinda. Geneviv alimtazama usoni Kim akiwa kama haamini alichokuwa anakisikia kutoka kwake.
Ni hapo ndipo alipokumbuka kuwa ni kweli baba yake Kim alikuwa ni mwanasheria mzoefu na alishawahi hata kuja shuleni kwao siku za nyuma kuwapa semina juu ya ukatili dhidi ya wanawake na haki zao. Alijikuta akianza kuingiwa na matumaini mapya.
“Naomba nikamuite mama uje umwambie na yeye asikie, She is depressed na ameshakata tamaa tusipomsaidia mapema kuna uwezekano mkubwa akaanza upya kuumwa. Geneviv aliinuka haraka na kwenda kumuamsha mama yake aliyekuwa amelala baada ya kupoteza matumaini na kutojua nini cha kufanya.
“Mama…mama! amka kuna habari njema, njoo usikilize” Geneviv alikuwa akimwambia huku akimtimgisha mama yake aliyekuwa tayari amepitiwa na usingizi. Bi Patricia aliamka na kwenda kusikiliza alichoitiwa. Aliinuka kwa uchovu na kutoka nje ambako alimkuta Kim akiwa amesimama mlangoni. Alimkaribisha ndani na Geneviv akamtambulisha kuwa yule ndio Kim.
“Kumbe wewe ndio Kim, karibu sana mwanangu na nakushukuru kwa kuwa msaada nuhimu kwa dada yako Geneviv”. Baada ya mazungumzo mafupi ya kujuana, Kim alianza kumweleza mama Geneviv kuwa baba yake ni mwanasheria mashuhuri na ameshawahi kushughulikia mikasa kama hiyo mara nyingi na anao uzoefu mkubwa sana.
“Lakini sina hela za kumlipa kwa sasa, atakubali kweli kutusaidia?” Bi Patricia alikuwa akiongea kwa sauti ya chini. Kim aliwahakikishia kuwa baba yake ni mtu wa watu na angekuwa tayari kuwasaidia bila shida. Bi Patricia alikuwa bado haamini kama kweli wanaweza kupata msaada wa kutetewa haki yao bila kuwa na pesa.
Baada ya mazungumzo marefu, Kim aliaga na kuondoka akiwaacha Geneviv na mama yake wakiwa na matumaini mapya. Aliwaahidi kuwa usiku huohuo angeenda kumweleza baba yake na wangekuja naye kesho yake asubuhi na mapema. Baada ya Kim kuondoka, Bi Patricia na mwanae waliendelea kujadiliana kwa muda mrefu hadi usingizi ulipoanza kuwachukua. Hawakuacha kumuomba Mungu wao kabla ya kulala kama ilivyokuwa kawaida yao.
Asubuhi na mapema kabla hata hawajaamka, walisikia mlango ukigongwa na walipotoka kufungua, walikuwa ni Kim na baba yake. Bi Patricia na Geneviv waliwakaribisha kwa uchangamfu… “Karibuni ndani wageni…” Baada ya kuingia ndani Kim alimtambulisha baba yake na akamtaka mama ake Geneviv amweleze hali halisi ya mkasa mzima. Geneviv na Kim wakaambiwa watoke nje ili kuwapisha wazungumze mambo yao kwa uhuru.
Baada ya Geneviv na Kim kutoka nje, Bi Patricia alianza kumueleza Bwana Magwaza (baba yake Kim) mkasa mzima tangu mwanzo hadi mwisho. Walizungumza kwa muda mrefu na kwa pamoja wakakubaliana nini cha kufanya. Mwanasheria Magwaza, baba yake Kim, alikuwa akisifika kwa kuwatetea wajane na watoto yatima waliokuwa wakitaka kudhulumiwa mali zao na ndugu au watu baki. Alikuwa na historia nzuri ya kusimamia haki na katika kesi zote alizokuwa akizisimamia, haki ilikuwa ikipatikana bila ubishi…na alimhakikishia Bi Patricia kuwa hakuna kitakachoharibika.
“Ondoa wasiwasi kabisa, cha msingi nipe hiyo hati ya nyumba na mimi naanza kuwashughulikia asubuhi hii hii. Mpaka jioni nitakuwa nimeshakamilisha kila kitu, nikirudi nitakuja kukueleza nini cha kufanya. Ondoa wasiwasi na uwe huru kabisa. Hapa ni kwako na hakuna atakayekutoa wala kukudhulumu haki yako.”
Geneviv na Kim walikuwa wamekaa nje wakilitazama jua la alfajiri lilivyokuwa linachomoza kutoka upande wa mashariki. Walikuwa wametulia kila mmoja akiwaza la kwake kichwani.
“But Kim, why do you act good to me like this? What special thing did I have to deserve this?” ( Lakini Kim, kwanin unanifanyia mambo mazuri namna hii? Nina nini cha ziada mpaka nistahili haya?)
Geneviv alimuuliza Kim swali ambalo hakulitegemea. Kim alimgeukia Geneviv wakawa wanatazamana usoni. Aliachia tabasamu pana kisha akaanza kumjibu kwa sauti ya chini…
“Sidhani kama kuna lolote kubwa nimekufanyia, yote ni ya kawaida, na lengo langu kubwa ni kutaka kukuona ukifurahi, I want you to shed no more tears…Geneviv! I want to see you rejoicing (sitaki kukuona ukitoa tena machozi Geneviv, napenda kukuona ukifurahi).”
Kim alijibu kwa sauti ya chini lakini iliyokuwa imebeba ujumbe mzito ndani yake…Wakatazamana tena na kila mmoja akatabasamu! Mara walisikia mlango ukifunguliwa na wazazi wao wakawa wanatoka. Bi Patricia alikuwa akimsindikiza Bwana Magwaza baada ya kufikia muafaka wa nini cha kufanya ili kuhakikisha nyumba ile haiuzwi wala Bi Patricia harithiwi na shemeji yake.
Geneviv na Kim walisimama na kuwafuata wazazi wao.
“Mbona mlikuwa mmetulia sana, mi nilijua hampo kumbe mna…”
Aliongea kwa masihara Bi Patricia na wote wakacheka kwa furaha. Ilikuwa ni asubuhi waliyoianza vizuri na hiyo iliashiria siku njema pia.
Bwana Magwaza na mwanae Kim waliaga na kuondoka huku Geneviv akizidi kuwasindikiza kwa macho akitoa tabasamu kwa Kim. Alikuwa akijiuliza bila kupata majibu ya kuridhisha kwa nini alikuwa akijisikia tofauti na kuwa na furaha sana akikaa karibu na Kim, na kwa nini Kim alijitolea kuwasaidia namna ile wakati hawakuwa na undugu wowote.
“Wewe nawe, ukishamuona Kim utachekecheka siku nzima, anakupa nini?” Bi Patricia alizidi kumtania mwanae huku akimpigapiga mabegani na wote wakawa wanacheka kwa furaha… wakaingia ndani. Matumaini ya kuishi salama yalikuwa yakizidi kuongezeka kadri muda ulivyokuwa unaongezeka. Baada ya kumaliza kujiandaa, Bi Patricia aliondoka na kuelekea kazini akimuacha Geneviv peke yake pale nyumbani.
“Ubaki salama dear, najua leo mmeonana na Kim asubuhi asubuhi utakuwa na furaha siku nzima… take care, see you!” Aliaga Bi Patricia na kumuacha Geneviv akicheka peke yake. Walau ile furaha waliyokuwa wameizoea kabla hawaajaanza kuandamwa na jinamizi la mikosi ilianza kurudi. Geneviv aliendelea kufanya shughuli ndogo ndogo za nyumbani na baada ya kumaliza, aliinga chumbani kwake na kama kawaida alichukua Biblia yake na kukaa nayo kitandani.
Majira ya kama saa saba mchana, alisikia mlango ukigongwa kwa nguvu.
“Nani tena anayegonga mlango kwa fujo hivyo?” Geneviv alikuwa akijiuliza wakati akiinuka na kwenda kufungua. Alikuwa ni baba yake mdogo. Japokuwa ilikuwa bado ni mapema, alionekana tayari amelewa chakari… bila hata kukaribishwa akaingia hadi ndani. Geneviv alikuwa mpole ghafla akitaka kuona baba yake mdogo angefanya nini. Kitu cha kwanza alichokitaka ni chakula.
“Fanya haraka nipikie chakula, njaa inaniuma!” Aliongea kwa kufoka Bwana Magafu, na bila hiyana Geneviv aliingia jikoni na kuanza kuandaa chakula. Wakati Geneviv akiendelea kuandaa chakula, Bwana Magafu alikuwa akifikiria yake. Sio kweli kwamba alikuwa na njaa kama alivyodai bali kuna kitu alichokuwa anajiandaa kukifanya.
Aliinuka huku akipepesuka kutokana na kuzidiwa na pombe na akaenda kufunga mlango wa kutokea nje kwa ndani. Alipohakikisha ameufunga kabisa, alimfuata Geneviv aliyekuwa akiendelea kumuandalia ‘baba mdogo’ wake chakula.
Alimfuata mpaka kule jikoni na akasimama mlangoni akimtazama Geneviv aliyekuwa akihangaika kusonga ugali. Hakujua kama kuna mtu anamtazama nyuma yake, akawa anaendelea kupika. Bwana Magafu aliendelea kumtazama mwanae kwa jicho la uchu na katika hali ya kustaajabisha, alianza kumshikashika Geneviv kiunoni, hali iliyomfanya ashtuke kupita kiasi na kuacha kazi aliyokuwa anaifanya.
Akiwa hana hata chembe ya aibu, alimsogelea Geneviv mwilini na kumkumbatia kwa nguvu. Geneviv alishindwa kuelewa baba yake alikuwa akitaka nini. Alifanikiwa kumtoka mikononi na akakimbilia sebuleni ambako alimuwahi na kumshika tena. “Unataka nini baba?” Geneviv alimuuliza baba mdogo wake huku akitetemeka baada ya kushindwa kuelewa alichokuwa anakitaka kutoka kwake.
“Si nimekwambia njaa inaniuma mamaa!” aliongea kilevi Bwana Magafu huku mate ya uchu yakimtoka.
“Lakini si ndio niko kukupikia… alijitetea Geneviv huku akijitoa mikononi mwa baba yake.
“Usiwe kama mtoto mdogo, we umeshakuwa mkubwa sasa, simaanishi chakula kama ulivyoelewa, ila ninamaanisha nanii…”
Bwana Magafu alishindwa kumalizia alichotaka kusema, akamsukumia Geneviv juu ya kochi na kumlalia. Wakaanza kuvutana, Geneviv akijitahidi kuchoropoka kutoka pale juu ya kochi kwa nguvu zake zote.
Bwana Magafu alizidi kumbana kisawasawa lakini Geneviv akawa anazidi kujaribu kuchomoka, mwishowe baba mdogo wake alimzidi nguvu. Akiwa bado anafurukuta, alishangaa kumuona akifungua mkanda wa suruali yake na kuishusha chini.
“Mungu wangu, yaani hata wewe baba unataka ku…”
Kabla hata hajamalizia kusema, alimziba mdomo kwa nguvu na kuanza kumvua sketi aliyokuwa ameivaa.
*******
Geneviv aliendelea kusumbuana na baba mdogo wake pale juu ya kochi kwa muda mrefu. Hakukubali kuona anabakwa tena kwa mara nyingine kirahisi namna ile. Alikuwa na historia mbaya ambayo bado ilikuwa haijafutika akilini mwake, na sasa baba yake alikuwa akitaka kumfanyia yaleyale tena. Alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote kuzuia kitendo kile kisimtokee tena… na mbaya zaidi safari hii alikuwa ni baba yake mdogo. Zile purukushani zilizokuwa zinaendelea, zilitoa nafasi kwa Geneviv kupiga kelele za kuomba msaada.
Kim alikuwa anaenda kumtembelea Geneviv kama kawaida yake. Alipofika jirani na nyumba yao, alishtuka kusikia sauti kama ya Geneviv akilia kwa nguvu kuomba msaada, akahisi kuna tatizo liliompata. Kwa haraka alikimbia mpaka mlangoni, lakini alipojaribu kusukuma mlango, ulikuwa umefungwa kwa ndani huku Geneviv akizidi kupiga kelele za kuomba msaada.
Alichanganyikiwa kusikia Geneviv akilia namna ile, akahisi kwa vyovyote kuna jambo baya linamtokea. Akili ikamjia haraka, akaona ni bora avunje mlango ili kuwahi kumuokoa Geneviv. Alirudi nyuma kwa nguvu na kujianza kutaka kuurukia mlango na kuingia nao.
Alipokaribia alisita kufanya alichotaka kufanya baada ya kusikia sauti nyingine ambayo ilimshtua. Ilikuwa ni sauti kubwa ya mwanaume aliyekuwa akiguna kutokana na maumivu. Alishindwa kuelewa ni nini hasa kilichokuwa kikiendelea mle ndani. Kelele za yule mwanaume zilizidi kuongezeka na Geneviv akawa hasikiki tena kama anaomba msaada. Akagundua lazima kuna mchezo mchafu unaoendelea ndani. Akajikuta akipandwa na mori kuliko awali. Hakuwa tayari kuona Geneviv anapatwa na jambo lolote baya.
Baada ya kuzidi kubanwa, Geneviv alikumbuka mbinu moja ambayo alishawahi kufundishwa na rafiki yake Alice. Alibana miguu yake kwa nguvu zake zote, kisha akapeleka mdomo wake shavuni kwa baba yake. Mzee akajua amemzidi nguvu na amelainika, akazidi kumsogezea shavu. Geneviv alitumia fursa hiyo ipasavyo. Alimng’ata na kuingiza meno kisawasawa shavuni kwa Magafu, akawa anazidi kuongeza nguvu ya kung’ata hali iliyomfanya Bwana Magafu ahisi maumivu makali kupita kiasi. Uvumilivu ulimshinda na akajikuta akiguna kwa sauti ya juu kutokana na maumivu. Geneviv alizidi kumshikilia shavu kwa meno yake makali na kumfanya azidi kupiga kelele.
Kim alikuwa akihangaika kuvunja mlango. Aliurukia kwa nguvu lakini haukufunguka, akarudia kuukanyaga kwa miguu yote miwili huku akitumia nguvu zake zote, lakini bado haukufunguka. Akakusanya nguvu upya na kuurukia mlango kwa nguvu zake zote. Kitasa kilivunjika na kuufanya mlango ufunguke kwa nguvu. Kim aliingia kwa kasi ndani na kuanza kufuata sauti ilikokuwa inatokea. Alikimbia mpaka sebuleni huku akitweta… alichokiona hakuamini macho yake. Alibaki kuduwaa asijue cha kufanya. Alijihisi kama yuko ndotoni, akajifikicha macho kuhakikisha kama ni kweli au anaota.
“Kim save me! Save me my dear im dying”… Geneviv aliongea kwa sauti na kuanza kulia baada ya kumuona Kim ameduwaa. Akili ilicheza kwa haraka na akaona huo ndio muda muafaka wa kumuonyesha Geneviv kuwa anamjali. Kwa haraka aliokota stuli na kuanza kumpiga nayo mgongoni Magafu kwa nguvu zake zote. Aliendelea kumpiga nayo mpaka alipohakikisha amemuachia Geneviv. Baada ya kuona amemuachia, alimkanyaga usoni kwa nguvu…akaangukia upande wa pili wa kochi akiwa taabani.
Kwa haraka Kim alimuinua Geneviv na kumkumbatia kwa nguvu. “Are you okey Genny, didn’t he harm you? Oh My God…(Uko salama Geneviv? Vipi hajakudhuru? Oooh Mungu wangu…)
Geneviv alishindwa kujibu chochote zaidi ya kuendelea kulia kwa uchungu huku akimkumbatia Kim na kukilaza kichwa chake kifuani mwake huku akizidi kumwaga machozi. Kim alimtoa nje Geneviv na kwenda kumkalisha nje kwenye hewa safi. Alishtuka kuona Geneviv akiwa na damu mdomoni…akahisi alikuwa ameumia. Geneviv alimweleza kuwa hajaumia mahali popote ila zile damu alizipata baada ya kumng’ata mbaya wake. Japokuwa alikuwa ametoka kwenye purukushani nzito, alijisikia amani sana kuokolewa na Kim.
“Kweli wewe ni mwanaume, sijaamini kwa jinsi ulivyoweza kuniokoa…kumbe unanipenda eeh! Ahsante sana Kim, sina cha kukulipa ila Mungu ndiye atakayenilipia!” Aliongea Geneviv huku akianza upya kutokwa na machozi. Kim akawa anamfuta machozi huku akizidi kumbembeleza. Alianza kumueleza kila kitu kilivyokuwa. Kim alijikuta akimuonea huruma sana, na akajiona shujaa kwa kumsaidia kutoka kwenye wakati mgumu aliokuwa nao.
Magafu alifanikiwa kusimama kutoka pale chini alipokuwa ameanguka, na kuanza kujkongoja kutoka nje. Aliona ingekuwa aibu sana endapo watu wengi zaidi wangesikia kilichomtokea. Akawa anajivuta kutoka nje, usoni akiwa na alama za meno shavuni huku damu zikiwa zinaamchuruzika. Mgongo nao ulikuwa kama unawaka moto kwa kipigo kikali alichopokea. Alikuwa akijuta kuabishwa na watoto…
Akatoka mpaka nje na kuanza kuwatolea macho Geneviv na Kim waliokuwa wamekaa pale chini wakibembelezana. Aliwatazama kwa hasira na akaapa kuwa lazima angerudi tena kuja kulipa kisasi. ”Mnajifanya wajanja siyo, ngoja niende…nikirudi mtanitambua mimi ni nani.”
Muda mfupi baada ya Magafu kuondoka, Bi Patricia alirudi kutoka kazini. Aliwakuta Geneviv na Kim wamekaa nje, akajua wako kwenye mazungumzo yao ya ujana kama kawaida yao, wakasalimiana juu juu na kupitiliza hadi ndani. Alipofika sebuleni alishangaa kuona vitu vikiwa vimevurugika ovyo ovyo. Macho yake yalitua juu ya kochi na alipolikaribia aligundua kuwa limevunjika upande.
Alipozidi kuchunguza akaona michirizi ya damu. Akajikuta mwili wote ukimsisimka.
“Whats the hell is this!” Ilibidi atoke kwenda kumuuliza Geneviv ni nini tena kilichotokea. Wakakutana mlangoni Geneviv naye akiwa anamfuata ndani huku akiwa na hamu ya kutaka kumsimulia mama yake kilichotokea. Kim alibaki nje kuwapisha wafanye mazungumzo yao kwa uhuru.
Geneviv alieleza kila kitu kilichotokea kwa mama yake. Bi Patricia alibaki ameduwaa kwa mshangao. “Hivi ni kweli au naota? Yaani hawa watu wanataka nini kutoka kwetu? Mi nafikiri wanataka roho zetu,this is too much! sasa wameuwasha moto, ama zetu, ama zao!” Aliongea kwa jazba na kuingia ndani kwenda kubadilisha nguo. Japokuwa alikuwa akimwamini Mungu, alijikuta akipandwa na hasira kuliko kawaida.
“Wanafikiri kwa sababu mimi ni mwanamke ndio kila mtu anaweza kunitendea anavyotaka, haiwezekani! Noo! Na nitahakikisha napigana mpaka dakika ya mwisho, kama matatizo nimeshayazoea, siogopi kitu tena ”
Bi Patricia alikuwa akijisemesha peke yake kwa jazba. Aliapa kupambana na kila mtu anayetaka kumharibia maisha yake na mwanae wa pekee Geneviv.
Muda mfupi baadae, Bwana Magwaza (baba yake Kim) alikuja kumpa taarifa ya hatua alizozifikia katika suala lao la kutaka kudhulumiwa haki yao. Ilikuwa ni taarifa njema ambayo kwa kiasi Fulani ilimtuliza Bi Patricia ambaye alionekana kuanza kuchanganyikiwa baada ya binti yake kuponea chupuchupu kufanyiwa kitu mbaya na shemeji yake.
Bwana Magwaza alikuja na taarifa kuwa suala lile limefikishwa mbele ya mahakama ya jamii na imeamriwa kwamba, aliyenunua nyumba na aliyemuuzia wote wanatakiwa kuwekwa chini ya ulinzi na kufikishwa mbele ya mahakama kujibu mashtaka ya unyanyasaji na udhalilishaji wa kijinsia kwani walikuwa wamekiuka sheria mpya iliyokuwa imetungwa maalum kwa ajili ya kuwatetea wajane na mayatima.
Aliwahakikishia kwamba, baada ya hayo masaa 72 ambayo waliamriwa kuwa yakiisha wawe wamehama, wasiondoke kwani polisi watakuwepo kuwapa msaada wa kuwakamata wahusika.
Taarifa ile ilileta utulivu ndani ya mawazo ya Bi Patricia na akaanza kuona njia ya kutokea kwenye tatizo lile lililokuwa likimkabili. Aliwaona Kim na baba yake kama malaika walioshushwa na Mungu kutoka mbinguni kuja kuwafuta machozi yeye na mwanae Geneviv. Alishindwa namna ya kushukuru kwa msaada ule aliokuwa amepewa na Bwana Magwaza na mwanae Kim, zaidi ya kumshukuru sana Mungu kwa kuwakutanisha.
Siku tatu (masaa 72) waliyopewa Bi Patricia na mwanae kuhama yakawa yanaelekea kuisha.
Hawakuwa na hofu tena kwani wanausalama walishawahi kufika pale nyumbani asubuhi na mapema wakiwa na Bwana Magwaza, na wakaandaa mtego kabambe wa kuwatia nguvuni Magafu na mteja wake aliyemuuzia nyumba. Ilibidi bi Patricia asiende kazini ili kutoa ushirikiano kwa wanausalama kuhakikisha haki yake haichukuliwi na watu wengine. Baada ya masaa machache baadae, Bwana Magafu na mteja wake wakawa wanakuja, wakiwa wameongozana na mabaunsa watatu kwa lengo la kuwatoa kwa nguvu Bi Patricia na mwanae.
Hao wanakuja, tena wamengezeka na mabaunsa… Wanausalama walikuwa wakijiandaa kupambana nao. Walitaka kusubiri kidogo waanze kufanya vurugu ndipo wawakamate wakiwa na ushahidi na vidhibiti vya kutosha kuwatia gerezani. Wale wanausalama wakajificha mle ndani na wakamuamuru Bi Patricia awapokee halafu awasikilize wanachotaka kukifanya. Bi Patricia akatii kama alivyoambiwa. Kwa muda huo Geneviv alikuwa amerjifungia chumbani akiwa hataki kabisa kumuona baba mdogo wake.
Wakasogea mpaka mlangoni na kuanza kubisha hodi kwa vurugu. Bi Patricia akafungua mlango na kuwasikiliza walichokuwa wanakitaka. Bila hata kuongea nae kitu, waliwaamuru wale mabaunsa kuanza kutoa vitu vyote nje, na bila kupoteza Muda wakaanza kazi yao. Wakawa wanarusha vitu nje na kuvitupia mbali. Muda mfupi baadae wale wanausalama wakaibuka kutoka mafichoni na kuwazunguka wote watano, Magafu, Mteja aliyenunua nyumba na mabaunsa watatu.
“Mko chini ya ulinzi, wote inua mikono juu…” takayekadi tunamwaga damu yake ardhini” Mkuu wa wale wanausalama alitoa amri kali huku wakiwanyooshea bunduki.
Baada ya Bwana magafu na wenzake kubanwa na polisi eneo la tukio, waliishiwa ujanja na kuamua kusalimu amri. Polisi waliwakamata na kuwatia pingu na muda mfupi baadae gari la polisi likafika na kuondoka nao kuwapeleka gereza maalumu la kijamii. Bi Patricia, Geneviv, Kim na baba yake waliendelea kupongezana kwa kazi nzuri ambayo hatimaye ilifanikiwa. Ilikuwa ni kama mpango wa Mungu kwani bila msaada wa Kim na baba yake, hakika nyumba ile ingeshauzwa. Walimshukuru sana Mungu wao kwa yote aliyowafanyia.
Furaha ikawa imerudi upya. Siku nzima ilikuwa ya furaha mno kwa kila mmoja. Bi Patricia alikaa kwa muda mrefu na Bwana Magwaza wakizidi kupongezana, huku Geneviv na Kim nao wakiendelea kufurahi kwa pamoja. Masaa yalikatika kwa haraka na hatimaye usiku uliingia. Waliaga na kuondoka wakiwaacha Geneviv na mama yake wakiendelea kufurahi.
Baada ya kula chakula cha usiku, walimshukuru Mungu kama kawaida yao na kwenda kulala. Walijadiliana pia kama kuna umuhimu wa kumuongezea mashtaka Bwana Magafu baada ya kitendo chake cha kutaka kumfanyia kitu mbaya Geneviv.
“Mum we should forgive him, let the world teach him” (mama mi nafikiri tumsamehe tu, dunia ndio itayomfunza), aliongea Geneviv kwa upole na mama yake akamuunga mkono. Wakakubaliana kumsamehe na kutomuongezea kosa lingine la kutaka kumbaka Geneviv.
Usiku wa manane wakiwa wamelala, walianza kusikia mambo ya ajabu juu ya paa la nyumba yao. Paka wengi walikuwa wakicheza juu ya bati huku wakilia milio ya ajabu, wengine kama watoto wachanga huku wengine wakicheka kama watu.
“Mama!... mamaa!… hebu sikiliza huko nje…”
Geneviv alikuwa akimnong’oneza mama yake baada ya kusikia kelele za mapaka zikizidi kuongezeka juu ya paa la nyumba yao.
Kelele zile ziliendelea kwa muda mrefu sana huku pia sauti za milio ya bundi zikaanza kusikika na kupafanya pale nyumbani kwao patishe sana hasa ukizingatia kuwa ilikuwa ni usiku wa manane. Bi Patricia na mwanae waliamka wakiwa na hofu kubwa, wakachukua Biblia zao na kuanza kusali kwa kukemea kwa nguvu zao zote. Waliendelea kusali kwa muda mrefu huku kelele za mapaka nazo zikizidi kuongezeka.
Ilifika mahali ikawa ni kama vita kati ya nguvu za Mungu na nguvu za shetani. Baada ya kudumu kwa muda mrefu, hatimaye zile kelele zilitulia kwa muda, kisha vikaanza kusikika vicheko vya watu kutoka nje ya nyumba yao. Baada ya vicheko, ikaanza kusikika sauti ya mwanaume ikitoa amri kwa ukali. Ilikuwa ikimuamuru Bi Patricia kufanya chochote kinachowezekana kuhakikisha ndugu yao Bwana Magafu anaachiwa huru siku inayofuata la sivyo angekiona cha mtema kuni. Ujumbe ulikuwa mzito na mkali na ilionyesha dhahiri wamedhamiria kweli kuwafanyia kitu kibaya.
Wote walipigwa na butwaa baada ya kugundua kuwa kumbe kelele zile za mapaka, bundi na watu kucheka juu ya paa la nyumba usiku wa manane zilikuwa ni kwa sababu ya Magafu kufungwa jela. Walijikuta wakiingiwa na hofu kubwa kwani siku za nyuma katika enzi za uhai wa Mzee Rwakatare aliwahi kuwasimulia kuwa kijijini kwao kuna wachawi magwiji na walioshindikana na wengi walikuwa ni ndugu kutoka ndani ya ukoo wao mmoja. Walikuwa hawaaamini kwa sababu hawakuwahi kushuhudia kwa macho yao kama kweli kuna kitu kinaitwa uchawi, lakini kwa miujiza ya usiku huo, walijikuta wakiamini yale waliyokuwa wakiambiwa.
Pamoja na kukumbwa na hofu ya ajabu, lakini waliendelea kuomba na kusali kwa Mungu wao ili awaepushe na dhahama ile iliyokuwa mbele yao. Waliendelea kumlilia Mungu wao kwa muda mrefu na hatimaye zile kelele zikatoweka na kukawa kimya. Hata baada ya hali kutulia waliendelea kumwomba Mungu wao mpaka alfajiri. Hakuna aliyepata hata tone la usingizi.
“Mama hivi kumbe ni kweli ndugu zake baba ni wachawi? Basi tumwambie baba yake Kim wamwachie baba mdogo wasije kutudhuru kichawi, mi nawagopa sana wachawi” Geneviv alikuwa akiongea na mama yake baada ya kupambazuka. Yaliyotokea usiku ule yalitisha mno na yaliweza kummaliza Geneviv imani yake kabisa.
“Mwanangu hatupaswi kuuogopa uchawi kwa sababu Mungu wa Israeli yu pamoja nasi. Hatupaswi kuogopa kabisa kwani tukianza kuruhusu hofu ndani ya mioyo yetu tunaukaribisha huo uchawi utuingie vizuri. Tuzidi kumwamini Mungu kwani damu ya Yesu itatulinda kama alivyotuahidi kwenye vitabu vitakatifu.”
Maneno yale hayakumwingia Geneviv kwani aligopa sana uchawi kwa yale aliyoyashuhudia usiku. Aliona ni bora kumtoa gerezani baba mdogo wao na hata ikibidi kuwaachia nyumba waliyokuwa wanaitaka kuliko kuendelea kushindana na wachawi. Baada ya mazungumzo marefu alfajiri ile, Bi Patricia alianza kujiandaa kuelekea kazini kwake kama kawaida. Alimuacha Geneviv amelala. Wakati anatoka mlangoni, alikutana na mambo ya ajabu. Pembe za mlango zilikuwa zimepakwa vitu kama dawa za kienyeji halafu pale chini palikuwa na bahasha iliyofungwa ndani ya kitambaa chekundu. Palikuwa pia na shanga nyingi zilizomwagwa chini kuizunguka ile bahasha.
Bi Patricia alijikuta akiingiwa na hofu kupita kawaida. Ni kweli kwamba alikuwa akimuamini Mungu, lakini mambo yale aliyoyashuhudia yalimtisha sana. Alitamani kurudi ndani, lakini akapiga moyo konde na kuamua kutoka nje na kuviruka vile vitu pale mlangoni. Alipotoka alianza upya kusali kwa kukemea na kwa ujasiri wa hali ya juu aliichukua ile bahasha na kuanza kuifungua. Akiwa anaendelea kuifungua, akakutana na vitu vya ajabu. Ni ujumbe mzito kama ule aliousikia usiku wa manane, tena huu ukiwa umeandikwa kwa kitu kama damu kwenye karatasi nyeupe. Unazidi kumsisitiza kuwa asipofanya kama alivyoamriwa atakiona cha mtema kuni.
Alishusha pumzi ndefu na akajikuta mwili mzima ukitetemeka. Hata nguvu za kwenda kazini zilimuishia akabaki amekaa chini akiwa amekumbwa na hofu ya ajabu. Aliendelea kuwaza na kutafakari kwa makini nini cha kufanya. Aliona njia bora ni kwenda kwa mchungaji wake kuomba msaada zaidi wa kiroho kwani alianza kuona imani yake ikimezwa na hofu ya uchawi.
Anakutana na mambo ya kishirikina yaliyotegwa mlangoni kwake, yote yakiwa yamefanywa kichawi kwa lengo la kuzidi kumtia hofu na kumshinikiza akamtoe haraka shemeji yake , Bwana Magafu gerezani. Anapatwa na hofu kuu na anajikuta akianza kuhaha kutafuta msaada. Lakini anapiga moyo konde na kuamua kumkimbilia Mungu wake amuokoe. Anapanga kwenda kuonana na mchungaji wake ili kumpa msaada wa kiroho wa jinsi ya kupambana na jaribu kali la kiroho lililokuwa linamkabili.
Anaamua kuahirisha kwenda kazini kwa siku hiyo na badala yake anafunga safari kuelekea nyumbani kwa mchungaji wake kumuelezea yaliyowatokea usiku kucha mpaka alfajiri ile. Anamuacha Geneviv akiwa bado amelala…
****
Bi Patricia alikuwa akitembea kwa haraka kuelekea nyumbani kwa mchungaji Edward Simkoko aliyekuwa akiishi ndani ya kanisa la Holly Spirit alilokuwa akiabudu. Japokuwa ilikuwa bado ni asubuhi sana, Bi Patricia alikuwa akitokwa na kijasho chembamba. Hofu ya uchawi ilikuwa ikizidi kuongezeka na kumtesa akilini kwa kadri muda ulivyokuwa unazidi kwenda na kumfanya akose kabisa amani ndani ya moyo wake. Alikuwa akiwafikiria ndugu zake jinsi walivyogeuka na kuwa kikwazo kikubwa kwake na kwa mwanae baada ya kufiwa na mumewe. Badala ya kuwa msaada kama alivyotegemea, wanageuka na kuwa sumu kali ndani ya maisha yao.
Zaidi alikuwa akimhofia mwanae Geneviv kwani endapo jambo lolote baya lingemtokea kama ndugu zake walivyokuwa wakimtishia, Geneviv angebaki bila msaada wowote kwani baada ya kifo cha baba yake, mama yake ndio alibakia kuwa mtu pekee mwenye msaada maishani mwake. Ndugu wote walikuwa wamegeuka na kuwa kama wanyama wakali wa porini, waliingiwa na tamaa ya mali na ubinadamu wakauweka pembeni.
Akiwa anakaribia kufika nyumbani kwa mchungaji, alianza kuhisi maumivu makali ya kichwa yaliyoambatana na kizunguzungu kikali. Alipga moyo konde na kuzidi kusonga mbele. Mara akaanza kusikia kama kelele za watu wengi wakicheka kwa nguvu. Aligeuka huku na huko lakini hakuona mtu yeyote.
“Oooh My God! What the hell is this?... Ooh my Lord save me!” (Mungu wangu! Balaa gain tena hili? Eeh Bwana niokoe).
Bi Patricia alikuwa akiongea peke yake huku moyoni akisali na kukemea nguvu za giza zilizokuwa zinamuandama, akatafuta sehemu ya kukaa baada ya kuzidiwa na maumivu ya kichwa na kizunguzungu. Alikaa chini ya mti na baada ya muda mfupi hali yake ilitulia na kurudi kuwa ya kawaida. Bila kupoteza muda alinyanyuka na kuendelea na safari yake.
Cha ajabu ni kwamba alipoanza tu kutembea kuelekea kule kwa mchungaji, hali yake ilianza kubadilika na kuwa kama ile ya mwanzo. Kizunguzungu kilizidi kuongezeka huku kichwa nacho kikiwa kinamgonga mithili ya mtu anayepigwa na nyundo. Zile kelele za watu kucheka zikaongezeka kuliko mwanzo na kusababisha vurugu kubwa kichwani mwake, ingawa alipogeuka tena huku na kule bado hakumuona mtu yeyote. Akagundua moja kwa moja kuwa zile ni nguvu za kichawi kutoka kwa ndugu zake. Aliamua kupiga moyo konde na kuzidi kusonga mbele huku akilitaja jina la Mungu wake.
Aliendelea kutembea mpaka alipoikaribia kabisa nyumba ya mchungaji, lakini kwa kadri alivyokuwa akizidi kuikaribia, ndivyo alivyozidi kuumia ndani kwa ndani, ikafika mahali akawa anahisi kama akili inaacha kufanya kazi. Kichwa kilikuwa kikimuuma sana na kizunguzungu kilizidi kumbana kiasi cha kushindwa kuendelea kutembea. Aliamua kukaa tena chini, cha ajabu alipokaa tu, maumivu yote yalitoweka kabisa na akawa mzima. Alibaki akijiuliza ni kitu gani kinachosababisha hali ile. Alitambua kuwa nguvu kubwa ya giza kutoka kwa ndugu wa marehemu mumewe ilikuwa ikimzuia asiende kuonana na mchungaji.
Wazo la mwisho aliloliona linafaa ilikua ni kurudi nyumbani kutafakari upya nini cha kufanya kwani hilo la kuonana na mchungaji lilionekana kushindikana kwa muda huo. Kwa jinsi hali ilivyoonesha, hakutakiwa kufanya mzaha tena kwani dalili hizo alizokumbana nazo wakati akielekea kwa mchungaji, zilitosha kumfanya aelewe kilichokuwa mbele yake kama angekaidi yale aliyoambiwa usiku.
Alinyanyuka pale chini na kugeuka kuelekea kule alikotoka bila kuingia ndani ya nyumba ya mchungaji. Aliamini kuwa ni kweli kuna uchawi na una nguvu kubwa sana kwani alivyolifuta wazo la kwenda kwa mchungaji na kuanza kurudi kwake, ile hali haikujirudia tena mpaka anafika nyumbani kwake.
Alikuwa akijiuliza maswali mengi njia nzima bila kupata majibu. Alipofika karibu na nyumbani kwake Alimuona mwanae Geneviv akiwa amekaa nje katika mkao ambao ulionyesha dhahiri kuwa lazima kuna jambo baya lililomsibu. Alichokifikiria kilikuwa ni kweli kwani alipofika karibu, alishangaa kumuona Geneviv akiwa anajikuna ovyo mwili mzima huku akiwa ameanza kutokwa na vipele vya ajabu.
“Jamani! Umepatwa na nini tena? Mbona nimekuacha ukiwa mzima kabisa!”
Geneviv hakujibu kitu zaidi ya kuendelea kujikuna huku akivua nguo na kuzitupa pembeni . Mwili mzima ulikuwa ukimuwasha mithili ya mtu aliyemwagiwa upupu. Jinsi alivyokuwa akizidi kujikuna, mwili ulikuwa ukianza kutoa vipele vidogovidogo na ngozi yake kubadilika rangi na kuwa nyekundu.
Bi Patricia alishindwa namna ya kumsaidia mwanae kwani hakuelewa amekumbwa na nini mpaka awe vile. Ni muda mfupi tu alipoondoka, alimuacha akiwa mzima wa afya, na alikuwa bado amelala. Alivyozidi kumhoji kilichomsibu alimwambia kuwa aliamka akiwa salama kabisa ila alipofungua tu mlango aliona vitu vya ajabu vikiwa vimewekwa mlangoni na baada ya kuviruka na kutoka nje, ndipo alipoanza kujisikia mwili mzima ukimuwasha.
Haikuwa kitu kingine, bali nguvu za uchawi uliotegwa usiku. Alijikuta akishindwa kujizuia kutoa machozi kwa jinsi alivyokuwa akimuonea huruma mwanae. Geneviv alikuwa akijikuna mwili mzima na vipele vilikuwa vikizidi kuongezeka na kuifanya ngozi yake ianze kutisha. Wazo jingine likaja kuwa ni lazima akaonane na baba yake Kim haraka iwezekanavyo ili kama inawezekana waende kuifuta ile kesi mahakamani asubuhi ile ile na kumuachia huru Bwana Magafu ili kuepusha shari kubwa iliyokuwa mbele yao.
Akanyanyuka na kuanz akuhaha kama mwendawazimu. Alianza kukimbia kuelekea nyumbani kwa Bwana Magwaza, baba yake Kim. Muda mfupi baadae akawa ameshafika na kuanza kugonga mlango kwa nguvu. Ulifunguliwa na Kim na alipomuuliza kama baba yake yupo, alimjibu kuwa ameondoka alfajiri na mapema kwa safari ya kikazi na angerudi kesho yake kwani safari yake ilikuwa ndefu.
Whaaat? Hakuna namba zake za simu? Please mwanangu nisaidie! Mwenzio Geneviv anaumwa ugonjwa wa ajabu, hapa nilipo nahisi kuchanganyikiwa. Kim kusikia Geneviv anaumwa na yeye alianza kuchanganyikiwa. Kwa haraka aliingia ndani na kutoka na simu yake ya mkononi. Akabonyeza namba na kuanza kumtafuta baba yake hewani. Simu ya bwana Magwaza ilikuwa haipatikani. Wakabaki kutazamana wakiwa hawajui nini cha kufanya.
Akawa anatembea taratibu kurudi kwake, akiwa amekata tamaa kabisa. Hakujua nini hatma ya mwanae Geneviv, wala nini hatma yake. Mawazo mengi yalikuwa yakipita akilini mwake kiasi cha kumfanya aanze kuongea peke yake barabarani kama mwendawazimu. Machozi yalishakauka kwani alilia sana maishani mwake, ikafika kipindi moyo wake ukawa kama umekufa ganzi.
Wazo pekee lililokuwa limebakia ilikuwa ni kwenda kumbeba Geneviv na kwenda naye kwa mchungaji wao, bila kujali ambacho kingemtokea.
“Potelea mbali, saa hizi nimeshaamua, liwalo na liwe ila lazima nifike na mwanangu kwa mchungaji, hata nikifia njiani sitajali, lakini lazima nifike.”
Alipofika nyumbani kwake alikuta hali ya Geneviv ikizidi kuwa mbaya zaidi. Vile vipele ambavyo mwanzo vilikuwa vidogo, sasa vilibadilika na kuwa vidonda vikubwa vikitoa majimaji yaliyozidi kumfanya ajikune zaidi. Yaani ndani ya muda mfupi sana kila kitu kilikuwa kimebadilika. Geneviv aliyeamka akiwa mzima kabisa, masaa manne yaliyofuata alikuwa taabani utadhani ameugua mwaka mzima.
Ama kwa hakika nguvu ya uchawi ilikuwa imefanya kazi yake. Bi Patricia alibaki kumtazama mwanae kwa huruma, bila kupoteza muda akamuinua na kumfunika kitenge kisha wakaanza upya safari ya kuelekea kwa mchungaji. Hakutaka kujali kitakachotokea njiani kwani aliona ni bora afe akiwa anahangaika kuliko kuendelea kumalizwa na woga.
Alipita njia ile ile aliyopita asubuhi. Geneviv alikuwa akilalamika njia nzima kwa maumivu aliyokuwa anayahisi.
“Jikaze mwanangu mpaka tufike kwa mchungaji, kwa Mungu hakuna linaloshindikana, jikaze mama…”
Bi Patricia alikuwa akimfariji mwanae. Alikuwa akiumia mno kwa jinsi alivyokuwa akimuona Geneviv anateseka.
Walipokaribia kufika Bi Patricia akaanza kuhisi hali kama ile iliyomtokea asubuhi ikianza upya. Aliamua kumuuliza Geneviv kuona kama na yeye anahisi vilevile. Cha ajabu Geneviv alikuwa hazisikii zile kelele ambazo mama yake alikuwa anazisikia.
“Nasikia kabisa watu wanacheka na kutuzomea huku wakiniita jina langu.”
Japokuwa Geneviv alikuwa kwenye maumivu makali, alishtushwa na alichokisikia kutoka kwa mama yake. Akahisi ameanza kuchanganyikiwa akili. Bi Patricia alizidi kukazania kuwa anasikia kelele za ajabu tena zikisikika karibu kabisa na hapo walipo.
“Mbona sikuelewi mum, kelele gani mbona mi sizisikii? Nifikishe kwa mchungaji please, nakufa mum!”
Maneno yale ya Geneviv yalimfanya Bi Patricia apige moyo konde na kuendelea kusonga mbele licha ya mauzauza aliyokuwa akiyahisi. Kwa kadri alivyokuwa akijikaza na kuzidi kuelekea kule kwa mchungaji, maneno ya ajabu yalianza kumtoka bila mwenyewe kujielewa. Sasa akawa ni kama anayeanza kuchanganyikiwa. Akaanza kupiga mayowe kwa nguvu, na Geneviv akiwa bado anashangaa kinachoendelea, akashuhudia mama yake akianza kukimbia huku na huko akizidi kupiga mayowe.
Mum! Muuum! Whats happening to you? (mama! mamaaa! Umepatwa na nini) Geneviv alizidi kumshangaa mama yake, kwani alianza kujipaka udongo usoni na kichwani huku akitoa maneno yasiyoeleweka. Kwa kifupi alikuwa amechanganyikiwa akili. Alianza kuvua nguo alizozivaa na kuzichanachana huku akicheka kwa sauti ya juu. Mara akaanza kutimua mbio kuelekea kusikojulikana.
Safari ya kwenda kwa mchungaji ikawa imeishia kwa Bi Patricia kuchanganyikiwa akili. Alitia huruma mno.
Geneviv hakutaka kuamini macho yake kama kile kilichotokea ni kweli. God where are you? (Mungu uko wapi?) Geneviv alikuwa akiongea kwa uchungu huku akijikongoja kuelekea kule mama yake alikokimbilia. Alikuwa na hali mbaya kwani vidonda vilikuwa vikizidi kuongezeka mwili mzima na kumfanya awashwe vibaya mwili mzima.
Alijikongoja mpaka kule mama yake alikoelekea. Alizidi kumfuata mpaka alipofika kwenye dampo karibu na soko kuu. Hakuamini alichokiona. Mama yake alikuwa ndani ya lundo la takataka akichakura huku na huko kama anayetafuta kitu.
“Mum, stop that! Don’t leave me alone! Come back to me mum” Geneviv alianza kupiga kelele zilizowakusanya watu. Hakuna aliyeamini kuwa kweli yule Bi Patricia wa siku zote.
“kwani amepatwa na nini? Mbona asubuhi ya leo nimekutana naye akiwa mzima kabisa na tumesalimiana vizuri?” Alikuwa akiuliza mama mmoja akionekana kushangazwa mno na hali ya Bi Patricia. Wasamaria wema wakajitosa kwenda kutaka kumkamata lakini haikuwezekana kwani alicharuka na kuanza kumpiga kila aliyemsogelea, na baadae akakimbia na kuondoka kabisa eneo lile kuelekea kusikojulikana.
Geneviv alikuwa akimfuata huku akizidi kulia na kuomba msaada wa watu kumkamata. Hatimaye alimpotea kabisa. “Nitafanya nini mimi jamani? Nitakuwa mgeni wa nani ndani ya dunia hii! Eeh Mungu kwanini uliniumba nije kuteseka namna hii hapa duniani. Geneviv alikuwa akilia peke yake wakati akizidi kutembea huku na huko kumtafuta mama yake.
Kwa kadri jua lilivyokuwa linazidi kukolea, yale madonda yaliyomtoka geneviv mwili mzima yalikuwa yakimsababishia maumivu makali kama amemwagiwa maji ya moto mwili mzima. Ilibidi atafute mahali penye kivuli, akajisogeza chini ya mti na kukaa. Hakujua hapo ni wapi kwani pilika za kumkimbilia mama yake zilimfanya afike mbali sana.
Akakaa chini ya mti na kuendelea kujiuliza ni nini kilichotokea mpaka mambo yote yakageuka ndani ya masaa machache na kumfanya aishie katika hali kama ile aliyokuwa nayo. Alijitazama mwilini, mwenyewe hakuamini kama ni yeye kweli kwani ni siku hiyohiyo alimka asubuhi akiwa mzima wa afya njema kabisa.
Masaa machache tu, ngozi yake ilibadilika na kuwa kama ameugua kwa muda mrefu. Alijikuta machozi yakimmwagika, na zaidi alipomfikiria mama yake.
Hakutaka kuamini kuwa ni kweli ameshakuwa kichaa na kumuacha peke yake.
Alikuwa akiyafikiria yote yaliyotokea kuanzia usiku uliopita ambapo walianza kushuhudia mambo ya ajabu.
Sasa aliamini kuwa ni kweli hapa duniani kuna uchawi na una nguvu kupita kawaida. Ni uchawi wa ndugu zake dio uliomfanya mama yake achanganyikiwe na kuwa kichaa, ni uchawi huohuo ndio uliomfanya awe mahututi pale chini ya mti akiwa hajui nini hatma yake.
Alishindwa kuelewa ndugu wa baba zake wana roho za namna gani mpaka wasiwe na huruma na kuamua kuwatesa namna ile. Zaidi alibaki kumwachia Mungu kwani aliamini yeye ndiye mpangaji wa yote na kamwe asingeendelea kuvumilia kuona watu wasio na hatia wakinyanyasika namna ile.
Aliwachukia mno ndugu wa baba zake, aliwachukia pia wanaume kwani aliamini yale yote yaliyokuwa yanawakuta yeye na mama yake yalisababishwa na wanaume.
Alijiapiza kuwa kamwe hatarudi nyumbani kwao kwani kama angerudi inawezekana ule uchawi uliokuwa umetegwa ungeweza kumdhuru zaidi. Aliendelea kuugulia maumivu makali akiwa hana msaada wowote. Masaa yakawa yanazidi kukatika na hatimaye jioni ikaanza kuingia. Kwa kadri masaa yalivyokuwa yanakatika ndivyo hali yake ilivyozidi kuwa mbaya.
Akawa anajifariji kwa kurudia rudia vifungu vya Biblia alivyokuwa amevikariri kichwani
Kila jambo huja kwa wakati wake…
Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa,
Wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna vilivyopandwa
A time to kill and a time to heal;
A time to tear down and a time to build up.
A time to weep and a time to laugh;
A time to mourn and a time to dance…
A time to love and a time to hate;
A time for war and a time for peace…
********
Habari zilizokuwa zinatapakaa kama moto wa nyika zilimfikia Kim kuwa mama yake Geneviv amechanganyikiwa akili na kuwa kichaa. Hakutaka kuamini kama ni kweli kwani ni asubuhi ya siku ileile alikuja pale nyumbani kwao kuja kumuulizia baba yake mzee Magwaza.
Kim alikumbuka kila kitu mpaka wakati anaaga na kuondoka. Iweje masaa machache baadae aambiwe amechanganyikiwa na kuwa kichaa? Hilo halikumuingia kabisa akilini, akaona ni bora aende nyumbani kwa kina Geneviv akahakikishe mwenyewe.
Alipofika nyumbani kwao alikuta eneo lote likiwa kimya kabisa.
Aliposogea mlangoni aliona mambo ya ajabu ambayo moja kwa moja yalimfanya aanze kuamini yale aliyokuwa akiyasikia mtaani kutwa nzima. Kwa macho yake alishuhudia vitu kama dawa za kienyeji zikiwa zimemwagwa pale mlangoni.
Alijikuta akitetemeka kwa hofu na kuanza kurudi nyuma. Alihisi hizo ndizo zilizomfanya achanganyikiwe, Swali lililokuwa kichwani mwake ni mahali aliko pamoja na mwanae Geneviv.
Alijaribu kumuita Geneviv kwa mbali lakini bado kuliendelea kuwa kimya. Akaanza kuondoka eneo lile huku akikimbia. Alipofika mbele alikutana na msichana ambaye alimsimamisha na kuanza kumuuliza maswali…
“We vipi mbona unakimbia kimbia kama chizi, umepatwa na nini?
Ilibidi Kim asimame na kuanza kumueleza aliyoyaona kule alikotoka.
“Niulize mimi nikupe full story, mi nakaa jirani kabisa na kina Geneviv na isitoshe Geneviv alikuwa rafiki yangu mpenzi ingawa kwa sasa tuna Beef”.
Kim alikuwa amekutana na Alice. Baada ya kuambiwa kuwa yeye ndio alikuwa akifahamu kila kitu kilichokuwa kinaendelea, ilibidi aanze kumdadisi kwa undani.
“Mi ukitaka nikuambie kila kitu kilichotokea niko tayari, ila lazima na wewe uwe tayari kunitimizia ninachokitaka.
Kim bila kuelewa Alice alichokuwa anamaanisha, alikubali haraka ili mradi aambiwe kilichowatokea Geneviv na mama yake. Alikuwa na shauku kubwa ya kujua. Akakubali kuongozana na Alice mpaka kwenye chumba anachoishi. Alice alikuwa akifahamu kuwa Geneviv na Kim ni marafiki na ukaribu waliokuwa nao ulimfanya ahisi wana uhusiano mwingine zaidi ya urafiki ingawa hakuwa na uhakika.
Akaona huo ndio muda muafaka wa kulipiza ksasi kwa Geneviv kama alivyomuapia baada ya kumsaliti kwenye kazi yao ya uchangudoa kipindi cha nyuma. Alipanga kufanya kitu ambacho kitamfanya asimsahau kamwe. Aliamini ni rahisi sana kulipiza kisasi kwa Kim kwa kuwa yeye Kim alikuwa hamfahamu Alice. Akajifanya mpole ili atomize azma kwa urahisi.
Kim bila kuelewa kuwa yuko chini ya mikono ya msichana hatari, Alice… alikuwa akimfuata nyuma kuelekea kwenye chumba chake kama kondoo anayepelekwa machinjioni. Akilini mwake alikuwa na hamu ya kutaka kufahamu kwa undani kilichomtokea Geneviv ili aone kama anaweza kutoa msaada wa haraka kuokoa jahazi.
Karibu ndani kakaangu, jisikie uko nyumbani na hapa ndio umefika, utafahamu kila kitu. Kabla ya kuanza kuongea naomba nikuhudumie kinywaji unachokitaka.
Alice alikuwa akimkaribisha Kim kwa uchangamfu mno. Kim alibaki kushangaa jinsi kile chumba kilivyokuwa kimejaa vitu vya thamani.
Alihisi huenda Alice anaishi na mtu mwingine mle ndani, lakini alimtoa wasiwasi kuwa yuko peke yake.
Baada ya kuendelea kumng’ang’aniza aseme kinywaji anachokitaka, Kim aliomba soda. Alice akatoka na kwenda kumletea. Aliona ho ndio muda muafaka wa kumfanyia Kim alichokitaka.
***********
Geneviv alikuwa akizidi kuomboleza pale chini ya mti alipokuwa amekaa kwa muda mrefu. Maumivu aliyokuwa akiyahisi yalimfanya ahisi kama anakaribia kufa. Japo kuwa giza lilikuwa linaanza kuingia, hakutaka kabisa kurudi nyumbani kwao, aliona ni bora alale palepale chini ya mti ili hata akifa, watu wauone mwili wake kwa urahisi.
Aliona kama Mungu amewatupa na ndio maana wanapatwa na yote yale. Japokuwa aliendelea kuvikumbuka vifungu vya Biblia ambavyo aliamini vitampa moyo, bado ukweli uliendelea kuwa uleule.
Maumivu yalikuwa yakizidi kuogezeka na vile vidonda vilivyomtoka mwili mzima sasa vilianza kutoa usaha na kusababisha nzi waanze kujaa.
Masaa yalizidi kukatika na hatimaye ikawa usiku.
Upande wa pili, Bi Patricia ambaye sasa alikuwa tayari ni kichaa alikuwa akihama kutoka jalala moja kwenda jingine, akiokota vyakula majalalani na kula bila hofu. Alikusanya takataka nyingi na kuzibeba mgongoni kama mtoto. Kila aliyekuwa akimfahamu alikuwa akitoa machozi alipomuona.
Siku moja tu ilitosha kumuhamisha moja kwa moja kutoka ulimwengu wa kawaida na kumpeleka mahali ambapo alipoteza kabisa kumbukumbu za yeye ni nani. Alikuwa akiimba na kucheza majalalani kwa lugha ambayo haikuwa ikieleweka.
Ilipofika usiku alianza kutafuta mahali pa kulala, ambapo alijilaza kwenye lundo la takataka na kujifunika matambara machafu.
**********
Baada ya Kim kunywa soda aliyoletewa na Alice alianza kuhisi kichwa kikiwa kizito na muda mfupi akaanza kuhisi usingizi mzito ukimuelemea.
“Umeweka nini kwenye hii soda, mbona nahisi kama nimelewa!”
Aliuliza Kim kwa sauti ya kilevi akijilaza kwenye kochi. Alice alikuwa akishangilia ushindi kwani lengo lake lilikuwa likikaribia kutimia.
Bila kupoteza muda alimuinua Kim na kwenda kumlaza kitandani.
Kim alikuja kushtuka baada ya kusikia jogoo akiwika. Alianza kuvuta kumbukumbu ya pale alipo. Alijishangaa kuona kuwa amelala bila nguo hata moja, kitu ambacho hakikuwa kawaida kwake. Kilichomshtua zaidi ni kwamba alikuwa amekumbatiwa na mwanamke. Hakutaka kuamini kwa haraka kama ni kweli, akahisi yuko ndotoni.Ilikuwa tayari ni alfajiri.
Alipozidi kuvuta kumbukumbu akagundua kuwa haikuwa ndoto bali ni kweli. Kumbukumbu zake zilimrudisha jioni alipokuwa akitoka nyumbani kwa kina Geneviv na kukutana na msichana alijitambulisha kuwa anaitwa Alice. Alijaribu kukumbuka kilichoendelea lakini kumbukumbu zilikuwa zikiishia alipokaribishwa soda na Alice akiwa ndani ya chumba chake.
My God! What happened to me? Alice umenifanya nini? Cant believe this
Alishtuka kwa nguvu Kim na kuinuka kutoka pale kitandani. Hakuyaamini macho yake alipogundua kuwa alikuwa amelala na Alice usiku mzima bila kujitambua.
Kwa haraka aliinuka na kuanza kutafuta nguo zake zilipo. Alice alijifanya bado yuko usingizini, akawa anamuangalia alivyochanganyikiwa kwa jicho la wizi. Moyoni mwake alikuwa akishangilia ushindi kwani alichokitaka alikuwa ameshakipata. Alijipongeza kwa mtego wake kumnasa Kim kirahisi namna ile.
Kim alivaa nguo kwa haraka na bila kuaga akafungua mlango huku akiendelea kumlaani Alice kwa kitendo kichafu alichomfanyia. Tayari ilikuwa ni saa kumi na moja alfajiri.
Alitoka na kuanza kukimbia akiwa hajui anakoelekea. Kitendo alichofanyiwa na Alice kilimfanya awe kama mwendawazimu. Alikimbia kwa umbali mrefu mpaka akaanza kuhisi kuchoka. Alitafuta mahali akakaa na kuanza kutafakari kwa makini juu ya kilichomtokea. Alikuwa akimlaani vikali Alice na alimuona kama shetani aliyejivika ngozi ya malaika.
Baada ya kutafakari sana, aliamua kuchukulia kawaida na kusahau yote yaliyotokea. Wazo pekee lililokuwa kichwani mwake ilikuwa ni kumtafuta Geneviv kwa udi na uvumba. Aliinuka kutoka pale chini alipokuwa amekaa na kuanza kutembea taratibu kukatiza mitaani.
Baada ya kwenda umbali mfupi, aliona kitu ambacho kilimfanya ashtuke. Alikuwa ni mtu amelala chini ya mti. Kwa kuwa bado ilikuwa ni Alfajiri, ilionyesha moja kwa moja kuwa amelala pale usiku kucha. Ilibidi aanze kusogea taratibu kutaka kuona ni nani aliyeweza kulala nje usiku kucha ilhali mitaani kulikuwa kumejaa vibaka na watu wa wabaya.
Kwa kadri alivyokuwa anasogea mapigo ya moyo yalianza kumwenda kasi. Hii ni kwa sababu yule mtu alikuwa amejifunika kitenge ambacho Kim alikhisi kama anakifahamu ingawa hakukumbuka haraka kuwa alimuona nani akiwa amekivaa.Alisogea mpaka jirani kabisa. Aliinama chini na kumfunua yule mtu usoni…
“Geneviv! Geneviv! Oooh my Lord, what happened to you? Mimi ni Kim! Nimekutafuta sana my dear, hebu nieleze, umetokewa na nini” Hakuamini macho yake. Alikuwa ni Geneviv akiwa amelala chini ya mti. Alishangaa kwa jinsi alivyokuwa amebadilika mwili mzima, uso ulikuwa umejaa vidonda na alipomchunguza vizuri, alikuwa na madonda mwili mzima. Hakuyaamini macho yake.
Alimuinamia kwa upole huku machozi yakimwagika. Alijikuta akiumia mno kwa hali aliyomkuta nayo Geneviv. Hakuelewa amepatwa na nini mpaka awe katika hali kama ile. Geneviv alikuwa kimya akimsikiliza Kim. Alijikuta na yeye akimwaga machozi kwani hakutegemea kama anaweza kukutana naye tena.
“Just leave me Kim, leave me alone please! Im ready to die”
(We niache tu Kim, Niache peke yangu! Niko tayari kufa.
Geneviv anarudia tena kauli yake, safari hii kwa sauti ya juu zaidi huku akianza kumwaga machozi kwa uchungu…
“Shed no more tears Geneviv, kila kitu kina mwanzo na mwisho, haya yote yatakwisha! Amini Mungu ana makusudi na wewe!”
Kim alikuwa akiongea kwa majonzi huku naye akibubujikwa na machozi. Hali aliyokuwa naye Geneviv ilimliza sana. Aliendelea kumbembeleza kwa maneno ya kumtia nguvu na taratibu Geneviv akaanza kumuelewa.
Geneviv alikuwa akishangaa kitu kimoja, kwa hali aliyokuwa nayo, yeye mwenyewe alijiona anatisha na kutia kinyaa, lakini alishangaa kumuona Kim akiwa hajali kabisa, alikuwa amemuinamia karibu kabisa bila ya kuogopa wala kuona kinyaa. Ilibidi amwambie Kilichokuwa moyoni mwake, aliamini lazima angekufa, lakini kabla hajafa alitaka Kim afahamu kuwa amekuwa mtu wa kipekee mno katika maisha yake.
“Before I die…let me tell you that I have never meet with a boy of your kind… I have nothing to pay you back…May God grant you long living…let me go!”
(Kabla sijafa… naomba nikwambie kuwa sijawahi kukutana na mvulana mwenye roho kama yako, sina cha kukulipa… Mungu akupe maisha marefu…acha mi nitangulie).
Maneno yale machache yalimchoma sana Kim mtimani na akajikuta akizidi kulia kama mtoto mdogo.
“No Geneviv! Don’t Go! Bado nakuhitaji Geneviv, you are everything to me! Usiende…”
Aliongea Kim huku akilia na kumkumbatia Geneviv kwa nguvu. Hakujali kama mwili wake ulikuwa na vidonda vinavyotoa usaha. Ilikuwa bado ni alfajiri sana, na taratibu jua likawa linachomoza.
“Angalia jua linavyochomoza Geneviv, hivi ikitokea kuwa kabla halijachomoza likazama na kurudi lilikotoka, unafikiri dunia itakuwaje?” Kim alimpiga swali la kimitego huku akifuta machozi. Geneviv alilitazama lile jua kwa makini na kutafakari kile kilichozungumzwa na Kim.
“Unamaana gani!”
Alijikuta akipata nguvu za kuinuka, akakaa kwa shauku akiugemia mti huku akizidi kutafakari Kim alikuwa na maana gani.
“Namaanisha kuwa wewe ni kama jua linaloanza kuchomoza moyoni mwangu na maishani mwangu, lakini ghafla unataka kuondoka na kurudi ulikotoka, unafikiri mi ntabaki na hali gani hapa duniani endapo jua langu litazimika asubuhi?”
Japokuwa alikuwa kwenye maumivu makali, alijikuta akiachia tabasasmu hafifu. Hakuwahi kuambiwa maneno kama yale na mtu yeyote na kwa mara ya kwanza alijihisi ana umuhimu mkubwa katika maisha ya Kim. Aligeuza uso wake na kumtazama Kim machoni. Alionekana kweli anamaanisha kile alichokisema.
Wakabaki kutazamana. Ile hali ya kupoteza matumaini iliyokuwa imetawala mawazoni mwake ikaanza kuondoka na kuchukuliwa na taswira ya Kim.
Kim aliendelea kumwaga sera na hatimaye akawa amefanikiwa kumteka Geneviv kimawazo. Akambembeleza kuwa amchukue mpaka nyumbani kwao ili wakaangalie namna ya kumtibu ugonjwa wake wa ajabu.
“And how about my mum?” (na vipi kuhusu mama yangu?) Aliuliza Geneviv wakati Kim akimsaidia kuinuka tayari kwa kurudi nyumbani kwa kina Kim.
“Worry not my dear, everything is going to be alright, nothing is impossible under the sun.”
(Usihofu mpendwa, kila kitu kitakuwa sawa, hakuna lisilowezekana). Kim alimjibu na wakaanza kutembea taratibu, Kim akiwa amemshikilia Geneviv kwani mwili wake haukuwa na nguvu kabisa.
Wakawa wanatembea taratibu kuelekea nyumbani kwa kina Kim. Jua lilizidi kuchomoza na watu wakawa wanaendelea na shughul zao kama kawaida. Kila walipopita Geneviv na Kim, watu walikuwa wakiwakodolea macho kama wanaojiuliza ni nini kilichotokea. Hakuna aliyeelewa, wakabaki kuduwaa.
*************
Bwana Magwaza, baba yake Kim, alikuwa amepata safari ya dharula ya kikazi kwa ajili ya kwenda kumsaidia mjane mmoja ambaye naye alikuwa na tatizo kama la Bi Patricia ambapo ndugu zake walikuwa wameuza mali zote zilizoachwa na mume wake na kumuacha akiteseka na watoto.
Alipanga kulala huko huko kuhakikisha kuwa anasaidia mjane yule kupata haki yake. Akiwa njiani wakati anaenda, alipigiwa simu na mmoja wa wafanyakazi wenzake ambaye alimpa taarifa ambayo ilimshtua na kumfanya aahirishe safari yake.
Alipigiwa simu na kupewa taarifa kuwa yule mwanamke ambaye jana yake walifanikiwa kuzuia nyumba yake kuuzwa kwa nguvu baada ya mumewe kufariki,( Bi Patricia) alikuwa akionekana mitaani akiwa na dalili zote za kuchanganyikiwa akili.
“Amepatwa na nini? Cant believe it! Lazima watakuwa ni ndugu zake tu…maskini! Basi hata hii safari inabidi niiahirishe. Lazima nije tuwashikishe adabu wote waliohusika.”
Bwana Magwaza alikuwa akiongea kwa simu na yule mfanyakazi mwenzake. Mara moja akaanza safari ya kurudi mjini. Kichwani alikuwa akijiona kama hajafanya kitu kumsaidia Bi Patricia kwani kama amechanganyikiwa lazima ile nyumba ingechukuliwa tena na kazi yote waliyoifanya ilikuwa ni bure.
Alitaka kuhakikisha kuwa anamuokoa na kumfanya apone kabisa. Alijua namna ambavyo angefanya kwani alikuwa na uzoefu wa kutosha wa masuala kama yale na haikuwa mara yake ya kwanza kushughulikia kesi zinazohusisha imani za kishirikina.
Safari yake ya kurudi ilimchukua masaa mengi , lakini hatimaye jioni ya siku ileile akawa tayari amesharudi. Alipitiliza mpaka nyumbani kwake ili akapate taarifa kutoka kwa mwanae Kim kwani alijua kwa vyovyote anaelewa kinachoendelea. Alipofika hakukuta mtu nyumbani kwake, akajua lazima watakuwa nyumbani kwa kina Geneviv, lakini hata alipofika kule nako hakukuwa na mtu.
Hakutaka kupoteza muda, akaanza kupeleleza hali ilivyokuwa. Haikumuwia vigumu kufahamu stori nzima kwani karibu kila mtu kwa siku ile alikuwa akilizungumzia suala lilelile. Kwa kutumia pesa aliwatafuta vijana wa kusaidia kuhakikisha wanampata bi Patricia siku ileile. Kazi ikaanza mara moja. Walianza kufuatilia njia zote na mitaa aliyokuwa anapita Bi Patricia.
Walizunguka karibu maeneo yote ambayo vichaa hupendelea kuishi. Walizunguka karibu majalala yote lakini kila mahali walipofika, waliambiwa kuwa mtu wanaemtafuta alikuwepo na walimuona muda mfupi uliopita. Kazi ile iliwachukua masaa mengi sana mpaka giza likawa limekolea. Bwana Magwaza hakutaka kukata tama mapema, aliendelea na kazi akisaidiwa na vijana wa mitaani. Mpaka inatimia saa sita za usiku bado walikuwa hawajafanikiwa kumpata Bi Patricia wala mwanae Geneviv.
Wakawa wameanza kukata tamaa.
“Hebu tujaribu kwa mara ya mwisho kwenye lile jalala pale. Kama tukimkosa basi turudi kulala tutaendelea Kesho”
Aliongea Bwana Magwaza akionyesha kuwa ameshachoka kwani kazi walioyoifanya ilikuwa si ya kitoto. Walikuwa wamezungukia karibu mitaa yote bila mafanikio.
Wakalivamia jalala la mwisho kujaribu bahati yao kwa mara ya mwisho. Wote walishtuka kuona mtu akiinuka kwa kasi kutoka katikati ya takataka na kuanza kuwafukuza kwa mawe na fimbo.
“Ndiyo mwenyewe! Mkamateni kwa uangalifu msimuumize, mkamateni…” Bwana Magwaza aliwaamuru wale vijana baada ya kugundua kuwa yule ndio Bi Patricia waliyekuwa wakimtafuta. Hakuyaamini macho yake…
Baada ya purukushani ya muda mrefu hatimaye wale vijana walifanikiwa kumkamata na kumfunga kamba mikononi na miguuni.
Kwa haraka wakambeba juu juu mpaka barabarani ambako waliita taksi na kumkimbiza hospitali. Walipofika Hospitali, manesi walimpokea kwa kumdunga sindano ya usingizi ili atulie kwani alikuwa akifanya vurugu kubwa sana. Baada ya sindano ya usingizi kumlewesha, walianza kwa kumuosha mwili mzima kwani alikuwa hataminiki kwa uchafu. Baada ya kuwa safi walienda kumlaza kwenye wodi maalum ya wagonjwa wa akili. Wakaanza kumpatia tiba ya haraka.
Bwana Magwaza alikuwa akizunguka huku na kule akiwa kama asiyeamini yale yaliyomkuta Bi Patricia. Muda mfupi baadae aliitwa kwenye chumba cha daktari…wakawa wanazungumza. Alikuwa ni daktari Zayumba, yule aliyewahi kuwa msaada mkubwa sana kwa Bi Patricia na mwanae Geneviv siku za nyuma, kabla hata ya kifo cha Mzee Rwakatare.
Kwa pamoja wakawa wanatafakari nini cha kufanya ili kuyamaliza mateso ya muda mrefu aliyoyapata Bi Patricia na mwanae Geneviv.
“Lazima tuwasaidie sana kwa kweli! Mimi ni shahidi wa matukio ya kutisha yaliyowapata. Kwa kweli inahitaji moyo jasiri kuweza kuvumilia” Aliongea Daktari Zayumba wakati wakiendelea na majadiliano na Bwana Magwaza.
***********
Kim alimsaidia Geneviv mpaka wakafika nyumbani kwao. Walipofika alimkalisha kwenye kiti na kwa haraka akaanza kuandaa maji ya moto kwa ajili ya kumsafishia Geneviv ambaye sasa mwili wake ulikuwa umeanza kutoa harufu.
Muda mfupi baadae maji yakawa tayari…
“Would you allow me to wash your body?”
(Utaniruhusu nikuogeshe?)
Kim alimuuliza Geneviv kimasihara akitaka kuona atamjibu nini.
“Stop kidding kim, I will do it on my own, I know you care intensely for me, thank you very much”
(Acha utani Kim, ntaoga mwenyewe…najua unanijali kupita kawaida, ahsante sana)
Wakawa wanatabasamu. Taratibu furaha ilianza kurudi moyoni mwa Geneviv kwani Kim alikuwa akijitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote kumhudumia. Akamsindikiza mpaka bafuni na kumuwekea kila kitu tayari. Geneviv akaanza kuoga kwa kutumia dawa maalum ya kusafishia vidonda.
Baada ya kumaliza kuoga, Geneviv alijikuta akipata nguvu mpya. Kim alikuwa akihangaika kuandaa kifungua kinywa kwa ajili ya Geneviv, na alipomaliza kuoga alimkaribisha mezani. Wakati wanaendelea kupata kifungua kinywa, baba yake Kim akawa anaingia.
Alishtuka kwa jinsi Geneviv alivyokuwa. “Unamshangaa saizi wakati hapo ana nafuu kubwa kabisa, alikuwa na hali mbaya sana. Tumshukuru Mungu kwa kumnusuru” Aliongea Kim wakati akimkaribisha baba yake aliyeonekana bado kaduwaa kwa hali aliyomuona nayo Geneviv. Bwana Magwaza hakutaka hata kupumzika. Aliingia ndani na kubadilisha nguo, kisha akawa anajiandaa kumpeleka Geneviv hospitali.
“Malizeni haraka twende Hospitali Geneviv akatibiwe”
Muda mchache baadae wakawa tayari kwa kuondoka. Bwana Magwaza hakutaka kumwambia Geneviv mahali aliko mama yake, alitaka kufanya kama Surprise ili kuwaongezea nguvu ya kupona haraka. Wakaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea Hospitali ikaanza. Walienda kwenye hospitali ile ile aliyolazwa mama yake.
Baada ya kuhakikisha Bi Patricia anahudumiwa kisawasawa, Bwana Magwaza na daktari Zayumba wanajadiliana nini cha kufanya ili kukomesha mateso ya muda mrefu yaliyoharibu maisha ya Bi Patricia na mwanae Geneviv. Baada ya kufikia muafaka wa nini cha kufanya, Bwana Magwaza anaaga na kurudi nyumbani kwake akiacha Bi Patricia anashughulikiwa kikamilifu.
Anapofika nyumbani kwake, anashangaa kumkuta mwanae Kim akiwa na Geneviv, na kinachomshtua zaidi ni hali ya Geneviv kwani mwili wake umeharibika vibaya kwa ugonjwa wa ajabu. Bila kupoteza muda, anaamua kumpeleka Geneviv Hospitali usiku huo huo
“Malizeni haraka twende Hospitali Geneviv akatibiwe” Aliongea Bwana Magwaza akimharakishe Kim amalize kumsaidia Geneviv kula haraka ili waende Hospitali.
Muda mchache baadae wakawa tayari kwa kuondoka. Bwana Magwaza hakutaka kumwambia Geneviv mahali aliko mama yake, alitaka kufanya kama Surprise ili kuwaongezea nguvu ya kupona haraka. Wakaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea Hospitali ikaanza. Walienda kwenye hospitali ile ile aliyolazwa mama yake.
Walipofika Hospitali, Bwana Magwaza alipitiliza mpaka ofisini kwa Daktari Zayumba na akamueleza alichokutana nacho nyumbani kwake juu ya hali ya Geneviv.
“Are you serious? Its like a miracle! Where is she?” ( unasema kweli? Ni kama muujiza! Yuko wapi?) Alikuwa akiongea mfululizo daktari Zayumba akiwa kama haamini vile. Alikuwa na shauku ya kumuona Geneviv alivyo. Bwana Magwaza alimuelekeza kuwa amewaacha ndani ya gari pale nje. Kwa haraka wakatoka na kueleka pale Bwana Magwaza alipokuwa amewaacha Geneviv na Kim.
Daktari Zayumba hakuyaamini macho yake kama kweli Yule ni Geneviv aliyekuwa akimfahamu. Alijikuta akisikia uchungu mkali moyoni na kumuonea huruma sana. Hakutaka kupoteza muda zaidi, akawaita manesi ambao nao bila ya kupoteza muda walimchukua hadi wodini walikoanza kumhudumia.
Walianza kwa kumsafisha mwili wote kwa kutumia dawa maalum ya kuzuia uambukizo (Disinfectant) kisha wakamtundikia dripu ya dawa. Alilazwa na matibabu yakawa yanaendelea. Hakujua kuwa mama yake yuko hapohapo Hospitali katika wodi nyingine akipewa huduma nzito.
Baada ya kuhakikisha wote wanahudumiwa vizuri,Bwana Magwaza alirudi nyumbani kwake, akimuacha Kim pale Hospitali. Alikuwa akienda kuandaa mipango madhubuti ya kuwashikisha adabu ndugu wa mzee Rwakatare ambao ndio walikuwa sababu kubwa ya Bi Patricia na mwanae kupata mateso makubwa namna ile. Alijiapiza kuwashikisha adabu ili iwe fundisho kwa wote wenye tabia kama ile.
Hakupata shida kuamua nini cha kufanya kwani tayari alishakuwa na uzoefu wa kutosha wa kupambana na jamii zinazoamini ushirikina. Aliendelea kupanga mikakati kabambe, na akawa anasubiri kupambazuke ili aanze kazi mara moja.
Saa kumi na moja Alfajiri, Bwana Magwaza alikuwa mbele ya gereza kuu alimokuwa amefungwa Bwana Magafu (Shemeji wa Bi Patricia).
Aliomba kuonana na mkuu wa gereza ambapo alimsimulia kila kitu kilichosababishwa na Bwana Magafu na ndugu zake kwa Bi Patricia na mwanae.
Tofauti na nchi nyingine, serikali ya Blaziniar ilikuwa ikiamini juu ya uchawi na nguvu za giza na ilipitisha sheria kadhaa za kuwatia hatiani watu wanaoshutumiwa kuwadhuru wengine kichawi, ambapo hukumu yao ilikuwa kali kuliko ya wezi au majambazi.
Bwana Magwaza na mkuu wa gereza walifikia uamuzi wa kwenda kuwatia nguvuni wote waliohusika na nguvu za giza zilizowadhuru Bi Patricia na mwanae Geneviv. Kulipopambazuka, Bwana Magafu alienda kutolewa gerezani na akiwa chini ya ulinzi mkali, alitakiwa kuwapeleka askari zaidi ya sita kijijini kwao ili wakawashughulikie wote waliohusika na kuwadhuru Bi Patricia na mwanae.
Magari mawili ya polisi aina ya Defender, yalikuwa yakitimua vumbi kuelekea kijijini iliko asili ya ukoo wa mume wa Bi Patricia, ukoo wa Rwakatare. Bwana Magafu alikuwa amefungwa pingu akiwa chini ya ulinzi wa polisi wenye silaha akitakiwa kuonyesha njia ya kuelekea kijijini kwao. Baada ya safari ndefu, hatimaye wakawa wamekikaribia kijiji wanachoishi ukoo wa Rwakatare.
Wanakijiji walipoona magari mawili yanakuja kwa kasi huku yakitimua vumbi, wakajua ni Bwana Magafu, waliyemtuma kwenda kuuza nyumba na kumrithi mjane ndio alikuwa anarudi. Waliamini ameshamaliza kazi aliyotumwa na ukoo, wakawa wanapiga vigelegele na kushangilia wakijua utajiri wote sasa ni mali yao.Walishangaa kuona polisi wenye silaha wakishuka garini wakiwa na ndugu yao Magafu, akiwa amefungwa pingu. Kila mmoja akianza kutafuta njia ya kukimbilia, lakini polisi waliwawahi na kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
Bila ya kupoteza muda, viongozi wa ukoo walitiwa nguvuni na kuunganishwa na ndugu yao Magafu na baada ya kuwapakia ndani ya magari ya polisi, Bwana Magafu alipewa nafasi ya kuzungumza na wanaukoo wanaobaki. Aliwaonya kuwa wakitaka ndugu zao waachiwe huru, lazima wahakikishe Bi Patricia na mwanae wanapona haraka iwezekanavyo,vinginevyo ndugu zao wangeishia jela.
Aliwatolea vitisho vingi ikiwa ni mbinu kali ya kisaikolojia ya kuwamaliza nguvu za uchawi. Mbinu kama ile ilikuwa ilikuwa ikitumiwa sehemu nyingi kunapotokea shutuma za matumizi ya nguvu za giza na matokeo yake ilikuwa ni kufanikiwa kuwamaliza kabisa wachawi na kuwafanya waishiwe nguvu za kuroga tena.
Baada ya kuwachimba mkwara wa nguvu, magari ya polisi yalianza safari ya kurudi mjini, viongozi watano wa ukoo wakiwa wameunganishwa na Bwana Magafu na kutiwa pingu chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Baada ya masaa mengi ya safari ngumu, hatimaye waliwafikisha gereza kuu na wakaingizwa ndani chini ya ulinzi mkali. Walifungiwa kila mmoja kwenye chumba chake peke yake ili kuwazuia kuwasiliana na kukusanya upya nguvu ya giza.
****
Masaa machache baada ya ndugu wa ukoo wa marehemu Rwakatare kutiwa gerezani kwa makosa ya kusababisha mateso kwa Bi Patricia na mwanae kwa kutumia nguvu za giza, wana ukoo waliokuwa wamebakia kijijini waliitana kwenye kikao cha dharula cha kujadili nini cha kufanya ili kuwaokoa wenzao.
Walifikia muafaka wa kutegua mitego yao yote ya kichawi waliyokuwa wamewategea Bi Patricia na mwanae ili wapone. Hawakuwa na njia nyingine zaidi ya hiyo kwani walishaambiwa kuwa mpaka wapone ndipo ndugu zao watakapoachiwa huru. Wazee wa mila walianza kufanya mambo yao wakizivunja nguvu zote walizokuwa wamezitega ili kuwadhuru Bi Patricia na mwanae.
Katika hali ya kushangaza, Bi Patricia alirudiwa na akili zake kwa haraka na akajikuta yuko wodini manesi wakikimbia huku na huko kumsaidia.
“She is awake! Amepona!” manesi walikuwa wakipeana taarifa baada ya kuona Bi Patricia amerejewa na fahamu zake kwa haraka mno.
Hakuna aliyeamini kilichotokea kwani Bi Patricia alikuwa amepona kabisa ndani ya muda mfupi. Alikuwa hajui ni nini kilichomtokea mpaka akawa na hali kama ile. Akawa anawauliza manesi ambao kila mmoja alikuwa akimpa pole kwa yaliyompata.
Muda huo huo, kwenye wodi aliyokuwa amelazwa Geneviv, manesi walikuwa wakishangaa kilichotokea. Ndani ya muda mchache mno, Geneviv alipata nafuu kubwa mno. Vidonda vyote mwilini vilikauka na alama zikawa zinapotea haraka.
“What is happening here?”(Nini kinachotokea hapa) Aliuliza nesi mmoja baada ya kushindwa kuelewa kilichokuwa kikiendelea kwani mtu na mama yake walikuwa wakipata nafuu kwa kasi ya kushangaza.
“Ama kweli hapa duniani kuna uchawi! Kumbe ni kweli walikuwa wamerogwa…maskini! Mungu wao amewapigania” manesi walikuwa wakizidi kujadiliana. Muda mfupi baadae, Bwana Magwaza na mwanae Kim walikuja kutazama hali za wagonjwa wao zinavyoendela. Hakuna aliyeamini kumuona Bi Patricia akiwa amerudiwa na akili zake timamu huku Geneviv naye naye akiwa ameshapona ugonjwa wa ajabu. Walienda ofisini kwa daktari Zayumba na wakamuomba wawakutanishe rasmi, mtu na mama yake kwani kwa muda wote huo hakuna aliyejua mwenzake yuko wapi.
Bi Patricia alikuwa bado akishangaa shangaa mle wodini, mara akaona mlango unafunguliwa na wanaingia watu wanne, wakiongozwa na mwanae Mpendwa Geneviv. Alijikuta akiinuka kwa nguvu na kumkimbilia mwanae. Walikumbatiana kwa nguvu hadi wakadondoka wote hadi chini. Hakuna aliyeamini kuwa hatimaye wamekutana tena baada ya kupitia kipindi kigumu kuliko vyote maishani mwao. Waliendelea kukumbatiana pale chini huku kila mmoja akitoa machozi ya furaha.
Kim naye alikumbatiana na baba yake kwa furaha. Hakika walijiona kama mashujaa baada ya kufanikiwa kuwaunganisha Geneviv na mama yake. Daktari Zayumba alikuwa amesimama pembeni akiwatazama walivyofurahi. Baada ya muda, waliinuka na Bwana Magwaza akawa anaongea na Bi Patricia wakati Kim akiwa bega kwa bega na Geneviv.
Baada ya kuhakikisha hali zao zimekuwa nzuri na za kuridhisha, Bwana Magwaza aliomba waondoke hadi nyumbani kwake hadi watakapopona kabisa. Bi Patricia aliridhia na wakaanza kujiandaa kutoka kuelekea kwa kina Kim. Baada ya muda wakawa tayari wameshatoka Hospitali na wakawa wanaelekea nyumbani kwa kina Kim.
*******
Baada ya kufika nyumbani kwa Bwana Magwaza, Bi Patricia na mwanae walikaribishwa kwa ukarimu mno, wakaingia ndani na bila kupoteza muda Kim akaingia jikoni kuanza kuandaa chakula cha jioni.
Historia ya Kim na baba yake, ilikuwa tofauti na ambavyo ungewadhania. Kwa kuwa walikuwa wakiishi wawili tu, Kim alikuwa na uwezo wa kufanya shughuli zote za nyumbani.
Aliweza kupika, kuosha vyombo, kupiga deki, kufua na kazi zote ambazo vijana wengi wa kiume wa siku hizi hawawezi. Alilazimika kujua kufanya shughuli zote hizi sio kwa kupenda ila kwa matatizo ambayo yalitokea akiwa bado mtoto mdogo. Kwa kifupi ni kwamba Kim alikuwa hamjui mama yake zaidi ya kumuona kwenye picha, kwani alifariki dunia kutokana na matatizo aliyoyapata akiwa na ujauzito wa Kim na alimuacha akiwa na siku tatu tu duniani.
Baada ya kuondokewa na mkewe kipenzi, Bwana Magwaza alikuwa na wakati mgumu sana kwani kichanga Kim alikuwa akihitaji sana malezi ya karibu ya mama, lakini aliyakosa. Alilelewa na mahausigeli na alikulia maziwa ya ng’ombe mpaka alipokuwa mkubwa. Bwana Magwaza alijiwekea nadhiri ya kutooa tena siku za karibuni kwani aliamini asingeweza kumpata mwanamke aliyekuwa sawa na mkewe.
Kwa kuwa baba yake alikuwa ni mfanyakazi, Kim alipoongezeka umri kidogo, alilazimika kujifunza kufanya shughuli za nyumbani mwenyewe. Baba yake alikuwa na kazi ya ziada ya kumfanya asimkumbuke mama yake na alijitahidi kumtimizia mahitaji yake yote ikiwa ni pamoja na kumtafutia wafanyakazi wa kumlea, lakini Kim alipenda kujilea mwenyewe.
Kwa kuwa hakuwahi kupata penzi la mama, uwepo wa Bi Patricia na mwanae Geneviv pale nyumbani kwao, ulimfanya ajisikie hali tofauti ambayo hakuwahi kuihisi hapo awali. Alijisikia amani sana kukaa na ‘mama’ wa kufikia. Akawa anahangaika jikoni kuandaa chakula ili kuwafurahisha wageni. Bwana Magwaza alikuwa sebuleni na wageni, akiendelea kubadilishana mawazo na Bi Patricia. Geneviv naye alikuwa ametulia pembeni akiwasikiliza mama yake na baba Kim wakiwa kwenye mazungumzo yao. Baadae aliamua kumfuata Kim jikoni aliyekuwa bize kuandaa chakula cha jioni.
“Nataka nikusaidie Kupika na wewe ujisikie raha, maana najua kila siku unajipikia mwenyewe…”
Aliongea Geneviv akimtania Kim, wakawa wanacheka huku Geneviv akianza kumsaidia kazi ndogondogo. Ilikuwa ni jioni ya kipekee sana kwao. Bwana Magwaza naye aliendelea kuongea na Bi Patricia sebuleni, wakijadiliana namna ya kukomesha kabisa matatizo mfululizo yaliyokuwa yanamuandama yeye na mwanae.
Alimsimulia siri ya wao kupona ghafla namna ile, na akamueleza namna walivyoenda kuwatia nguvuni ndugu wa ukoo wa mumewe.
“Do You mean they are under arrest right now?”( Unamaanisha kuwa sasa wako chini ya ulinzi?)
Aliuliza Bi Patricia akionekana kushtuka. Bwana Magwaza alimueleza kila kitu na akazidi kusisistiza kuwa wao (Bi Patricia na Mwanae) wamepona baada ya ndugu zao kuwekwa gerezani kwa muda huku wakiacha vitisho kwa ndugu wengine waliobakia kijijini. Bwana Magwaza alitegemea Bi Patricia atafurahishwa sana kusikia ndugu zake waliomsababishia matatizo makubwa wamefungwa jela, lakini hali ilikuwa tofauti.
Bi Patricia alijisikia vibaya ndugu wa mumewe kufungwa kwa ajili yake…japokuwa walikuwa wamemfanyia unyama na ukatili wa kutisha. Hata baada ya kifo cha mumewe, bado alikuwa akiwapenda na kuwaheshimu sana ndugu wa mumewe na hakupenda wapatwe na jambo lolote baya.
“ Mi nilishawasamehe kwa yote waliyonifanyia na Mungu ndiye atakayenilipia, naongea kutoka ndani ya moyo wangu…”
Aliongea Bi Patricia kwa masikitiko akimueleza Bwana Magwaza kilichokuwa moyoni mwake. Zaidi alimsisitiza kuwa kwa kuwa wao wameshapona, basi kama kuna uwezekano afanye mpango wa kuwatoa ndugu zake wote gerezani, kuanzia bwana Magafu na wale wengine wote. Bwana Magwaza alibaki kumshangaa Bi Patricia kwani hakutegemea kusikia kauli kama ile kutoka kwake.
Alitegemea kuwa kwa sababu waliwafanyia unyama sana kiasi cha kutaka kuwatoa uhai, angekuwa na chuki kali dhidi yao. Aligundua kuwa Bi Patricia alikuwa wa kipekee sana. Ilibidi naye aeleze kilichokuwa moyoni mwake.
“You are soo unique Patricia, tangu kifo cha mke wangu mpendwa sijawahi kukutana na mwanamke mwenye roho kama yako, You deserve good!”
Bi Patricia alitabasamu baada ya kusifiwa na Bwana Magwaza na muda si mrefu, Kim na Geneviv wakawa wameshamaliza kupika na wakawa wanasaidiana kuandaa meza.
Ilikuwa ni jioni ya kipekee sana kwao. Walikuwa wamekaa kama familia iliyokamilika, ikiwa na baba, mama na watoto wawili. Wote walikuwa na furaha isiyo na kifani, huku Bwana Magwaza akiwa mwingi wa masihara, hali iliyowafanya wakifurahie sana chakula chao. Baada ya kumaliza kula, Geneviv na Kim walisaidiana tena kutoa vyombo na kusafisha meza. Wakarudi kujumuika na wazazi wao.
“Natamani sana familia hizi ziungane na kuwa familia moja, hakika tutaishi maisha ya furaha sana na bila shaka kila mmoja atasahau matatizo yaliyompata” Aliongea kwa sauti ya chini Bwana Magwaza akiwa anamtazama usoni Bi Patricia. Bi Patricia hakujibu kitu, wakawa wanaendelea kutazamana na Bwana Magwaza.
Geneviv naye alikuwa akiongea kwa sauti ya chini akimnong’oneza Kim kuwa anatamani siku moja yeye (Geneviv) awe mama na Kim awe baba na wawe na watoto wawili kama walivyokuwa pale sebuleni, Kim alitabasamu na wakawa wanatazamana na Geneviv. Baadae ukimya mkubwa ukatawala mle ndani. Bwana Magwaza alikuwa akitazamana na Bi Patricia huku macho yao yakiwa kama yanayoongea lugha moja, huku Geneviv naye akiwa anatazamana na Kim, nao wakionekana kuzungumza lugha moja ya ishara.
Baadae Bwana Magwaza aliuvunja ukimya na kuwataka wageni wakapumzike kwenye chumba chao maalum walichoandaliwa. Wakatakiana usiku mwema na Kim akainuka kwenda kuwaonyesha chumba chao. Bwana Magwaza naye aliinuka na kuelekea chumbani kwake. Kim alirudi sebuleni, na kama kawaida yake akachukua daftari zake na kuanza kujisomea. Kwa kawaida kila siku alikuwa akijisomea mpaka usiku wa manane kwani masomo ya sekondari yalikuwa magumu kwake hivyo kulazimika kutumia muda mwingi kujisomea.
Geneviv hakupata usingizi mpaka usiku sana, alikuwa akitamani kumfuata Kim pale sebuleni anapojisomea, lakini akaogopa kumuudhi mama yake kwani asingefurahia kitendo kile na angemuhisi ameanza tena tabia mbaya. Alipohakikisha mama yake amelala kabisa, alinyata na kufungua mlango. Akatoka mpaka sebuleni ambako alimkuta Kim akiendelea Kujisomea.
“Vipi! Ulikuwa bado hujalala?” Aliongea Kim kwa sauti ya kunong’ona akimuuliza Geneviv.
Geneviv hakuwa na jibu zaidi ya kumdanganya kuwa alipolala tu amemuota na ndio maana ameamua kuamka na kumfuata. Kim akatabasam kwa uchovu na kumkaribisha Geneviv, ambaye alimsogelea na kukaa jirani kabisa na Kim, akiwa amevaa kigauni cha kulalia. Kim alielewa kwa haraka kilichokuwa kinataka kutokea. Moyoni mwake alikuwa na jeraha kwani bado alikuwa na kumbukumbu ya kuangukia kwenye mikono ya msichana hatari, Alice, ambaye alimuwekea madawa ya kulevya kwenye soda na kufanikiwa kulala naye mpaka asubuhi bila ridhaa yake.
Kwa kuwa alimuamini sana Geneviv, aliona huo ni muda muafaka wa kumwambia kilichomtokea kwani aliamini angepata ahueni moyoni mwake. Alimpenda Geneviv na alitaka afahamu kila kitu kumhusu yeye. Wakiwa wamekaa jirani kabisa, alianza kumueleza kwa upole kilichomtokea . Geneviv alitega masikio kwa makini kutaka kusikia Kim atamwambia nini.
Kim alimueleza kila kitu kilichomtokea mpaka alipojikuta akilala kitanda kimoja na Alice.
“Whaaat! Ulilala na Alice? Mlitumia Kinga?”
Aliuliza kwa mshangao wa ajabu Geneviv, hali iliyomshtua Kim. Alijibu kwa kutingisha kichwa kuonyesha kuwa hakuna tahadhari yoyote iliyotumika alipokutana na Alice.
“My God! Alice is a harlot…and the great possibility is that she is living with H.I.V!” (Mungu wangu! Alice ni changudoa na uwezekano mkubwa ni kwamba anaishi na virusi vya Ukimwi) Aliongea Geneviv huku akimkumbatia Kim ambaye sasa alishtuka kupita kawaida kusikia kuwa Alice alikuwa ni changudoa. Kilichomstua zaidi ni kwamba hawakutumia kinga yoyote. Hiyo ilimaanisha kuwa kama ni kweli Alice alikuwa na virusi vya Ukimwi, basi Kim naye alishavipata.
Alijikuta akishindwa kujizuia na kuanza kulia kwa sauti, hali iliyowafanya Bi Patricia na Bwana Magwaza kushtuka. Wote wakatoka vyumbani mwao na kwenda sebuleni kuangalia kumetokea nini usiku wote ule mpaka Kim apige kelele.
“Whats happening here?”
Aliuliza bwana Magwaza akitembea kwa haraka kuelekea pale Geneviv na Kim walipokuwa wamekaa.
Ilibidi Kim atumie uongo ili kuwatuliza baba yake na Bi Patricia. Alidanganya kuwa kichwa kimeanza kumgonga ghafla na ndio maana alikuwa akilia . Aliogopa kueleza ukweli halisi kwani hakujua aanzie wapi kueleza. Geneviv alikuwa amekaa pembeni yake akiwa kimya, uso kauinamisha chini. Bi Patricia na Bwana Magwaza waliamini uongo uliosemwa na Kim kwani hawakudhani kuwa anaweza kuwa amewadanganya.
“Unasoma sana ndio maana kichwa kinakuuma, haya nenda kapumzike mpaka asubuhi, kama bado hali sio nzuri itabidi tuende Hospitali kupima damu!”
Aliongea Bwana Magwaza wakati akimsaidia Kim kunyanyuka kutoka pale alipokuwa amekaa. Alimpeleka mpaka chumbani kwake na akahakikisha amelala, ndipo naye akatoka na kuelekea chumbani kwake.
Geneviv na mama yake nao walienda kulala kwenye chumba chao.
“Sasa wewe usiku wote huu ulikuwa unafanya nini sebuleni wakati mwenzio anajisomea?” Aliuliza Bi Patricia akionyeshwa kukerwa na kitendo cha Geneviv kutoka na kumfuata kim sebuleni. Ilibidi adanganye kuwa alikuwa akimuomba amfundishe masomo ya sekondari.
Bi Miriam alimkubalia kwa shingo upande ingawa alishahisi kuwa zaidi ya urafiki wa kaka na dada, kuna kitu kilichokuwa kikiendelea kati ya Kim na mwanae.
“Yule ni kaka yako kabisa, na kuna uwezekano tukawa tunaishi hivi siku zote, usije kunitia aibu tena kwa ujinga wako, mheshimu kama kaka yako na sio zaidi ya hapo”
Aliongea Bi Patricia wakati akimpa somo mwanae Geneviv, ambaye hakujibu kitu zaidi ya kugeukia ukutani akiwa amekunja sura na kujifunika mpaka usoni. Aliona kama mama yake anamuimbia wimboasioupenda.
Aliendelea kutafakari kauli ya mama yake na hakuelewa alikuwa akimaanisha nini alivyomwambia kuwa yule ni kaka yake na wataendelea kuishi vilevile siku zote.
Alishampenda Kim na alikuwa tayari kuwa naye katika hali yeyote ile kwani alionyesha kumjali sana wakati walipokuwa na matatizo makubwa.
Fikra nyingine zilizomtesa Geneviv usiku kucha, ilikuwa ni kitendo cha Alice alichomfanyia Kim. Alimuona Alice kama muuaji na alijikuta akimchukia mno. Aliendelea kumlaumu sana kwa kumharibia uhusiano wake uliokuwa unataka kuchanua kama ua ridi.
Pamoja na yote, alijiapiza kuwa lazima awe na Kim hata iweje. “I Love him, He is my heart!”( Nampenda nay eye ndio moyo wangu).
Geneviv alikuwa akijisemea kimoyomoyo huku akijifuta machozi yaliyokuwa yanaliloanisha shuka lake. Kim naye hakupata usingizi hata tone. Hakutaka kuamini kuwa ni kweli amenaswa kirahisi namna ilê kwa Alice. Katika maisha yake hakuwahi kujihusisha kimapenzi na msichana yeyote, alikuwa mgeni kabisa katika uwanja wa huba.
Alice ndio alikuwa wa Kwanza kwake, ingawa naye haikuwa dhamiri yake kufanya nae waliyoyafanya. Kilichomtisha zaidi ni kusikia kuwa alikuwa changudoa. Siku zote alikuwa akiwaogopa machangudoa kama moto wa Jehanum. Kamwe hakutaka kuamini kuwa anaweza kuwa ameambukizwa ugonjwa hatari na Alice.
Alipanga kuwa kutakapopambazuka tu, lazima ajihimu nyumbani kwa Alice. Hakuelewa anataka kwenda kufanya nini ingawa alijikuta akiingiwa na roho kali ya kisasi.
“I don’t deserve this! Ooh My God! Save me from this hell fire.” ( Sistahili haya, Eeh Mungu wangu niokoe kutoka kwenye moto huu wa jehanum)
Aliongea Kim huku akilia kwa uchungu.
Kulipopambazuka tu, Kim alijihimu na kuelekea nyumbani kwa Alice. Ilikuwa bado ni asubuhi sana na Alice alikuwa bado amelala kwani alirudi usiku wa manane kutoka kwenye shughuli zake za kuuza mwili. Kim aligonga mlango kwa hasira, na muda mfupi baadae Alice akamfungulia. Alionekana kuchoka sana na alikuwa amejifunga kanga moja tu.
“Aah kumbe ni wewe baby wangu! Karibu sweetie” Alice alionyesha uchangamfu wa kinafiki na akamshika Kim mkono na kumvutia ndani.
Japokuwa Kim alikuwa amepania kumfanya kitu mbaya, kwa jinsi Alice alivyompokea, alijikuta akiishiwa nguvu na akawa anamwaga machozi kama mtoto. Alijihisi dhaifu sana mbele ya Alice, kuliko hata akivyokuwa akijihisi anapokuwa na Geneviv.
Alice alimvuta mpaka kitandani na akamsogelea karibu kabisa. Akashtuka kumuona akimwaga machozi kama mtoto.
“Jamani vipi tena mbona wantisha asubuhi yote hii, huyo mcharuko wako Geneviv ndio anakufanya ulie asubuhi yote hii”
Kauli ile ilimpandisha sana hasira Kim, akainuka kwa jazba na kumkwida Alice shingoni. Alianza kumhoji kwa hasira kuwa ni kwa nini ameamua kumuua.
“Mbona sikuelewi? Nimekuua kivipi! Au mcharuko wako ndio amekutuma uje kunifanyia fujo asubuhi yote hii, ntapiga kelele niseme unataka kunibaka”
Aliongea Alice kwa jazba akijaribu kumtoa Kim mwilini mwake.
Ilibidi Kim awe mpole kwani alikuwa amekutana na maji ya shingo, kisiki cha mpingo Alice. Alimuachia na kukaa kwenye stuli akiwa amejiinamia kichwa chini.
Baada ya kuona ametulia Alice alimsogelea kwa upole na kuanza kumuuliza ni nini kimemsibu mpaka achanganyikiwe namna ile. Alice alikuwa fundi kisawasawa wa kubembeleza. Kim alijikuta akilainika na kuanza kueleza hofu yake baada ya kugundua kuwa kumbe Alice ni changudoa.
Alice hakuwa na aibu hata chembe, akampasulia kuwa ni kweli yeye ni changudoa na anafanya vile sio kwa kupenda bali hali ya maisha ndio inamfanya awe vile. Alimtoa wasiwasi kuwa katika kazi yake, siku zote alikuwa akiujali sana uhai wake na hakuwahi kukutana na mwanaume yeyote bila ya tahadhari, na akazidi kumsisitiza kuwa yeye (Kim) ndio alikuwa wa kwanza kwenda nae bila Kinga, na kama ushahidi aliinuka na kufungua begi lake kisha akamtolea cheti cha daktari.
“Nimeenda kupima wiki iliyopita tu, mimi ni mzima wa afya, sina ngoma kama watu wanavyonidhania, na ushahidi wa hili ni hiki cheti hapa.
Kama bado huamini tuongozane hata sasa hivi tukapime upya, mi najiamini sana kwani siku zote niko makini”
Aliongea Alice Kwa nyodo huku akiwa amemshikia kiuno Kim.
Kim alishusha pumzi ndefu na kukichukua kile cheti kutoka mikononi mwa Alice na kuanza kukisoma. Ni kweli kilionyesha kuwa Alice hana maambukizi ya virusi vya UKIMWI kama walivyokuwa wakihisi. Hakutaka kuamini haraka akahisi kuwa labda ni cheti feki alichokinunua mitaani.
Alice akazidi kumsisitiza kuwa kama haamini waongozane asubuhi hiyo hiyo mpaka Hospitali kurudia kupima. Kwa kiasi kikubwa imani ilimrudia Kim na akawa anapumua kwa nguvu kama ambaye haamini anachokisikia kutoka Kwa Alice. Akainuka kwa haraka na akawa anauendea mlango akitaka kutoka nje Alice alimuwahi na kumzuia mbele yake.
“Kim naomba unisamehe kwa kitendo nilichokufanyia, sikupanga kukufanyia vile siku ile ila nilipitiwa tu, naomba unisamehe sana”
Alikuwa akiongea Alice kwa lugha ya upole sana. Kim hakujibu kitu, akamsukumia pembeni na kutaka kutoka. Alice akamzuia tena na akamvaa mwilini kwa nguvu na kumrudisha ndani. Wakawa wanavutana kama majogoo yanayotaka kupigana.
Bwana Magwaza aliwahi sana kuamka na kwenda kumuangalia mwanae Kim anaendeleaje. Alipofika chumbani kwake alikuta hakuna mtu, akajua labda Kim yuko uani. Alijaribu kuita lakini hakuitikiwa. Alienda mpaka kwenye chumba cha wageni na kuwaamsha Bi Patricia na mwanae waliokuwa bado wamelala.
“Mwenzio yuko wapi?” Bwana Magwaza alimuuliza Geneviv kama anajua alipo Kim. Hakuna aliyekuwa na Jibu ni wapi alikoenda Kim asubuhi yote ile. Wakabaki kutazamana usoni. Walipoenda kuangalia mlango wa kutokea nje, ulikuwa wazi kuonyesha kuwa Kim alikuwa ametoka nje.
Kengele ya hatari ikalia kichwani mwa Geneviv.Akahisi kuwa kwa vyovyote lazima Kim atakuwa amewahi kwenda kwa Alice kumfanyia vurugu kwa yale aliyomfanyia. Kwa jinsi alivyokuwa akimfahamu Alice, alijua lazima watafanyiana sana fujo na Kim. Akaingia ndani kwa haraka na kuvaa nguo, kisha akatoka kwa kasi akiaga kuwa anaenda kumuangalia nje.
Alikimbia mpaka anakoishi Alice na muda mfupi baadae akawa ameshafika. Alianza kusogea kwa kunyata kusikia kama Kim alikuwa ndani… akaisikia sauti ya Alice akinong’ona chinichini kutokea ndani. Akajua lazima Kim yuko mle ndani.
****
Baada ya Geneviv kuondoka kwa kasi, Bwana Magwaza na Bi patricia walibaki wakitazamana wakiwa hawaelewi nini kinachoendelea.
“Achana nao hao, wanajuana wenyewe wala usiumize kichwa chako”
Aliongea bwana Magwaza akimshika mkono Bi Patricia, wakaingia ndani.
Walikuwa wamebaki peke Yao, Bwana Magwaza akaona huo ndio muda muafaka wa kujadili na Bi Patricia juu ya hatma ya maisha yao. Alirudia kauli yake aliyoitoa usiku wa siku iliyopita.
“Patricia, naamini wewe ni mwanamke wa kipekee sana na bila shaka utaelewa vizuri ninachotaka kukwambia. Nimekuwa nikifikiria sana na nimeona itakuwa jambo la maana sana kuziunganisha familia zetu na kuwa kitu kimoja. Mke wangu alishafariki siku nyingi sana na kuniacha mpweke hapa duniani. Najua kuwa na wewe unajisikia upweke sana baada ya mumeo kutangulia mbele za haki… Kwa nini tusitoane upweke katika siku za maisha yetu yaliyobakia hapa duniani?”
Bwana Magwaza alikuwa akimwaga sera za kiutu uzima. Bi Patricia alianza kujiumauma vidole kama msichana mdogo akikosa jibu la kumpa Bwana Magwaza. Ni kweli kabisa kuwa na yeye alikuwa akijisikia upweke sana baada ya kifo cha mumewe, lakini alishindwa kuelewa jamii ingemchukuliaje.
********
Alice alihakikisha anaitumia nafasi ile ya Kim kumfuata chumbani kwake asubuhi ile kikamilifu. “Leo amejileta mwenyewe, ndege mjanja hunaswa katika tundu bovu!” Alice alikuwa akijisemea kimoyomoyo huku akitabasamu wakati wakitazamana na Kim. Zile hasira zote alizokuja nazo Kim zilikuwa zimeyeyuka kama barafu juani. Akajikuta kwa mara nyingine akiingia kwenye mtego wa mcharuko Alice. Alijaribu tena kutaka kutoka lakini Alice alimrudisha ndani na akawa anamfanyia vituko vingi ili kwa mara nyingine apate alichokitaka.
“Kim bwana usiwe kama mtoto, mwenzio nakutaka uwe mume wangu! Ukinikubalia utakuwa umeyaokoa maisha yangu, ntaachana kabisa na biashara hii hatari ninayoifanya! Please Kim save my soul!” Aliongea Alice kwa sauti laini huku akiyalazimisha machozi kutoka machoni mwake na akapiga magoti mbele ya Kim. Wizi mtupu!
Miongoni mwa kasoro alizokuwa nazo Kim ni kuwa na huruma kupita kiasi. Alikuwa akimchukia Alice kwa aliyomfanyia, lakini kwa upande wa pili alijikuta akianza kumuonea huruma kutokana na aina ya maisha aliyokuwa akiishi. Aliogopa sana machangudoa kwani kazi yao ilikuwa ikiwaweka katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Kauli ile aliyoitoa Alice huku akipiga magoti mbele yake ilizidi kummaliza nguvu. Akaishiwa la kuongea akabaki kumtazama Alice kwa huruma. Alice naye hakutaka kulaza damu, akazidisha vituko na kuzidi kumtega Kim. Muda mfupi baadae wakawa wamekumbatiana wakirushana huku na kule juu ya kitanda. Alice alishavua kanga moja aliyokuwa ameivaa na kubaki akiwa mtupu, hali iliyozidi kumuweka Kim mtegoni. Akaanza kumsalaula Kim. Akiwa anamalizia kumvua bukta yake, walishtukia mlango ukisukumwa kwa nguvu na mtu akaingia kwa kasi ya Ajabu.
“Kim! Kim! What are you doing with this bitch? Alice! Kwa nini unanitenda hivi lakini? Ooh my god! Why me?”
Geneviv alikuwa akipiga kelele huku akilia baada ya kuwafuma Alice na Kim wakiwa kama walivyozaliwa juu ya kitanda cha Alice. Alijikuta akipatwa na uchungu mkali moyoni kiasi cha kuanza kulia kama mtoto mdogo akijitupa chini kwa fujo.
Kim alipatwa na mshtuko mkubwa kupita kiasi. Alishindwa kuelewa ni nini kilichotokea, akawa kama yuko ndotoni. Kwa haraka alianza kutafuta nguo zake zilizokuwa zimetupwa chini na Alice. Alizivaa kwa upesi kisha akampigia magoti Geneviv aliyekuwa akigalagala chini akilia kwa uchungu mkubwa na kuanza kumuomba msamaha. Kuona vile Alice naye aliinuka na kufunga kanga yake kiunoni na kuanza kumvuta Geneviv kumtoa nje kwa madai kuwa alikuwa amemuharibia starehe yake.
Ikawa ni zogo mtindo mmoja kwani Geneviv naye alicharuka na kuinuka kwa hasira akitaka kupigana na Alice. Ilibidi Kim atumie uanaume wake kutuliza mambo kwani hakika kama watu wangeshuhudia kilichokuwa kikiendelea mle ndani asubuhi yote ile, ingekuwa aibu ya mwaka.
Geneviv alitoka kwa hasira na kupotelea kusikojulikana akiwaacha Alice na Kim wanazozana.Alice alikuwa akiporomosha matusi kwa Geneviv hali iliyomkera sana Kim, wakawa wanalumbana wenyewe kwa wenyewe. Kim alitaka kutoka kumuwahi Geneviv lakini Alice alimuwahi na kufunga mlango kwa funguo kisha akazitupia chini ya kitanda. Ikawa mshike mshike. Geneviv alikuwa ameumia mno kwani hakutegemea kuyaona yale aliyoyaona kwa Alice na Kim hasa ukizingatia jinsi alivyokuwa akimhusudu Kim. Akili yake iliacha kufanya kazi na akawa anafikiria kitu kimoja tu akilini mwake, kujiua.
“Nitaificha wapi aibu hii mimi? Bora kufa! Siwezi kuendelea kuishi! Bora kufa!” Alikuwa akijisemesha Geneviv huku akilia kama mtoto mdogo. Hakutaka kurudi kwa kina Kim tena, akaona bora aende kufia kwenye nyumba yao. Alitembea kwa haraka akikwepa kuonekana na mtu yeyote. Muda mfupi baadae akawa ameshafika kwenye nyumba yao. Hakuogopa tena uchawi ambao ndio uliowasababisha wahame kwenye nyumba ile. Akasukuma mlango na kuingia moja kwa moja mpaka ndani. Alipitiliza mpaka chumbani kwake, akajitupa kitandani na kuanza upya kulia.
Baada ya purukushani za muda mrefu, hatimaye Kim alifanikiwa kumzidi nguvu Alice na kutoka nje. Alianza kuhaha kumtafuta Geneviv akiwa hajui ameelekea wapi kwani ulikuwa umepita muda tangu alipoondoka na kuwaacha mle ndani na Alice. Alikimbia mpaka nyumbani kwao alikowakuta baba yake na Mama Geneviv wamekaa sebuleni.
“Geneviv amekuja huku?” Aliongea Kim kwa sauti kubwa huku akiwa anahema kwa nguvu. Bwana Magwaza na Bi Patricia waliokuwa wamezama kwenye mazungumzo yao ya kiutu uzima walishtushwa ana Kim, wakabaki kumshangaa.
Kilichowashangaza ni kwamba kwanza Kim aliyekuwa akilalamika usiku kuwa anaumwa kichwa alikuwa ameondoka hapo nyumbani Alfajiri na mapema bila hata kuaga, hali iliyowafanya wote wabaki roho juu. Kama hiyo haitoshi, Geneviv naye aliondoka katika mazingira ya kutatanisha akidai kuwa anaenda kumtafuta Kim. Sasa kitendo cha Kim kurudi mbiombio kiliwafanya wabaki wameduwaa.
“Mi si nilikwambia, hawa waache wenyewe wanajuana. Aliyekuwa anatafutwa ndio huyu na yeye anamtafuta mwenzake, ujana unawasumbua!” Aliongea Bwana Magwaza kwa masihara akimueleza Bi Patricia.
“Hapana! It seems ana tatizo huyu, hebu jaribu kuongea nae kwa upole utagundua kitu. Usipuuzie mambo namna hiyo”
Aliongea kwa busara mno Bi Patricia, na Bwana Magwaza akaupokea ushauri ule. Bi Patricia alikuwa na saikolojia kali ya kuwaelewa vijana kwani alishajifunza mengi kutoka kwa mwanae Geneviv. Aliinuka na kumshika mkono mwanae Kim wakaelekea chumbani kwake.
“Tell me Son! Whats wrong with you! You seems not to be alright. Tell me!” (Niambie mwanangu, una tatizo gani? Unaonekana hauko sawa. Niambie!) Bwana Magwaza alikuwa akizungumza na mwanae Kim kwa upole sana. Ilibidi Kim amueleze baba yake tukio lililotokea alfajiri hiyo. Alimueleza kila kitu maka jinsi Geneviv alivyowafuma wakiwa na Alice.
“Come on son! Why do you hurt her while you know she is mentally stressed and she has not recovered fully?” (Kwa nini unamuumiza mwenzio wakati unajua fika kuwa akili yake bado haijatulia na bado hajapona vizuri?) Alihoji Bwana Magwaza huku akijishika mikono kichwani. Sio siri na yeye aliishiwa nguvu. Alitoka na kumuacha Kim chumbani, akaenda kumuelezea Bi Patricia.
*****
Baada ya kulia kwa muda mrefu, Geneviv aliinuka na kwenda kwenye duka la madawa lililokuwa jirani na pale nyumbani kwao. Alitaka kununua idadi kubwa ya vidonge vya dawa aina ya Quinine.
“Dawa zote hizi za nini Geneviv?”
Aliuliza yule muuzaji wa duka la madawa kwani alishtushwa na kiwango cha
dawa alizokuwa anazitaka Geneviv.
Ilibidi Geneviv adanganye kuwa bado yeye na mama yake wanaumwa kwa hiyo hizo dawa zilikuwa ni kwa ajili yao wote wawili. Yule muuzaji aliukubali uongo wa Geneviv, na akampatia dawa alizokuwa anazitaka. Baada ya kufanikiwa kupata vidonge Thelathini vya Quinine, Geneviv alirudi kwa haraka mpaka chumbani kwake. Akachukua kalamu na karatasi na kuandika ujumbe mfupi, kisha akauweka juu ya meza. Akajifungia kwa ndani.
Baada ya Bi Patricia kusimuliwa na Bwana Magwaza kilichokuwa kinaendelea baina ya Kim na Geneviv, alijikuta akinyong’onyea mwili mzima. Kengere ya hatari ililia kichwani mwake na akajua kwa vyovyote lazima Geneviv ataamua kuchukua uamuzi wa kujidhuru kwani alikuwa akimpenda sana Kim.
“Oooh My God! She may harm herself, She is real in love with Kim. I don’t know what to do! ( Mungu wangu! Lazima atajidhuru tu, anampenda sana Kim! Hata sijui nini cha kufanya). Aliongea Bi Patricia huku akianza kutokwa na machozi. Hakutaka kuona mwanae akiigia matatizoni tena.
Aliinuka kwa haraka kutoka pale alipokuwa amekaa na kwa kasi ya ajabu akatoka na kuanza kukimbia kuelekea nyumbani kwake alikohisi lazima Geneviv ndio atakuwa amekimbilia. Njiani alikuwa akimuomba Mungu amkute salama Geneviv kwani alikuwa na uhakika kuwa lazima atajifanya kitu mbaya kwa jinsi alivyokuwa akimpenda Kim.
********
Katika ujumbe aliouandika Geneviv, alisisitiza kuwa ameamua kuchukua uamuzi wa kujitoa roho baada ya kuumizwa na mtu aliyetegemea aje kuja baba wa watoto wake, Kim. Alizidi kusisitiza kuwa rafiki yake Alice amechangia kwa kiasi kikubwa yeye kufikia uamuzi ule wa kujitoa roho. Aliuweka ujumbe ule mahali ambapo ingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kuuona kwa urahisi.
Alichukua glasi ya maji na kumeza idadi kubwa ya vidonge, kisha akajilaza kitandani na kutulia kimya.haikupita muda akaanza kusikia kizunguzungu kikali kilichoambatana na maumivu makali ya tumbo na kichwa. Akawa anajinyonga nyonga huku povu jingi likimtoka mdomoni na puani.
Bi Patricia alikuwa akikimbia njia nzima kiasi cha kuwafanya watu waliomuona kuhisi amerudiwa na uendawazimu wake. Bwana Magwaza naye alitoka na kuanza kumfuata Bi Patricia kwa nyuma. Kim naye hakutaka kubaki nyuma. Kwa aibu kubwa akwa anawafuata kwa nyuma huku akijificha ficha kwani alitambua fika kuwa yeye ndio chanzo cha yote yale. Alijihisi mkosefu sana na akwa anamuomba Mungu wake wamkute Geneviv akiwa salama ili apate japo nafasi ya kumuomba radhi kwa mara ya mwisho.
Muda mfupi baadae, Bi Patricia alikuwa ameshawasili kwenye nyumba yao. Alifungua mlango wa nje lakini akagundua kuwa ulikuwa umefungwa kwa ndani. Alijaribu kuutingisha kwa nguvu bila ya mafanikio. Akazidi kuchanganyikiwa. Muda mfupi baadae bwana Magwaza alikuwa ameshafika na kwa pamoja wakasaidiana kuuvunja mlango na kuingia ndani. Walipofika sebuleni walisikia sauti ya mtu akikoroma kwa nguvu kutoka kwenye chumba cha Geneviv.
Waliusogelea mlango na kujaribu kuufungua lakini nao ulikuwa umefungwa kwa ndani. Ilibidi nguvu kubwa itumike kuuvunja kwani ulikuwa umefungwa kwa vitasa vyote kwa upande wa ndani. Baada ya purukushani nzito hatimaye walifanikiwa kuuvunja na kuingia ndani. Hakuna aliyeamini walichokiona. Geneviv alikuwa akijinyonganyonga kitandani kwa maumivu makali aliyokuwa anayasikia baada ya kunywa idadi kubwa ya vidonge kwa lengo la kujiua. Povu lilikuwa likimtoka kwa wingi mdomoni na puani na alikuwa akikoroma kwa nguvu kama anayetaka kukata roho.
Wote walichanganyikiwa mno na wakawa wanatafuta mbinu ya kumuokoa haraka kabla hajakata roho. Muda mchache baadae, Kim naye aliingia na kujionea kwa macho yake kilichokuwa kikiendelea. Bwana Magwaza alimuinua Geneviv akisaidiwa na Bi Patricia na wakatoka nje na kuanza kutafuta usafiri wa haraka wa kuwawahisha Hospitali ili kunusuru maisha ya Geneviv.
Wote walipotoka, Kim alibaki peke yake mle ndani akiwa haamini kuwa ni kweli Geneviv ameamua kujitoa uhai kwa ajili yake. Alijihisi ni mwenye hatia kubwa moyoni mwake na akabaki kujiuliza imekuwaje kwani kila kitu kilikuwa kikitokea kwa kasi sana kiasi cha kumfanya ashindwe kuelewa.
Aliendelea kukitazama kitanda alichokuwa amelala Geneviv, huku idadi kubwa ya vidonge vikiwa vimetapakaa chini. Alipoendela kuchunguza huku na kule alikutana na ujumbe uliokuwa umeandikwa na Geneviv.
Aliinama na kuanza kuusoma. Yalikuwa ni maneno mazito aliyoyaandika Geneviv kabla hajafikia uamuzi wa kunywa sumu. Alikuwa ameeleza wazi kuwa ameamua kujiua baada ya kusalitiwa na Kim na Alice. Kim alibaki ametoa macho akiwa haamini. Kama ingetokea Geneviv akapoteza maisha, basi yeye ndio angekuwa mhusika wa kwanza. Alijikuta akijilaumu sana moyoni mwake, alishidwa kujizuia kulia kwa uchungu mkubwa. Alipiga magoti na kuanza kumuomba Mungu wake ayanusuru maisha ya Geneviv.
Bwana Magwaza na Bi Patricia walifanikiwa kumfikisha Geneviv kituo cha afya kilichokuwa jirani.
“Emetic serum! Inject her on blood venules for quick feedback!”
Daktari wa zamu alikuwa akiwaamuru manesi wake wampe haraka dawa ya kumtapisha sumu aliyokunywa kupitia mishipa yake ya damu. Wengine wakawa wanahangaika kumnywesha maziwa kwa nguvu ili kupunguza makali ya sumu ambayo sasa ilikuwa imeanza kukolea mwilini.
Pamoja na kuhangaika kwa muda mrefu, hali ya Geneviv ilizidi kuwa mbaya na sasa uhai wake ukawa mashakani. Ilibidi yule daktari awape rufaa ya kwenda Hospitali kubwa kwani yeye pamoja na manesi wake walionekana kushindwa.
Alipakiwa kwenye gari la wagonjwa (AMBULANCE) na akawa anakimbizwa kwenye Hospitali kuu ya Blaziniar. Ndani ya gari la wagonjwa, manesi wawili walikuwa wakizidi kuhangaika kuhakikisha wanaokoa uhai wa Geneviv.
Baada ya safari ya kasi iliyochukua karibu nusu saa, wakawa wamefika kwenye Hospitali kuu ya Blaziniar. Ambulance iliyombeba ilipiga honi mfululizo na kwa haraka manesi wakatoka na kuja kumshusha. Aliteremshwa na kitanda chake cha kwenye gari na akawa anakimbizwa kuelekea wodini.
Tofauti na mara zote, safari hii mama yake, Bi Patricia alikuwa ametulia kimya akitazama kila kilichokuwa kikiendelea. Hakulia wala kutoa hata tone la machozi. Alichukulia kama kila kitu ni cha kawaida, akawa anasubiri kuona nini hatma ya mwanae. Bwana magwaza ndiye aliyekuwa na wakati mgumu zaidi kwani alijua mwanae Kim ndio chanzo cha yote yale. Alijiapiza kuwa lazima afanye kila kinachowezekana kuhakikisha Geneviv anapona.
Baada ya kuingizwa wodini, Geneviv aliendelea kupatiwa tiba ya haraka kunusuru maisha yake. Madaktari walikuwa wakipigana vikumbo wao kwa wao, kila mmoja akijitahidi kwa kadri ya uwezo wake. Walikuwa wakimhangaikia sana Geneviv kwani wengi walikuwa wakimfahamu vizuri Bwana Magwaza, ambaye aliwaambia kuwa Geneviv ni binti yake.
“Usiwe na wasiwasi Mheshimiwa! Binti yako atapona tu. Tuachie kila kitu wala usiwe na hofu.” Daktari mmoja alikuwa akiongea na Bwana Magwaza, Bi Patricia akiwa nyuma yake. Aliwahakikishia kuwa atapona kwa kuwa alikuwa akipewa huduma ya uhakika. Bwana Magwaza alimshika mkono Bi Patricia na wakarudi kukaa kwenye viti vilivyokuwa pale mapokezi.
“Hivi unafikiri Geneviv akipona, kile ulichoniambia asubuhi kitawezekana?” Alihoji Bi Patricia akimkazia macho Bwana Magwaza. Hakuwa na jibu la haraka kwa swali lile, akabaki kubabaika. “Mimi na wewe tukiwa mke na mume, inamaanisha kuwa geneviv na Kim watakuwa dada na kaka, wakati huyu anataka kujiua kwa kuwa anataka aolewe na Kim! Don’t you see this as a serial confusion?” Bi Patricia alitoa hoja nzito na ya msingi akimuacha Bwana Magwaza akimkodolea macho kama asiyeelewa anachoambiwa.
“Mi nafikiri huu sio muda muafaka wa kulizungumzia hili. Tumuombee Geneviv apone kwanza mengine yatajiset baadaye.” Alijibu kwa Mkato Bwana Magwaza, kisha akageukia upande mwingine. Alichokisema Bi Patricia kilikuwa kimemuingia moyoni kisawasawa.
Nyumbani kwa kina Geneviv, Kim alikuwa bado ndani ya chumba cha Geneviv, akiwa amepiga magoti chini na kujikunyata, akilia na kumuombea Geneviv apone. Alizidi kulia kwani hakika hatia ya maisha ya Geneviv ilikuwa juu yake. Alijilaumu sana kwa kitendo chake cha kumfuata Alice chumbani kwake kwani hicho ndio kilikuwa chanzo cha yote hayo. Ilifika mahali akajiapiza kuwa endapo Geneviv angepoteza maisha, basi na yeye angejiua.
****
Baada ya tiba mfululizo, hali ya Geneviv ilibadilika na taratibu akaanza kupata nafuu. Madaktari waligundua tatizo kubwa sana kwenye mfumo wa fahamu wa Geneviv na wakawa wanahangaika kupunguza tatizo.
“ Tumegundua tatizo kubwa, kuna uwezekano mkubwa binti yako akapoteza uwezo wa kuona na kusikia kwani sumu ya Quinine imeshambulia vikali milango yake ya fahamu. Tuanaendelea kujtahidi kupunguza tatizo”
Whaaat? Ina maanisha Geneviv atakuwa ahwezi kusikia wala kuona? Oooh my God…”
Bi Patricia ugumu ulimuishia na akajikuta akianza kulia.
Kim aliendelea kuwaza kwa muda mrefu bila ya kupata jibu ya kilichotokea. Aliona kila kitu kama ni maluelue yanayotokea kwa kasi kubwa, akawa ni kama aliyechanganyikiwa. Aliendelea kukaa mle chumbani mwa Geneviv kwa muda mrefu akiwaza na kuwazua nini cha kufanya. Nafsi yake ilikuwa ikimsuta sana kwa kumsababishia Geneviv matatizo makubwa kama yale. Siku zote maishani mwake alikuwa akipigania kumuona Geneviv akifurahi na kusahau matatizo yote yaliyokuwa yanaiandama familia yao, lakini sasa alijikuta yeye ndio akiwa tatizo kubwa zaidi kwa Geneviv.
Aliendelea kulia kwa muda mrefu lakini bado hakuhisi ahueni yoyote moyoni mwake. Mara alikumbuka kitu ambacho ndicho alichokiona kinafaa zaidi kwa wakati ule. Akiwa shule alizoea kuwasikia vijana wenzake wakimweleza jinsi ambavyo madawa ya kulevya huweza kumfanya mtu kusahau shida zake zote. Aliona hicho ndio kitu pekee kitakachomfaa kwa wakati ule.
Hakuwahi hata mara moja kufikiria kuwa ipo siku atawaza kutumia madawa ya kulevya, lakini sasa aliona ni lazima afanye hivyo akiamini atakuwa amepunguza kwa kiasi kikubwa hofu, woga na mawazo yaliyokuwa yakimuandama akilini mwake juu ya yaliyompata Geneviv. Kilichomuumiza zaidi nai zile hisia za kujiona yeye ndio chanzo cha kila kitu kilichompata Geneviv. Alijikuta akijiingiza kwenye mtego hatari zaidi.
Bila ya kupoteza muda aliinuka na kuanza kutoka ndani ya ile nyumba ya kina Geneviv. Alienda mpaka kwenye kilinge kimoja walichokuwa wakishinda watoto wa mitaani wanaotumia madawa ya kulevya maarufu kama ‘mateja’ au ‘chokoraa’. Alipofika na yeye alijichanganya kati yao na akatoa pesa mfukoni mwake na kumpa kijana mmoja aliyekuwa anauza madawa, ambaye wenzake walikuwa wakimwita kwa jina lao walilozoea la ‘Pusha’.
Wengine walikuwa wakiendelea kuvuta bangi na kula unga (Cocaine) huku wakipiga stori zao na kufurahi. Kwa kuwa Kim hakuwahi hata mara moja kujichanganya nao zaidi ya kuwapita kwa mbali akitoka shule, wote walikuwa wakimtazama na kunong’onezana maneno ya chinichini.
Yule muuzaji wa dawa za kulevya, alikaa jirani na Kim na akawa anamfundisha namna ya kula unga baada ya kugundua kuwa alikuwa hajui kabisa.
“Mwanangu, acha ukuda, inatakiwa ufanye kama mimi, niangalie vizuri! Unanisoma?” Yule kijana muuza dawa za kulevya alikuwa akiongelea puani akimwonyesha Kim namna ya kuvuta unga.
Alimuelekeza namna ya kuvuta kwa kutumia pua, na taratibu Kim akawa anavuta. Kwa kuwa ilikuwa ni mara yake ya kwanza, baada ya kuvuta kidogo tu, alijikuta akiwa na hali ambayo hakuwahi kuihisi maishani mwake.
”Im flying without wings! Kumbe nilikuwa nikikosa vitu vizuri namna hii! Niongeze tena Bro!” Aliongea Kim kwa sauti ya kilevi kabisa. Akatoa hela na kumpa tena yule pusha, kasha akaongezewa mzigo. Wakiwa wanaendelea kupata dozi ya Cocain, Kim alishangaa kumuona mtu kama Alice akija kwenye lile kundi la wale vijana na kujichanganya nao.
Kwa kuwa tayari alikuwa ameshalewa, Alishindwa kuzingatia alichokiona, lakini aligundua kuwa ni kweli yule aliyemuona alikuwa ni Alice naye akija kununua madawa ya kulevya. Alijipenyeza katikati ya wale vijana ambao walionekana kuwa na uswahiba nae kwani wote walikuwa wakimuita kwa jina lake.
Akafika mpaka kwa yule muuzaji ‘Pusha’ na wakasalimiana kihuni kisha akakaa na kuagiza dozi yake. Alikuwa bado hajamuoana Kim kuwa yuko pale pale. Kim ambaye sasa alianza kuhisi mwili wote ukikosa nguvu na kuzingirwa na usingizi mzito hukufahamu zikimtoka. Aliinama na akawa anasinzia kutokana na kuzidiwa na dawa za kulevya.
“Oyaa, huyu si Kim mtoto wa mama?, ameanza lini kutumia mambo ya kikubwa kama haya, asije kutuletea msala hapa”
Alisikika kijana mmoja akiongea kwa kumdhihaki Kim ambaye sasa alikuwa amehama kwenye ulimwengu wa kawaida na kuzama ulevini. Hapo Ndipo Alice alipogundua kuwa Kim naye alikuwepo eneo lile, jirani kabisa na pale alpokuwa amekaa akiwa hoi kwa madawa ya kulevya.
Licha ya kushtushwa na uwepo wake pale, alijiona kama mshindi kwani aliona huo ni muda mwingine mzuri wa kumfaidi Kim, tena safari hii akiwa hajitambui kwa kula unga.
Alimsogelea pale alipokuwa amejiinamia, akamshika mkono na kumnyanyua, akawa anaondoka naye kumpeleka nyumbani kwake huku wale vijana wa kihuni wakishangilia kwa nguvu. Kim alikuwa hajielewi tena, akawa anamfuata Alice kama kondoo anayepelekwa machinjioni. Muda mfupi baadae wakawa tayari wamefika kwa Alice.
***
Hali ya Geneviv ilikuwa bado sio ya kuridhisha kwani licha ya kuendelea kupewa tiba mfululizo hakuweza hata kufumbua macho yake. Akawa amelala kama mfu, ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi kwenye Hospitali kuu ya Blaziniar. Madaktari waliendelea kumhangaikia lakini bado hali yake haikubadilika.
“Tulia mama Geneviv, unavyozidi kulia unamkosea Mungu wako, Amini yeye ana uwezo wa kumuokoa mwanao. Mangapi ameshakufanyia Ndio atashindwa hili! Tuliza moyo mpendwa.”
Bwana Magwaza alikuwa akimbembeleza Bi Patricia ambaye baada ya kuambiwa kuwa mwanae hatakuwa tena na uwezo wa kuona wala kusikia alianza kulia kama mtoto mdogo. Bwana Magwaza aliendelea kumbembeleza kwa upole wakiwa pale kwenye sehemu ya mapokezi. Bi Patricia alimuelewa na akaacha kulia akiamini kuwa lazima hilo jaribu nalo litapita kama mengine yote yalivyopita.
“Lakini Roho inaniuma sana mimi! Kwanini kila siku ni mimi tu, likiisha hili linaanza lingine, nimekuwa mtu wa kushinda Hospitali kila siku, mwisho wake si itakuwa ni uhai wangu kutoka! Eeh Mungu, kama kweli upo, nyoosha mkono wako kwangu na uniokoe.”
Alikuwa akiongea Bi Patricia kwa uchungu mno. Bwana Magwaza aliendelea kumfariji kwa karibu sana. Masaa yalizidi kwenda na hali ya Geneviv ikawa bado sio ya kuridhisha, ikabidi Bwana Magwaza amshawishi Bi Patricia waende kupumzika kidogo halafu wangerudi baadae kuendelea kumuuguza Geneviv. Bi patricia hakuwa mbishi tena kwani moyo wake ulionekana kufa ganzi. Wakatoka na kurudi nyumbani kwa Bwana Magwaza.
***
Baada ya Alice kumkuta Kim akiwa katika kijiwe cha watoto wa mitaani wanaotumia madawa ya kulevya, alifanikiwa kumchukua na kwenda naye nyumbani kwake. Kwa kuwa Kim alikuwa hajitambui baada ya kuvuta dozi kubwa ya madawa ya kulevya kwa mara ya kwanza, Alice alipata nafasi nyingine ya kufanya alichokitaka kwa Kim. Alimuingiza mpaka ndani na kuanza kumwagia maji ya baridi kupunguza nguvu ya madawa aliyobwia. Baada ya Kim kurudiwa kidogo na fahamu zake, alimvua nguo zote na kumlaza juu ya kitanda chake, kisha naye akavua za kwake.
Ilivyoonyesha, Alice alikuwa amenogewa na mchezo waliokuwa wakiufanya na Kim kwani kama lengo lake lilikuwa ni kulipa kisasi kwa Geneviv, tayari hilo alishalifanikisha lakini bado aliendelea kumganda Kim kama Ruba, akitumia udhaifu wake kama silaha ya kumnasa kirahisi. Waliendelea na mchezo wao kwa muda mrefu mpaka jioni kabisa, Kim akiwa hana fahamu za kutosha baada ya kula unga mwingi. Fahamu zilipokuja kumrudia kisawasawa alijikuta akiwa amekumbatiwa kwa nguvu na Alice, wote wakiwa watupu. Akajua kwa mara nyingine tena amenasa mikononi mwa Alice na kuangukia dhambini.
Safari hii hakuwa mkali tena kama ilivyokuwa awali, kwani alijua kupanic kwake badala ya kupunguza matatizo, mara zote kulikuwa kukimwongezea matatizo.
“Kim, najua nakufanyia kitu ambacho hukifurahii kabisa, lakini ukweli ni kwamba na mimi sipendi kukufanyia hivi ila moyo wangu ndio unaonituma Kim. Najua kwa tabia zangu sistahili kuwa mpenzi wako, lakini nilishakwambia Kim, ukinikubali nitaacha kila kitu nilichokuwa nakifanya.”
Alice alikuwa akiongea kwa hisia kali akiwa amelala kifuani kwa Kim. Aliyalazimisha machozi kutoka kwenye macho yae ili Kim aamini kile alichokuwa anamwambia. Alizidi kulalama kimahaba…
“Namimi nina haki ya kupendwa Kim hata kama nilikuwa changudoa! Naahidi nitalitunza penzi lako kwani umenionyesha ulimwengu tofauti maishani mwangu, sikuwahi kumpenda yeyote, nilikuwa natafuta pesa tu Kim, ila kwako nakiri kuwa nakupenda kwa dhati na nataka nikuzalie watoto”
Maneno yale yote aliyokuwa anayatoa Alice, hayakumwingia Kim ambaye sasa alikuwa akiwaza hatma ya Geneviv huko Hospitali. Madawa ya kulevya aliyoamini yangemsahaulisha matatizo yake, yalimfanya aangukie tena mikononi mwa Alice na kujikuta akirudia mchezo ule ule uliomfanya Geneviv akafikia uamuzi wa kujitoa roho. Alikuwa akikumbuka jinsi Geneviv alivyoumia alipowakuta alfajiri wakiwa ndani ya chumba hicho hicho. Kumbukumbu zile zilimfanya ashindwe kuyazuia machozi. Alice akawa anamfuta na kuzidi kumbembeleza akihisi alikuwa akitokwa na machozi baada ya kuguswa na kile alichokuwa anamueleza.
“Im sorry Geneviv, I didn’t intend to hurt you! Forgive me my Queen! I will never do this anymore” ( Nisamehe Geneviv, sikukusudia kukuumiza, nisamehe malikia wangu! Sitarudia tena) Alikuwa akilalamika Kim kwa uchungu, hali iliyomkasirisha sana Alice. Alitambua fika kuwa Kim alimpenda Geneviv kuliko yeye. Hakukata tamaa, akawa anajiapiza kuwa lazima ayabadili mawazo ya Kim mpaka amsahau Geneviv.
Masaa yalizidi kuyoyoma na giza likaanza kuingia, Kim akiwa bado ndani ya chumba cha Alice. Alitamani kupata tena dozi nyingine ya madawa ya kulevya kwani hisia zilizokuwa zinapita akilini mwake zilikuwa zikimuumiza sana. Alice alilitambua hilo na akainuka na kwenda kumletea unga (Cocaine) aliyokuwa ameificha kwenye kimkoba chake kidogo. Walisaidiana kuvuta na baada ya sekude chache, wakapitiwa na usingizi mzito.
Baada ya Bwana Magwaza na Bi Patricia kufika nyumbani kwao, walianza kazi nyingine ya kumtafuta Kim ambaye haikufahamika yuko wapi kwani tayari giza lilishaingia.
“Huyu ni mtoto wa kiume, achana nae atarudi mwenyewe nyumbani.” Aliongea Bwana Magwaza kumtuliza Bi Patricia ambaye alishaanza kuingiwa upya na wasiwasi. Waliandaa chakula cha mgonjwa, kisha wakajiandaa na kurudi tena Hospitali. Bwana Magwaza alikuwa bega kwa bega na Bi patricia na alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote kumsahaulisha matatizo yake.
Baada ya kupitiwa na usingizi mzito kwa muda mrefu, Alice alikuwa wa kwanza kushtuka kabla ya Kim aliyekuwa bado anakoroma. Akawa anapanga mikakati ya kufanya ili kuhakikisha Kim hamkumbuki tena Geneviv. Aliona njia bora ni kwenda kummaliza kulekule Hospitali ili kuwa na uhakika wa kumpata Kim kwa asilimia mia moja kwani aliamini Geneviv ndio kikwazo pekee kwake. Akawa anapanga mkakati wa jinsi ya kwenda kutekeleza azma yake hiyo.
********
Bi Patricia na Bwana Magwaza wanaendelea kukaa Hospitali kwa muda mrefu wakimuuguza Geneviv ambaye bado ana hali mbaya kwani tangu alipofikishwa Hospitali hapo, alikuwa bado hajarudiwa na fahamu zake na madaktari walishasema kuwa hata kama angepona, angepoteza kabisa uwezo wa kuona na kusikia. Waliendelea kujadiliana nini cha kufanya ili kunusuru hali yake na Bwana Magwaza akawa na wazo jipya.
“Inawezekana bado nguvu za kichawi za ndugu zenu zinawaandama, mi nafikiri kitu muhimu nikafuatilie taratibu za kuwatoa Bwana Magafu na ukoo mzima gerezani kwani naamini kwa siku hizi walizokaa lupango, hawataweza kurudia tena kufanya ujinga wao, nikishakamilisha hili itabidi tumpeleke Geneviv kanisani pamoja na wewe mkaombewe ili mikosi kama hii isiwarudie tena.”
Bi Patricia alikubaliana na wazo lile na akamruhusu Bwana Magwaza aendelee na taratibu zote.
Bwana Magwaza aliaga na kuondoka akimuacha Bi Patricia akiendelea kumuangalia mwanae pale wodini. Alikuwa akiendelea kusali kimoyomoyo ili apone, na zaidi alifurahia kitendo cha Bwana Magwaza kwenda kuwatoa gerezani ndugu zake kwani aliamini mikosi yote ingeisha. Muda mfupi tangu Bwana Magwaza aondoke, Kim alifika Hospitali huku akiwa na wasiwasi mkubwa. Aliuliza mapokezi na akaelekezwa wodi aliyokuwa amelazwa Geneviv, na kwa unyonge mkubwa akawa anatembea kuelekea wodini.
Bi Patricia aliwahi kumuona kabla yeye hajawaona, na kwa kumtazama tu, alitambua kilichokuwa ndani ya mawazo yake. Alimuona jinsi alivyokuwa akisutwa na nafsi yake kwa matatizo aliyomsababishia Geneviv. Ilibidi Bi Patricia ageuke kuwa mshauri nasaha kwani aliamini Kim hakufanya vile kwa makusudi, na hata kama ilitokea basi ilikuwa ni bahati mbaya kwani siku zote yeye ndio alikuwa mfariji mkuu wa Geneviv.
“Usiumie sana mwanangu! Mungu ana kusudi lake kwa kila jambo. Geneviv atapona na haya yote yatapita. Usijiumize nafsi yako bure, muombe Mungu wako akusamehe na muombee mwenzio apone.” Bi Patricia alikuwa akizidi kumpa somo Kim ambaye kila neno lililotoka kwa Bi Patricia lilikuwa likiuchoma mno moyo wake. Akawa anabubujikwa na machozi kwa wingi wakati akimtazama Geneviv aliyekuwa amelala kama mfu juu ya kitanda cha wagonjwa.
Hakuweza kufumbua macho wala kugeuka, mwili wake ulikuwa umetulia tuli. Hali ile ilizidi kumtia uchungu mkali na akajikuta akilia kwa sauti, hali iliyomlazimu Bi Patricia amshike mkono na kutoka nae nje. Walienda kukaa kweye Bustani ya maua iliyokuwa ndani ya ile Hospitali na Bi Patricia akawa anazidi kumfariji Kim.
***
Baada ya Kim kuwahi kuondoka asubuhi bila kuaga, Alice naye alijitayarisha haraka na akawa anamfuata nyuma nyuma bila ya Kim kufahamu kuwa anafuatiliwa. Aliamini kuwa kwa vyovyote atakuwa anaenda Hospitali kumuona Geneviv, akaona huo ndio muda muafaka wa Kwenda kummaliza Geneviv.
Alichukua bomba la sindano kisha akaweka kiasi kikubwa cha Cocaine aliyokuwa nayo ndani ya chumba chake. Aliamini kabisa kuwa kwa kiwango kile alichokuwa amekiweka kwenye bomba la sindano, endapo angepata nafasi ya kumchoma Geneviv lazima angekufa haraka kwani madawa ya kulevya na dawa za Hospitali vikichanganywa pamoja vilikuwa vikitengeneza sumu hatari.
Aliendelea kumfuata nyuma nyuma Kim mpaka walipofika Hospitali. Akawa makini kumtazama angeingia wodi gani. Baada ya kumuona akiuliza pale mapokezi, naye alijichanganya kwa watu akijificha Kim asije akamuona. Alimsindikiza kwa macho mpaka alioingia wodini. Akajua kazi yake inaelekea kukamilika. Aliendelea kukaa pale mapokezi kwa muda, akikodolea macho mlango wa ile wodi aliyoingia Kim. Roho ya kishetani ilikuwa imemuingia na hakuwa na huruma tena.
Baada ya muda mchache, alimuona Kim akitoka akiwa ameshikwa mkono na mwanamke ambae alimtambua mara moja kuwa ni mama yake Geneviv. Alishusha pumzi ndefu kisha akageukia upande mwingine kujificha asionekane usoni. Aliendelea kuwatazama kwa jicho la wizi mpaka walipopita jirani kabisa na pale alipokuwa amekaa, wakielekea nje. Aliendelea kuwasindikiza kwa macho mpaka alipowaona wakikaa kwenye bustani ya maua iliyokuwa nje ya ile wodi.
Alipohakikisha wametoka kabisa, aliinuka kwa haraka na kuanza kuelekea kwenye ile wodi aliyokuwa amelazwa Geneviv. Alifungua mlango ambao ulikuwa umeegeshwa na moja kwa moja macho yake yakatua juu ya kitanda alichokuwa amelazwa Geneviv huku dripu za dawa zikiendelea kutiririka kuingia mishipani mwake. Alishusha pumzi ndefu na akawa anakisogelea kile kitanda taratibu. Alisogea mpaka jirani kabisa, akawa anamtazama Geneviv aliyekuwa hana fahamu kabisa juu ya kilichokuwa kinaendelea. Alitoa bomba la sindano kutoka kwenye kimkoba chake kidogo na kuanza kulitikisa kwa nguvu kuchanganya ile sumu iliyokuwa ndani yake.
“Wewe ni rafiki yangu kipenzi Geneviv, roho inaniuma sana lakini sina cha kufanya. Ni lazima ufe ili nipate nafasi ya kuwa na Kim. Nampenda sana Kim na nataka awe baba wa watoto wangu. Buriani Geneviv!” Aliongea Alice kwa sauti ya chini, kisha akatoboa sehemu ndogo ya dripu ya dawa iliyokuwa ikitiririka kuingia mwilini mwa Geneviv. Aliichanganya ile dawa na Cocaine iliyokuwa kwenye bomba la sindano. Akaitingisha kwa nguvu kuhakikisha imechanganyikana vizuri, mchanganyiko ule hatari ukawa unatiririka kuingia mishipani mwa Geneviv.
Kwa kasi ya ajabu akatoka wodini na kuanza kuharakisha kutafuta njia ya kutokea nje ya Hospitali ile bila ya kushtukiwa na mtu yeyote. Alifanikiwa na muda mfupi baade akawa kwenye geti la nyuma la kutokea nje. Mlinzi alimsimamisha na kumuuliza kwa nini alikuwa akipitia mlango wa nyuma wakati geti la mbele lilikuwa wazi.
***
Bi Patricia hakuwa na habari juu ya kilichokuwa kikiendelea wodini alikomuacha mwanae Geneviv. Alikuwa akizidi kumbembeleza Kim ambaye naye alikuwa akizidi kulia kwani hali aliyomuona nayo Geneviv ilimuumiza sana roho yake. Baada ya kubembelezwa na kupewa faraja kwa muda, alianza kurudi kwenye hali yake ya kawaida. Mara walishtukia kuona manesi wakikimbia kuelekea kwenye chumba alicholazwa Geneviv. Wakainuka kwa haraka na kuanza kukimbia kuelekea kule wodini, lakini walizuiwa mlangoni.
Geneviv alikuwa akitapatapa kitandani akiwa ni kama anayetaka kukata roho baada ya sumu iliyowekwa kwenye dripu yake ya dawa kusambaa mwilini. Manesi walikuwa wakihangaika kumuokoa wakiwa hawajui ni nani aliyefanya unyama ule. Cha ajabu ni kwamba, wakati Geneviv akitapatapa, aliweza kutoa sauti na kufumbua macho yake, hali ambayo haikuwezekana kabla ya hapo. Madaktari walitoa amri ya Geneviv kurudishwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi na kwa haraka aliwekwa juu ya kitanda chenye magurudumu na akawa anakimbizwa ICU.
“Its wonderfull that instead of killing her, it makes her recover her mental ability” ( Ni maajabu kuwa badala ya kumuua, sumu aliyowekewa imemrejeshea fahamu zake). Madaktari walikuwa wakijadiliana wakati wakichunguza ni aina gani ya sumu ilichanganywa kwenye dripu la mgonjwa Geneviv. Waliendelea kuua makali ya ile sumu, na katika hali ya kushangaza zaidi, makali ya sumu yalipoisha, Geneviv alikuwa amefumbua macho na akawa analia akiomba mama yake aletwe. Kila mtu mle wodini alibaki kuduwaa kwani hali kama ile haikuwahi kutokea.
Alirudishwa kwenye wodi aliyokuwa amelazwa awali, lakini safari hii ulinzi uliongezwa mara dufu. Bi Patricia alizuiwa kabisa kuingia wodini na akawa amekaa eneo la mapokezi akiwa na Kim. Bwana Magwaza alipigiwa simu na muda mfupi baadae alifika Hospitali akiwa anahema kwa nguvu kwani alihisi mambo yameharibika. Alipofika aliwakuta Bi Patricia na Kim wakiwa pale mapokezi na wakamueleza kila kitu kilichotokea. Wote walibaki kushangaa kwani hawakuelewa ni nani aliyefanya kitendo kile.
Baada ya muda mfupi, daktari aliwaruhusu waingie wodini kumuona mgonjwa wao kwani alikuwa amepata nafuu kubwa ndani ya muda mfupi.
“Geneviv my queen, forgive me please! I will do this no more, ni shetani alinipitia…nisamehe tafadhali.” Alikuwa akilia Kim akiwa amepiga magoti pembeni ya kitanda cha Geneviv. Hakumjibu kitu zaidi ya kuendelea kumwaga machozi.
“Mwenzio anakuomba msamaha, maandiko matakatifu yanasema samehe saba mara sabini”. Bi Patricia alikuwa akimsaidia Kim kuomba msamaha kwa Geneviv, akiwa amemkumbatia mwanae. Bwana Magwaza alikuwa amesimama pembeni akisikiliza yote yaliyokuwa yanaendelea. Hakuwa na neno la kuongeza zaidi.
Wakiwa wanaendelea kuombana radhi, daktari aliiingia wodini na akawapa taarifa kuwa kuna binti amekamatwa na walinzi akijaribu kutoroka kupitia mlango wa nyuma, na ilivyoonyesha yeye ndiye aliyehusika kumuwekea mgonjwa sumu.
“Yuko hapa kwenye jengo la walinzi. Njooni mumuone labda mnaweza kumtambua.” Aliwataarifu daktari na wote wakatoka kwenda kumuona muuaji wao, wakiwaacha Kim na Geneviv peke yao wodini.
*****
Alipanga kuwalaghai walinzi hata ikibidi kwa kuwapa penzi lake, ilimradi tu wamuachie. Ilikuwa ni kama bahati kwake kwani wale walinzi waliondoka wote na kumuacha akiwa chini ya ulinzi wa mtu mmoja, ambaye naye alianza kuonyesha masihara kwa Alice. “Hapa hapa sifanyi makosa” Alijisemea kimoyomoyo Alice wakati akijiandaa kuanza kumtega yule mlinzi.
Baada ya kumfanyia vituko vya hapa na pale, mlinzi alijikuta akiingiwa na shetani na kutamani kuvunja amri ya sita na binti Alice. Kwa muonekano wa nje, usingeweza kumdhania Alice kuwa ni changudoa. Alionekana kama bado ni mwanafunzi tena ambaye bado ni mbichi kabisa. Alimzidishia vituko mlinzi mpaka akili yake ikawa imehama, akiwaza kitu kimoja tu akilini mwake, kumfaidi Alice.
Alice alijirahisisha kama kawaida yake, yule mlinzi akamkumbatia kwa staili ya kutaka kuvunja amri ya sita. Hakulaza damu, akili yake ikawa inacheza kama Kompyuta. Mikono yake aliingiza kiufundi mifukoni mwa mlinzi na akawa anatafuta funguo za mlango wa kutokea nje. Baada ya mlinzi kuzidiwa, alimuomba Alice ampe hisani, naye bila ya hiana akakubali kwa sharti moja tu, la kuachiwa huru.
Mlinzi ambaye sasa alikuwa amerukwa na akili kabisa, alimvutia Alice kwenye chumba cha walinzi na kuanza kulifaidi tunda la mti uliokatazwa. Alice aliutumia vizuri muda ule na akafanikiwa kumchomoa funguo yule mlinzi kutoka kwenye mfuko wake. Wakati akiwa amezama kwenye huba la shetani, Alice alikurupuka kwa nguvu na kumrusha yule mlinzi pembeni. Alivaa nguo yake na ndani ya dakika chache baadae akawa kwenye mlango wa kutokea.
Aliingiza funguo kwenye kitasa na akafanikiwa kufungua na kutoroka akimuacha yule mlinzi akiwa bado hajitambui baada ya kuonjeshwa sumu ya penzi la Alice. Baada ya kufanikiwa kutoka, alikimbia mpaka ng’ambo ya pili ya barabara na kuanza kutimua mbio kwa kasi kurudi nyumbani kwake. Alimshukuru Mungu wake kwa kumuwezesha kutoroka na kuukwepa mkono wa Sheria.
Kwa kuwa hakuna aliyemuona kati ya Geneviv , Kim au wazazi wao, aliamini hawataweza kuja kugundua kuwa ni yeye ndiye aliyamfanyia Geneviv kitu kile. Akilini aliendelea kuamini kuwa sumu aliyomchoma Geneviv lazima ingemuua muda mchache baadae na yeye angepata nafasi ya kujivinjari na Kim kwa uhuru.
Kwa mara ya Kwanza alijikuta akiwa mtumwa wa penzi la Kim kiasi cha kuwa tayari kufanya lolote ili ampate. Alijishangaa kwa nini anase kimapenzi kwa Kim namna ile wakati tayari alikuwa ameshakutana na kulala na wanaume karibu wa kila aina. Alijiapiza kuwa atafanya lolote lile aliwezalo mpaka Kim awe wake na alijiapiza kuwa endapo Kim angemkubalia kabisa basi alikuwa tayari kuachana na biashara yake ya uchangudoa.
“Hata kama mimi ni changudoa, nahitaji kupendwa! Na mimi ni binadamu kama wengine ila ni hali ya maisha ndio iliyonilazimisha niwe hivi. Nikubali Kim uyaokoe maisha yangu.”
Alice alikuwa akiongea peke yake baada ya kufanikiwa kufika salama nyumbanii kwake. Alikuwa amejilaza kitandani huku machozi yakimtoka. Penzila kijana mdogo Kim lilikuwa limempagawisha kabisa na sasa akawa anamuwaza yeye tu akilini mwake. Alijua itakuwa ngumu sana kwa Kim kumkubali lakini alijipa moyo kuwa hakuna lisilowezekana.
*****
Bwana Magwaza akifuatana na Bi Paricia na mwanae Kim walitoka na kuelekea kwenye chumba cha daktari mkuu wakitaka kuonyeshwa mtuhumiwa aliyekamatwa kama wangeweza kumtambua.
“Kwani mlikuwa bado hamjaenda kumuona tangu muda ule?” Alihoji Daktari kwa mshangao kwani alishaagiza wapelekwe wakamuone muda mrefu uliopita. Aliinua mkonga wa simu yake ya mkononi na kumpigia mlinzi aliyekuwa zamu, ambaye kwa hofu kubwa alimwambia kuwa mtuhumiwa wao ametoroka katika mazingira ya kutatanisha na haifahamiki amekimbilia wapi.
Taarifa zile ziliwafanya wote wabaki wameduwaa. Ikabaki kuwa siri sirini juu ya mtu aliyetaka kumtoa Geneviv uhai. Akilini mwake Kim alishajua kuwa lazima ni Alice aliyafanya kitendo kile, akajikausha kama na yeye hafahamu kitu.
“Basi tumuachie Mungu, labda ni miujiza yake kwetu. Tumshukuru kwa kumbadili muuaji kuwa mponyaji” Aliongea Bi Patricia na wote wakatabasamu kwa furaha kutokana na kauli ile . Wakatoka na kurudi wodini ambako Geneviv alikuwa amelazwa. Walimkuta akiwa amekaa juu ya kitanda chake, akionesha kurudiwa na nguvu zake zote.
Taratibu za kutoka Hospitali zilifanywa na baada ya muda mfupi wakaruhusiwa. Daktari alimpa maelekezo Bi Patricia kuwa mgonjwa alitakiwa kupumzishwa kwa muda mrefu na akaonya kumuepusha na mambo yote ambayo yangeziumiza tena hisia zake. Daktari alisisitiza kuwa lazima akae mbali kabisa na mtu aliyemfaanya akataka kujiua vinginevyo angerudia tena jaribio lake kwani tayari akili yake ilishaathirika kisaikolojia.
Bi Patricia aliukubali ushauri wa daktari mbele ya Bwana Magwaza na akaahidi kuwa atafanya kila liwezekanalo ili kumlinda mwanae mpaka apone kabisa. Baada ya kutoka Hospitali, Bi Patricia alienda na mwanae Geneviv nyumbani kwake. Alimshukuru Bwana Magwaza kwa msaada mkubwa aliowapa ila akamuomba kuwa anahitaji kuwa na muda wa kukaa na binti yake ili wayaanze maisha mapya.
Bwana Magwaza alikubaliana na Bi Patricia na akamruhusu kwa moyo mkunjufu akiamini kuwa baada ya yote kupita na kusahaulika, lazima ndoto yake ya kuishi na Bi Patricia kama mkewe ingetimia. Kim hakutaka kabisa kuendelea kumuona Geneviv machoni kwa kuhofia kumuumiza tena. Alijiapiza kuwa huo ndio mwisho wake kukutana na Geneviv. Roho ilimuuma sana lakini hakuwa na jinsi, aliukubali ukweli na kujitenga mbali na Geneviv.
Geneviv na mama yake wakawa wameyaanza maisha mapya ndani ya nyumba Yao, huku Kim na baba yake nao wakiendelea na maisha yao kama kawaida.
Pamoja na Geneviv na mama yake kuamua kuanza ukurasa mpya wa maisha na kusahau kila kitu, bado akili ya Geneviv ilikuwa haitulii kila alipomfikiria Kim, ambaye sasa alikuwa amebadilika kabisa. Kim hakuwa tena yule aliyemfahamu. Hakuenda tena kumtembelea nyumbani kwao na hakupata hata muda wa kuagana naye. Alikuwa ameamua kuyaanza maisha mapya kivyake, maisha tofauti kabisa na aliyozoea kuyaishi.
“Mwanangu we tulia na Mshukuru Mungu kwa kila kitu. Huenda Mungu hakupanga wewe uwe na Kim na ndio maana haya yote yakatokea. Wewe ni mzuri na endelea kujitunza utampata tu atakayekufaa maishani.” Bi patricia alikuwa akimpa moyo mwanae baada ya kuona alivyoanza kuhangaika kumtafuta Kim. Alishindwa kuzidhibiti hisia zake, hali iliyomfanya mama yake awe na kazi ya ziada.
Siku zilizidi kwenda na taratibu Geneviv akaanza kumsahau Kim mawazoni mwake. Baada ya mama yake kuona kuwa ameshaanza kurudi kwenye hali yake ya kawaida, alianza kumfanyia mipango ya kuanza shule ikiwa ni njia ya kumfanya asahau kabisa matatizo aliyopitia masihani mwake.
“Cant Believe it that im going to start Secondary education! very funny! (Siamini kama ni kweli naenda kuanza sekondari mimi! Furaha iliyoje!) Aliongea Geneviv kwa furaha wakati mama yake akimpa taarifa kuwa anatakiwa kujiandaa kujiunga na kidato cha kwanza siku chache zijazo.
Kwa upande wa Kim, mambo yalikuwa tofauti sana,kwani hisia za kushtakiwa na dhamira zilizidi kumsumbua na kumfanya ajione kama mkosaji sana hapa duniani. Hali hiyo ilimfanya aanze kuonesha mabadiliko makubwa sana ya kitabia ambayo baba yake, Mzee Magwaza aliweza kuyagundua waziwazi.
Alianza kuchelewa kurudi nyumbani na akawa akirudi anapitiliza kwenda kulala. Hakuwahi kuwa na tabia kama hiyo hata siku moja. Mabadiliko haya yalianza siku Geneviv alipotaka kujiua kwa ajili yake.
“Son!, you seems not to be alright! You come back home in mid-nights and you behave like a hooligan. Tell me what is weighing in your mind” (Mwanangu, unaonekana hauko sawa! Unarudi nyumbani usiku wa manane na umeanza kuwa kama mhuni hivi. Niambie nini kinachokusumbua mawazoni mwako.”
Bwana Magwaza alikuwa amemkalisha mwanae Kim akimdadisi sababu za kubadilika kwake kitabia. Kim hakuwa na jibu zaidi ya kuinama chini akionekana kuzama kwenye dimbwi la mawazo. Akawa kila anapoulizwa kuhusu mienendo yake na kinachomsumbua akilini mwake, haelezi chochote zaidi ya kujiinamia chini.
Bwana Magwaza alitambua haraka kuwa mwanae amepatwa na msongo mkali wa mawazo na kulikuwa na kila dalili kuwa tukio la Geneviv kutaka kujiua kwa ajili yake lilikuwa limemuathiri sana kisaikolojia. Akawa anatafuta namna ya kumsaidia. Hakusikika kumtaja tena Geneviv kama ilivyokuwa hapo awali, hakutaka hata kwenda tena kumtembelea kwao. Ikawa muda wa mchana akitoka shuleni anajifungia chumbani kwake na jioni ikifika anaondoka kuelekea anakokujua mwenyewe mpaka usiku wa manane.
Ilibidi Bwana Magwaza kwa kushirikiana na Bi Patricia waanze kumfuatilia Kim kujua huwa anaenda wapi. Kazi haikuwa ngumu kwani siku chache baadae waligundua kuwa huwa anajichanganya na kundi la vijana wa mtaani kwao ambao wanafahamika vizuri kwa matumizi ya madawa ya kulevya,ikiwemo Cocaine na Marijuani.
“Kim is Dopping? Cant believe! This is a reason behind his behavioural changes…Oooh my God, he is finished.” (Kim anatumia madawa ya kulevya? Siamini! Hii ndio sababu ya kubadilika kwake kitabia…eeeh Mungu wangu, amekwisha).
Bwana Magwaza aliongea kwa kustaajabu mno baada ya kugundua kuwa kumbe mwanae alikuwa ameanza matumizi ya madawa ya kulevya. Bi Patricia alimtuliza sana na akamtahadharisha kuwa akitumia ukali kamwe hataweza kupata ufumbuzi wa tatizo lile la mwanae.
Kwa Bwana Magwaza hili lilikuwa jipya kabisa. Kwa haraka akaanza kutafuta njia ya kumnusuru mwanae kutoka kwenye tabia hatarishi kama ile. Baada ya kumbana sana, Kim alikiri kuwa ni kweli anatumia madawa ya kulevya na akaeleza wazi kuwa anafanya vile kwa sababuya Geneviv.
“Kwa sababu ya Geneviv kivipi? Yeye yuko salama kwao na wewe uko kwenu. Niambie kwa nini unafanya hivi?”
Kim aliendelea kusisitiza kauli yake kuwa Geneviv ndio sababu ya yeye kufanya vile. Bwana magwaza akaona njia bora ni kumhamishia mbali na pale nyumbani kwao ili amsahau kabisa Geneviv. Alifanya mipango haraka na akamtafutia shule ya Bweni nchini Kenya na baada ya siku chache taratibu zote zikawa tayari. Alisafirishwa kimya kimya mpaka jijini Nairobi kuyaanza maisha mapya kwenye shule ya bweni ya wavulana ya Kasarani Boyz Camp iliyoko katikati ya jiji la Nairobi. Hakupata hata nafasi ya kuwaaga marafiki zake.
Taratibu naye akaanza kumsahau Geneviv na akaachana na tabia ya matumizi ya madawa ya kulevya. Kwake ilikuwa rahisi kuacha matumizi ya madawa ya kulevya kwani yalikuwa vado hayajamkolea mwilini. Akabadilika na kurudi kuwa kama alivyokuwa zamani. Alisahau kila kitu na akawa akiutumia muda wake mwingi kujisomea. Baba yake alimwambia kuwa hatarudi nyumbani mpaka kipindi cha likizo ya mwezi Desemba na itakuwa hivyo mpaka atakapohitimu masomo yake.
Siku chache baada ya Kim kupelekwa jijini Nairobi, Geneviv alianza rasmi masomo yake ya sekondari, kidato cha kwanza kwenye shule ileile aliyokuwa anasoma Kim kabla hajahamishiwa Nairobi. Ilikuwa ni furaha ya aina yake kwa Geneviv kuungana na rafiki zake waliosoma pamoja shule ya msingi. Akawa anajihisi ni kama amezaliwa upya.
Bi Patricia naye aliamua kuanza kazi tofauti kabisa maishani mwake. Alifungua kituo cha kulelea watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu kwa kushirikiana na Bwana Magwaza. Baada ya muda mchache wakaanza kampeni maalum ya kuwakusanya watoto wote wenye shida. Walianza na Alice ambaye mwanzoni aliwasumbua sana lakini baadae wakafanikiwa kumtoa katika ajira mbaya ya uchangudoa na wakawa wanamfanyia utaratibu wa kuanza shule.
Bi Patricia hakusahau kijiji wanachoishi ndugu wa ukoo wa mume wake ambao kipindi cha mwanzo walitaka kumuua yeye na mwanae. Uhasama wao ulimalizwa kabisa baada ya wale wote waliokuwa gerezani kuachiwa huru. Waliendelea na maisha yao kama kawaida. Walianza kumuogopa na kumheshimu Bi Patricia baada ya kugundua kuwa ni mwanamke shupavu ambaye hayuko tayari kuyumbishwa na mtu. Migogoro yote ikamalizwa kwa tambiko maalum la kijadi na wakaanza ukurasa mpya kama hakuna kilichotokeaa kati yao.
Maisha yakarudi kuwa ya furaha na amani kama zamani. Uzuri wa Geneviv ukaanza kuchanua upya, safari hii akiwa ameongezeka na kuwa mkubwa. “Im now a beatiful lady” (Sasa nimekuwa binti mrembo). “Hebu niangalie mama” Geneviv alikuwa akimuonesha mama yake jinsi nguo zake za shule zilivyokuwa zinampendeza.Sitalia tena! I will shed no more tears! Aliongea Geneviv kwa hisia kali, wakakumbatiana kwa nguvu na mama yake.
******
Mwisho wa sehemu ya kwanza-The End of Episode I
Jiandae kusoma sehemu ya pili ya simulizi hii itakayokuwa inaitwa
My Beauty,My Grave! (Urembo wangu, Kaburi langu).
Coming soon…Stay blessed!
amenibarikihash@rocketmail.com
Newera7113.blogspot.com
+255 (0) 768540912.